Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

[emoji23] [emoji23] wazee wa kuonganisha dots.. Mimi sijui
Kama huyo ni ndg yangu kabisaaaaaaaaa
Na kesi hiyo naifahamu
Huyo Bwana anageukwa na ndg zake ambao wanaungana na mwanamke yeye anabaki peke ake

Kama ni yeye basi ndio huyo
 
Mtu ataambuwa ukweli wa Jambo lililotokea a to z bila kuficha na kila process nahifadhi Kama kumbukumbu za kila Jambo, na Wala sio sumu
Kuishi maisha huku ukitengeneza ushahidi wa kila kitu unachofanya na mumeo, ni bora usiolewe..!! Unaishi kwenye ndoa kama afisa mpelelezi wa mwenzio kila siku... yaani unaishi kama unaishi na mtuhumiwa...!! BORA USIOLEWE
 
Ndo msimamo wangu,,maisha mafupi kuanza kuishi kinafiki na kusubiri uzeeni akifa na ujana wake je?? Hizo hasira zitaishia wapi,, anakusaliti unajua unampiga matukio mpaka anainua mikono juu,
Tena wanaume walivyo na roho nyepesi, akipigwa tuiko la kuchapiwa mkewe huwa anavurugwa kweli kweli, na hakuna rangi wana acha kuona wallah. [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
That marriage is done.
Kuna kitu kimoja inabidi uweke akilini pia, kua sex sio love. Kuna mtu anaweza mpenda kabisa partner wake 100% ila bado akawa ana-have sex na watu nje, ila akirudi kwa partner anakua loyal na hataki hata kuachana wala nini. Sometimes sex is just sex. Ni maneno gumu kuyasikia ila kwa wanaume wengi ipo hivyo. Tatizo litakuja on bed ukiwa na jamaa unaimagine anatoa the same treatment kwa wanawake wengine inaku-turn off kabisa, hapo unahitaji therapy. Ila kupata mwanaume ambaye hatolala nje hata mara moja ni kitu kigumu mno, 1 in a million. Women do it as well
 
Mtoa mada nakushauri utafute mwanaume viwango vya juu kumzidi huyo mumeo,,mpimane mpe mchezo usiku kucha,
Tena wanaume walivyo na roho nyepesi, akipigwa tuiko la kuchapiwa mkewe huwa anavurugwa kweli kweli, na hakuna rangi wana acha kuona wallah. [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Ila wasome miandiko yao humu utadhani sio wao wanaojiua kisa wanawake
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] shem sio kila pambio linaloimbwa ulifikirie vibaya, mengine huwa tunaimba tukijazwa na roho.
Kuna siku niliimbiwa ekuemeee ekueme ghafla akaanza za Upendo Nkone na sijui nani yule anajiliza liza?... Kila nikijifukunyua sijui kosa langu, nikaona isiwe taabu saa tano asubuhi nikajitwisha huyo nae bar...hata sijui kesi iliishaje na hizo ekuemeee sizisikii tena zaidi ya "hapa nilipo mimi ni kwa neema za Mungu... "

Shemeji kaeni kikao muache hizo pambio mtatuua kwa visukari [emoji1][emoji1][emoji1]
 
Ndo msimamo wangu,,maisha mafupi kuanza kuishi kinafiki na kusubiri uzeeni akifa na ujana wake je?? Hizo hasira zitaishia wapi,, anakusaliti unajua unampiga matukio mpaka anainua mikono juu,
Mimi siwezi nafukia nafsi yangu nifuraishe jamii huku naumia ndani I will never, Kuna vitu vya kumvumilia mtu Kama maradhi, shida uchumi kuyumba na sio kuvumilia ujinga wa mtu kukuumiza hisia huwa inauma Sana Bora ivunjike mguu Kuna pain Killers sio mtu kukuumiza hisia zako hovyo. Na hisia zinauma jamani, Bora tu na Mimi nifanye yangu kwanza mda wa kumpenda mtu nautoa wapi Mimi. Acha niipende nafsi yangu na wanangu
 
Ukitoa hela Sina shida kabisa na Mambo yetu hawatajua, Sasa jifanye kichwa ngumu, utajuta kabisa hutaki kutoa matunzo natafta lawyer kabisa u sign, na nibahifadhi kumbukumbu nije kuwaambia jinsi baba alivogoma kuhudumia na ushahidi huu, usije sema niliwalisha sumu. Tumegombana Mimi na wewe kwanini utese watoto kwa kukataa kuwahudumia wao Wana kosa gani?
Hizo karata zichange vizuri haswa, uki mess up utakosa vyote, watoto wanakua, wanapata upeo na uelewa wa kuchakata mambo , hutoamini kitakacho tokea , uchange karata vizuri... unaweza dhani unajenga yakaja kukufikisha pabaya, wewe na baba watoto kwa watoto wenu thamana yenu kwao ni moja , watachakata taarifa, watapewa habari na ndugu marafik na watu wa karibu, chonde chonde incase ikawa hivyo changa karata vizuri..Omba Mungu yasitokee

nimesema hivyo Kwasababu nimekua kwenye mazingira yanayo karibia fanania
 
Back
Top Bottom