Wanawake na magari

Wanawake na magari

Umenikumbusha sister angu mmoja alisha wahi kunokisha engine ya gari hata haina week... kisa kajifanya siku hiyo kufungua boneti kaweka maji kasahau kufungu mfuniko... kakanyaga mafuta na safar zake mpaka gari likazimika

Eeeeehhh huyo alitoa mpyaaa, tena umenikumbusha wengine wanaendesha gari kila siku ila ikija kulifanyia service anataka mwanaume ndo alipeleke gereji, au mwengine maji yameisha kwenye rejeta wala hashituki, mshale wa kuonyesha engine inapata moto uko juu kwenye red yeye wala hashituki anakanyaga mafuta tuu matokeo yake engine inachemsha yaani.
 
wengi wanajua kudrive tu tena hizo zenye automatic gear system akikanyaga mafuta hadi anafika. Hawana ujanja ikizngua wanajua wanaume watahusika hapo


ni kweli kabisa, ila niseme ukweli hata manua mie mwenyewe kuiendesha ilikuwa wakati wa driving school na pale unajua mwalimu anaibia kukusaidia kukanyaga clutch na break hivo leo ukinipa gari ya manual looh nahisi ntaiendesha kwa notsi za kwenye kidiary changu ambapo ni kwamba tuu siwezi iendesha looh.
 
ukisema hivo huwa nawaza, ikitokea mdada yuko mwenyewe kwenye gari anaenda mahali in between safari anapata break down na anakuwa kwenye mazingira ambayo hamna watu au ni nia ambayo haipiti watu na labda ni kapori ambapo inasadikika kuna nyoka au hata fisi ambao unajua wanadhuru na jua linazama akipiga simu fundi aje atengeneze ni siku ingine. Hapo ndo huwa nawaza bora mdada anayeendesha gari walau ajue kubadili tyre ili aweze kuendelea na safari au hata ajue kucheki kama maji kwenye rejeta yapo, maji ya wiper, ajue kucheki oil, awe anacheki maji kwenye betri kama ni betri ya maji au kuiangalia kama betri terminals zimekaza au ziko loose walau ile first aid ya gari ili zaidi ya hapo sasa ndo una rely kwa fundi.

Mkuu Kasinde
Hata wazazi nyumbani wanawagawanya watoto kwa vizawadi kutokana na jinsia. Mimi nina pacha wangu yeye ni KE, tulivyokua wadogo baba akileta zawadi basi mimi naletewa toy ya kigari na yeye analetewa kimdoli.

Hii inaonyesha dhahiri wadada na magari hasa kutengeneza sio mambo yao, wachache wanafanya.
 
Hahahahahahaa nimejikuta nacheka tuu looh,
Natamani itokee siku moja nikutane na mkaka awe mwenyewe kwenye gari halafu awe hawezi kubadili tairi halafu mie nimpe hiyo service ya kubadili tyre, natamani hiyo hali initokee


1. tie rod end/ball joint etc ikikatika sio mwanamke tu hata mwanaume huna ujanja,utapaki pembeni utaita wenye kazi yao....fundi labda wewe mwenyewe uwe fundi magari.

2.pancha inahitaji uzoefu,kuna wanaume wanapata pancha nao hawajui mpaka unamshtua kwahio unahitaji kauzoefu fulani kuhisi mabadiliko kwenye gari yako na si kila mtu ana uwezo huo.

kuna wanaume wengi tu hawawezi kubadili tairi,wakipata pancha utawaonea huruma wanavyohangaika wakikosa mtu wa kuwatolea....
 
Habari zenu wapendwa.
Nikiwa njiani leo kuelekea kazini kuna mama mmoja tyroad hand ikaachia tairi ya mbele kulia ikakaa migulu baja.

Nikiwa kwenye foleni mama akawasha hazard na kuchukua kilongalonga probably alikuwa anampigia husband au fundi.

Mbele kidogo nikiwa kwenye hizi barabara za vumbi maana tunapita huko kukwepa foleni njia kuu. Ikapita gari mama mwingine tairi ya mbele kushotoina pancha mama hana habari anakanyaga wese tuu.

Nikajikuta nawaza wanawake wanapenda magari na kuendesha kwa mbwembwe.

Issue inakuja gari ikiharibika inakabidhiwa mwanaume. Ni kudeka au ndo kawaida maana mie gari pancha nabadili mwenyewe, na vitu vidogovidogo.

Au kwakuwa mie sina husband nimejiseti tatizo likitokea ni langu.
vpi umerudi lini kutoka kwa Obama au unaongele ukiwa uko
 
we naweeee, leo ndo umegundua nina gari inamaana siku zote hizo ulijua nawazuga MMU, mie niandikacho ni real na huwa ni matukio ninayokutana nayo au yanayonitokea 90% mbona huku note kuwa sina husbendi umeona gari tuu, anyway as gari ndio hoja kuu lets go...... Asante kwa kunipa pongezi nimezipokea.

Hahah mi nimekupa pongezi tu bana ila nilijua hili ni gari la pili umenunua si lile la makrashi...

okeee ila wanatakiwa wajifunze walau kubadiri tairi au hata kuchokonoa betri ikiwa iko loose sio gari inazima unapigia fundi anakuja kusogeza betri tuu gari inawaka .....................

Mkifanya nyie kila kitu mafundi watakula wapi?

Mazoezi kama kawa nafanya siwezi kuacha, yameshakuwa sehemu ya maisha yangu na ratiba yangu ya kila siku. Na nimekuwa nikifanya kila siku kwa sababu siku hz bajaji zinaringa sana, so nikitoka nampita muuza matunda yuleeeeee motooo hadi morocco nakimbia mdogo mdogo from posta to morocco non stop karibuu

We mara kibao nimekwambia twende wote jogging lakini wanikimbia...

If u serious utanitafuta mwenyewe...
 
Nitapata wapi mie hela yakukodisha gari?Labda kama unipe lote lote......lol

bure inaua dada bora ubaki bila kuwa nalo, maana akikupa bure tuu ujue utarudi kwake kutaka hela ya mafuta, service, tairi zimekuwa kipara bora usilitamani la uligharamikie kwa heloa zako
 
Habari zenu wapendwa.
Issue inakuja gari ikiharibika inakabidhiwa mwanaume. Ni kudeka au ndo kawaida maana mie gari pancha nabadili mwenyewe, na vitu vidogovidogo.

Au kwakuwa mie sina husband nimejiseti tatizo likitokea ni langu.
lmi.jpg
 
hawajui ujanja unashuka kwenye gari tana kama umependeza wewe unafungua boneti unajifanya unaangalia angalia watakuja wanaume tu..... kama ni pancha unachukua jeki unajifanya kuanza kurekebisha aah bwana wakaka wa mjini wanajisogeza pole pole mtoto wa kike huku unatabasamu ..... wanawake wengi hatujui hata kukagua gari ni basi.... kazi ya wanaume hiii sisi ni kuendesha tu
mer.jpg
 
Habari zenu wapendwa.
Nikiwa njiani leo kuelekea kazini kuna mama mmoja tyroad hand ikaachia tairi ya mbele kulia ikakaa migulu baja.Nikiwa kwenye foleni mama akawasha hazard na kuchukua kilongalonga probably alikuwa anampigia husband au fundi.
stock-photo-woman-calling-for-assistance-with-flat-tire-on-car-in-the-city-126992561.jpg
 
mie nimeshauzoea usafirngu niliopewa na Mungu hapa napita njia tu
 
Back
Top Bottom