Habari wanajamii
Naombeni mchango wa mawazo, imetokea wanaume wananiambia ati wananiogopa, mie ni mbabe, najiamini sana na wengine huenda mbali kwa kusema mwanamke wa dizain yako sioi.
Kwakweli sipo hivyo na huwa naumia sana mtu anaponitamkia hayo. Nasikitika mana sielewi ni kitu gani na kutongozwa na waume za watu kumezidi il a sio na singles?
Tafadhalini wanajamii naimani kuna watu wanaofahamu vizuri psychology wanishauri jamani.
Asanteni kwa kunijibu bila kejeli
Pole sana.
Nina rafiki yangu mmoja hivi mchaga msichana mwenye kazi yake shule nzuri tu na nahisi mnaendana kabisa na wewe.
Wanaume wanakaa nae mbali kabisa. Anyways dada ni mbabe kweli. Hatua zake tu za kutembea, pumzi yake, sauti na akifika sehemu lazma atambulike amefika.
Huyo rafiki ana shepu haswa. Mtoto wa kichaga ila ana mguu wa bia. Tatizo tu MBABE.
Tumemshauri kuhusu ubabe na kidogo amejifunza. Ameacha, amekuwa mpole na ananyenyekea. Kapata mchumba sasa na naona wameshibana haswa, nawaombea wafike mbali.
Jikaze, punguza au ficha tabia za ubabe. Pigana kuacha hiyo tabia utashinda.
kila kitu majanga....Hahahahahahahahah,
Umeona sasa matokeo yake??
Thank u B! Always love u
kila kitu majanga....
ukiwa mpole sana janga ukiwa mkali janga, sasa sijui tuweje!
Jitahidi tu utashinda kwa kuwa mwenyewe umeshalitambua hilo.Nitajitahidi mana MTU akitamka tu hilo neno ananihuzunisha sana
Ndio maaana sio kila mwanamke anafaa kuwa mke
Habari wanajamii
Naombeni mchango wa mawazo, imetokea wanaume wananiambia ati wananiogopa, mie ni mbabe, najiamini sana na wengine huenda mbali kwa kusema mwanamke wa dizain yako sioi.
Kwakweli sipo hivyo na huwa naumia sana mtu anaponitamkia hayo. Nasikitika mana sielewi ni kitu gani na kutongozwa na waume za watu kumezidi il a sio na singles?
Tafadhalini wanajamii naimani kuna watu wanaofahamu vizuri psychology wanishauri jamani.
Asanteni kwa kunijibu bila kejeli
sana maana wanakimbia then wanaanza kurudi lambda ni kweli unachowaza lol
Usikatae katakata kwamba hauko hivyo.
Jiangalie, jifanyie tathmini ya dhati.
Huenda huwa una-radiate vibe flani flani zinazofanya watu wahitimishe (kimakosa) hivyo wanavyohitimisha.
Katika maisha ni muhimu pia kujikosoa na kufanyia kazi mapungufu yako.
ha haaaa, huyo mwanaume hapo atakuwa kilaza, anaogopa challenges