Wanaume wenye Mahawara Please Muwe Makini sana

Wanaume wenye Mahawara Please Muwe Makini sana

Kuna watu wamekasirika vibaya sana utadhani hawajarogwa kumbe ndo washarogwa siku nyingiiiiiiiiii!
Jisalimisheni tu kwa Bwana Yesu.
 
dhambi gani? wewe mtu anakulilia ufanyeje?

Dhambi kwako utaipata kama ifuatavyo:
- Umesema jamaa anayechepuka ana mke na watoto 3, sasa yawezekana huo mchepuko umekuwa unaigharimu sana familia ya jamaa kiasi kwamba akakata shauri aupige chini na wakati anaelekea kufanikiwa wewe umemtibulia.
- Kama familia ya jamaa italala njaa, kukosa huduma muhimu na mengineyo wewe utabeba sehemu ya msalaba.
- Kama jamaa atazidiwa na mchepuko na kuamua kuitelekeza kabisa familia yake ujue na wewe umo pia.
- Kwa lugha nyinine ni sawa huyo binti siku nyingine aje kwako akuambie jirani naomba 50,000 au laki nikatoe mimba ili niweze kumaliza chuo, na wewe ukampa, hiyo dhabi nawe utaibeba. Sawa mkuu??
 
Jamen si kaja kutoa tahadhari kwa wanaume na kutupa mbinu wanawake ubaya uko wapi hapo?

Hawa ni wale wanaume wakimegewa pande na mke wa jirani hawachelewi kujikomba oooh mke wa Fulani(jina linahifadhiwa) ni mtamu sana!
 
Mkuu tujichange tupate 30000 nyengine tupeleke kwa mtaalamu amrogowe mwanaume mwenzetu haa haa haaa haaa

hahahahah! please jamani! msijaribu, najua nilikosea but naombeni radhi kwa wanaume wenzangu, hii ibaki kuwa lesson kwetu, yawezekana hawara yako akapewa pesa na mwanaume mwingine!!
 
Mkuu sasa unalaumu nini? hawara yako anaweza kuomba pesa kwa mwingine akufanyie wewe...ndo maana natoa tahadhari.
 
Kwa maana moja au nyingine wewe umefanikisha kumroga huyu jamaa. KATUBU DHAMBI HIYO
 
Kama na Mimi naijua hiyooo dawa nampa ciwajifanya kicheche warogwe mpaka
 
Jumamosi ya juzi nikiwa ndani mwangu nafuatilia Bunge, nilisikia hodi ikabidi nikajue ni nani, alikuwa ni Jirani yangu (Binti) ana miaka kama 24-26 hivi, toka nimehamia hapa sijui ana shughuli gani inayomwingizia kipato au inayomfanya aishi hapa mjini, Baada ya kumkaribisha ndani akaanza hivi.

(Jina Langu) samahani, nikamjibu...bila samahani...(Jina lake), nina shida ya sh.30,000/= naomba unisaidie,(kwa kuwa nimezoena nae sana akaanza kunisimulia)

Kuna hawara yake ni doctor hapa Bug...juzi yake alimwambia kuwa "hamtaki tena kuanzia Juzi hiyo" huyo hawara yake ana mke na watoto 3.

Ni yeye (hawara) ndiye anayemlipia kodi ya nyumba, anamsomesha chuo cha Hotel management na ndiye anayemtunza kwa maana ya chakula.

Sasa kodi inaisha mwezi wa kwanza mwakani na ada ya chuo anadaiwa na imebaki sh. 700,000/= na pesa ya kwendea field Zanzibar hana.

Akaniambia kuwa, ...Nimepata mtaalamu (mganga) ameniambia nimpe sh. 30,000/= ili anipe dawa nimvute, (Amchomee) ili kurudisha mawasiliano halafu nyingine atamwekea kwenye chakula au kinywaji ili "akiomba kiasi chochote kile cha pesa apewe"

Sikuwa na iyana ila nimuuliza swali moja, kwa nini usitumie njia ya mazungumzo? akasema nishajaribu sana but hataki! "sasa mimi nitaishije hapa wakati ada nadaiwa, kodi ya nyumba inaisha mwakani"?

Nilimpa sh. 30,000/= akaenda.

Jumapili (jana) huyo hawara yake alisalimu amri yy mwenyewe kwa yeye kuanza kumpigia simu (kwa mujibu wa huyu binti) jamaa alimuuliza "upo wapi"? demu akajibu nipo nyumbani, Njoo .....bar...sasa kilichojiri huko jana sikijui nadhani leo ataniambia tu..

Kwa hiyo, wanaume tuwe makini sana na mahawara kwani yawezekana unaye na unatamani ujinasue kwake ila moyo wako unakufa ghafla na kuamua kuendelea naye hadi sasa. Pls, tuwe makini sana.

anayeshiriki kumloga mwanamme mwenzake na yy mchawi tu.
 
Back
Top Bottom