Wanawake, oneeni huruma watoto wenu basi!!!!

Wanawake, oneeni huruma watoto wenu basi!!!!

Twin_Kids

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2016
Posts
4,000
Reaction score
5,969
Hivi, japo najua si mimi pekee, badhi ya wanawake, msio na chembe ya huruma kwa watoto wenu, japo mnasahau kuwa ipo siku mnacholingia hakitakuwa na thamani tena, mnafikilia kizazi mnachotengeneza!?

Nikiwa kama single father, nimejitahidi sana, na bado naendelea, ila wazee, ukiona mwanamke anakuleleawanao, kubali yaishe. Na waliokuza, wapeni maua yao. Single mothers, najua mmekuwa kama kila baya ni nyie, ila poleni na pigeni moyo konde, yataisha.

Siku zote ua nikiangalia vitoto vyangu,bado vidogo, huduma vipewe, havielewi unapataje, umekosaje,
Huyo huyo ndo baba ndo mama ndo kila kitu.

Mtu alie na sehemu, Dar; naomba anihifadhi japo miezi 3 tu. Ntakuwa nimejiimalishe niendelee kupambana, hali si shwali.



NB: Naona wengi wamenichukulia kama omba omba au mambo ndo mwisho kabisaaaa!! Nimemaanisha kama kuna mtu ambaye ana nyumba vacant, ambayo haina mtu.

Sijaomba kuishi kwa mtu na kumtegemea, nina kazi inayosiwezesha kulea, kilichogoma ni mahesabu tu kuyaweka sawa.
 
Duuh pole mkuu kwa changamoto yako sijawahi kusikia single faza analalamika ndo kwanza nasikia kwako.

Anyway pambana tu mzee
Tupo na sisi ndugu! Sema tu ni kama hivi unajikuta wiki inakata, usingizi hakuna, unakuwa huelewielewi. Wengine huhangaika kutuma tu matumizi, mengine wanakausha. Ila sasa, wale ambao ni kama single mother, kila kitu wewe tuuu, ni style hiyo
 
Tunaendelea kupata fundisho kupitia JF na maisha kwa ujumla

Zaeni mkiwa na uwezo wa kutunza watoto wenu tofauti na hapo sisiemu wataendelea kulaumiwa bure
Licha ya uwezo pia ni vyema mkakubaliana kuzaa. Haya mambo ya kutiana tu mimba bila mipango wala ndoa ndio mwanzo wa single parenting kitu ambacho kinamuuza mtoto ambaye ana haki ya kupata malezi ya baba na mama vilevile hakuwalazimisha mumzae
 
Peleka watoto kwa ndugu yako mwenye makazi rasmi wakati ukiangalia mipango mingine. Maisha ya mjini kumpa hifadhi stranger ni ngumu
Mkuu, umenena vema kwenye comment yako hapo juu. Unadhani, niliweza walipokua na mwaka mmoja, leo wamefikisha 3 ndo nifeli? Yaani wakose mama, wakose baba? Sijazaa mtu anilelee, japo labda bahati mbaya ni kuzaa na mtu asie na upendo, hata hao ndugu huenda nilichukua maamzi hayo kuepusha hizo lawama. Stranger ni binadamu kama wengine, kwa kidogo nikipatacho hata nikienda Kibiti watakua tu. Mzigo wangu, ntakomaa nao mkuu.
 
Huna dada...!!?
Mama, baba yako?
Shangazi yako au mama mdogo?
Bibi na babu hawa wawe wa mwisho.

Kuliko mtu asiyekufahamu akuhifadhi kwa miezi 3 borq hao ndugu zako wa damu na masimango juu hawatakukula ukakwisha.

Acha watoto kwa hao ndugu mmoja wapo wote kwa pamoja, nenda kasake tonge uwe unakuja kuwaona wanao kila wiki. Miezi mitatu ikifika uwe na kwako kwa kudumu uendelee kulea wanao.
 
Mkuu, umenena vema kwenye comment yako hapo juu. Unadhani, niliweza walipokua na mwaka mmoja, leo wamefikisha 3 ndo nifeli? Yaani wakose mama, wakose baba? Sijazaa mtu anilelee, japo labda bahati mbaya ni kuzaa na mtu asie na upendo, hata hao ndugu huenda nilichukua maamzi hayo kuepusha hizo lawama. Stranger ni binadamu kama wengine, kwa kidogo nikipatacho hata nikienda Kibiti watakua tu. Mzigo wangu, ntakomaa nao mkuu.

Jibu na maamuzi unayo hapa, uzi ufungwe.
 
Back
Top Bottom