EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,356
Wanawake nchini Malawi wametishia kuandamana uchi kama "wamachinga" wa huko wataendelea kuwanyanyasa kisa kuvaa suruali, miniskirts na leggings. Bado haijajulikana ni kwa nini hasa Wamachinga hao wanawavua wanawake nguo lakini inasemekana kuwa wanapinga kuondolewa kwenye mitaa wanayofanyia biashara zao.
Lakini wengine wanadai wamachinga hao wanawavua nguo wanawake kwa sababu kuvaa suruali, mini-skirts na leggings kunadhalilisha wanaume. Pia wapo wanaodai wanafanya hivyo kupinga utawala mbaya wa Rais Bingu wa Mutharika. Wanadai kwa vile utawala wa Mutharika umepiga marufuku maandamano ya amani hawana jinsi ya ku-express jinsi utawala wake ulivyo mbovu zaidi ya kuwavua wanawake nguo.
Hadi mwaka 1996 ilikuwa marufuku kwa mwanamke kuvaa suruali nchini Malawi. Baadhi ya wanawake wamevuliwa nguo na hao wamachinga. Pichani mmoja ya wanawake ambaye alivuliwa suruali kwenye hiyo kampeni ya wamachinga inayoitwa "anti-trouser and mini-skirt campaign to ladies"
Lakini wengine wanadai wamachinga hao wanawavua nguo wanawake kwa sababu kuvaa suruali, mini-skirts na leggings kunadhalilisha wanaume. Pia wapo wanaodai wanafanya hivyo kupinga utawala mbaya wa Rais Bingu wa Mutharika. Wanadai kwa vile utawala wa Mutharika umepiga marufuku maandamano ya amani hawana jinsi ya ku-express jinsi utawala wake ulivyo mbovu zaidi ya kuwavua wanawake nguo.
Hadi mwaka 1996 ilikuwa marufuku kwa mwanamke kuvaa suruali nchini Malawi. Baadhi ya wanawake wamevuliwa nguo na hao wamachinga. Pichani mmoja ya wanawake ambaye alivuliwa suruali kwenye hiyo kampeni ya wamachinga inayoitwa "anti-trouser and mini-skirt campaign to ladies"