Wanawake wengi sana hawaogopi UKIMWI

Wanawake wengi sana hawaogopi UKIMWI

Baadhi yao wanasemaga zinawachubua, zinapasukia ndani, na pia hawasikii raha yoyote.
 
Maranyingi wadangaji ndio husisitiza matumizi ya condom. Demu wako au yule ambaye hupita naye mara kwa mara huwa kimyaa
 
Gender inequalities na financial disparities ni kati ya sababu kubwa zinazowafanya wanawake kutonegotiate namna ya kushiriki tendo la ndoa ili kujikinga na maambukizi ya ukimwi. Ni kweli takwimu zinaonesha idadi ya wanawake wanaoishi na vvu kusini mwa jangwa la Sahara ni kubwa kuliko idadi ya wanaume. Swali what should we do to close if not minimise the gape. Nafikiri Tanzania tumeanza vizuri kuchukua hatua ila hatua zaidi zinahitajika kwa kila familia kuzungumzia njia za kuepuka maambukizi na vijana kwenda kwenye majukwaa kwa wakati wao kuelimisha Umma. Ni rahisi sana kutotokomeza VVU kwa pamoja
 
Habari ndg zangu, nimeona bora tujuzane humu pengine tutapata ufumbuzi wa hili jambo.

Nimejaribu kuchunguza tangu nianze mambo ya mapenzi sijawahi kumsikia mwanamke ananisisitiza kuhusu kutumia kinga wakati wa mambo fulani kila mwanamke akiingia ndani mkafanya michezo yenu lakini linapofika suala la tendo mwanamke anakuwa kimyaaa hata ukamuuliza vipi tutumie au anakuambia sijui wewe mwenyewe.

Na nimejaribu kuwauliza wanaume wenzangu kuhusu hili nao majibu yao ni hivihivi kwamba wanawake wao huwa hawasisitizi uvaaji wa kinga

Mara tu ukijaribu kumuambia mbona hunisisitizi kuhusu kuvaa kinga? Wengi wao hujibu mimi naogopa mimba si UKIMWI kwani ni bora ungesema niogope malaria vipi watu wangu wa Jf mnalionaje hili?
Umenena Vyema Kabisa Kaka!Wanawake Wengi Sijui Huwa Wanarukwa Na Akili Maana Utakuta Ukimuuliza Vp Kuhusu Kondomu anakwambia Tusitumie Zitasababisha Niwashwe!
 
Wanaume tumepewa majukumu makubwa Sana na Mungu mojawapo ikiwa hilo la kumlinda mwanamke . Maamuzi mengi yanategemea mwanaume iwe home au job au popote pale... So let's be responsible guys . It's up to us . Ndio maana hata shetani alipitia kwa mwanamke pale KatiKa bustani ya edeni
Na si kumlinda mwanamke tu. Ila tumepewa jukumu la kulinda uhai..
 
mwanamke makini humgusi bila ya kifanyio,hiyo unayobeba ni mizigo ya kimboka imeshajikatia tamaa
 
Habari ndg zangu, nimeona bora tujuzane humu pengine tutapata ufumbuzi wa hili jambo.

Nimejaribu kuchunguza tangu nianze mambo ya mapenzi sijawahi kumsikia mwanamke ananisisitiza kuhusu kutumia kinga wakati wa mambo fulani kila mwanamke akiingia ndani mkafanya michezo yenu lakini linapofika suala la tendo mwanamke anakuwa kimyaaa hata ukamuuliza vipi tutumie au anakuambia sijui wewe mwenyewe.

Na nimejaribu kuwauliza wanaume wenzangu kuhusu hili nao majibu yao ni hivihivi kwamba wanawake wao huwa hawasisitizi uvaaji wa kinga

Mara tu ukijaribu kumuambia mbona hunisisitizi kuhusu kuvaa kinga? Wengi wao hujibu mimi naogopa mimba si UKIMWI kwani ni bora ungesema niogope malaria vipi watu wangu wa Jf mnalionaje hili?
Enzi sijatulia kitabia nilikutana na mwamke wa ajabu Sana, ile tunaingia Gest ghafla alifungua mkoba wake na kutoa vipimo vya UKIMWI kilichoendelea hapo subiri nitaleta uzi maalumu
 
Jua kutofautisha ..haya maneno ..mwanamke ,malaya .. Msichana na mdada
Hao wote kwa ujumla wao; malaya, wasichana na wadada ni wanawake tu.

Kwa muktadha wa mwandishi, hakuwa-group, yeye kapiga jumla jumla.

Linapokuja suala la kimapenzi, halina cha msichana, mdada wala malaya.
Nadhani tungejikita katika udadavuzi wa mambo tunayokutana nayo falaghani.

Mleta uzi aliyoyaongea yana ukweli.
Watu wengi wanapenda sana 'ngozi' kama ngozi, ina thamani ya kipekee.

Kwanza ngozi halisi kwa kuitazama hujenga taswira ya unachokiangalia, inavutia hata kupelekea kuanzisha mahusiano.

Pia ngozi kama chakula kwa kuliwa kama kitoweo, ina ladha tamu sana kushinda hata nyama, mf: ngozi ya samaki, kuku, nguruwe ama ng'ombe.

Ukija kwenye masuala ya mapenzi sasa, ngozi halisi(kavu) kwa kuwa ni 'nature' ina thamani na hisia zaidi kuliko hiyo ngozi bandia('ndom).
Mambo ya 'ulaku' wasibebeshwe lawama wanawake pekee, hilo ni janga la kihisia na ni la kidunia kila mtu linamhusu.

Utakuta watu wanaanza vizuri kwa kuvalishana hiyo mipira, lakini mwishoni kwenye umaliziaji hujiona kama wanajipunja, na kwa pamoja hukubaliana kuvua kwa hiyari, kwamba lolote na liwe ilimradi tendo limalizike kwa ufasaha.

Sasa hapo kuna mwanamke wa kulaumiwa!

Wengine kwa uelewa wa kuwa ngozi halisi ina raha zaidi, hujitoza gharama kubwa kwa hiyari yao kumrubuni mwanamke ili kufikia matamanio yao tofauti na gharama za kutumia hizo mnazozisema kinga.

Tena wanaume wengine wakiwa kwenye 'ninakutaka mode' husimangwa kabisa kuwa 'wewe baba, unaniaminije na wala hatujawahi kuonana hata siku moja'?
Utakuta njemba inapanda kijingajinga ikimpa marks za juu huyo mwanamke huku ikikoroma 'mimi nimepima juzi na ninajiamini, wewe nipe tu hivyohivyo...hag...hag...hag! Njemba ikielekea kwenye kilele cha kubembeleza!

Hili jambo limekaa kama vile chatu anavyowinda mbwa.
Chatu hutengeneza mazingira ambayo mbwa hujisogeza kuliwa kwa kuridhika mwenyewe, huku akielewa kabisa kuwa anaenda kumezwa, lakini huwa hana namna ya kujidhibiti na kuweza kutoroka mtego wa adui yake, hilo huwa ndiyo jinsi alivyojichagulia, kujisogeza ili aliwe, maana hakuna namna nyingine.

Na kwenye mapenzi iko hivyo, hakuna wa kulaumiwa kati ya mwanamke ama mwanaume maana ni janga la kihisia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom