Mulhat Mpunga
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 27,650
- 16,722
so ishu aendelee na mambo mengine kuliko kuishi kwa kusimangana na kulala mzungu wa nnee bora kila mtu ale kona kwani nini!!!?
Kama inabidi aulize ushauri Instagram kuhusu azungumzie maisha yake binafsi au asizungumzie basi hata siwezi kushangaa kashindwa kukaa na Jide.
Na anavyojianika anaishi kwa hisani ya yule na huyu, anahakikisha kuna wanaume kama mabinti kama alivyoimba Jide.
Hawa wote wamekutana, yule Jide ana kiburi na anajua kukitumia, huyu Gardner anajua kujifanya victim.
Reversal of roles, kibongo kawaida mwanamme ndiye anakuwa na kiburi na nwanamke anajifanya victim.
No wonder Jide aliimba wanaume kama mabinti na Yahaya.
The Boss
Hahahaaaa,kuna jamaa juzi juzi hapa aliniambia eti nina LL.B Marekani hawatoi LL.B.
But then again I went to the School Hard of Knocks where I majored in Major and got a PhD. in Common Sense:smile-big:.
Mbona unakiburi ivyo wewe mwanamke...alafu ndio unaniambia nichepuke na wewe... nimekushtukia kumbe unataka
unigardne.
Hehehe, #VJM ndo nani tena?
Nacheka kama mazuri,nampenda sana jide na kwa ajili ya mziki wake. Gadner nilipenda support aliyokuwa anampa mkewe. Seen a few gestures between them nikaona wanapendana. Ila kwa hili jide anachemka. Ingetosha kusema ilikuwa ndoanyenye physical and emotional abuse akaishia hapo. Too much info sijui za kushika makalio wahudumu blah blah
Wanawake mnao m-support Jide jiangalieni mara mbili mbili kama mnafaa kuwa wife materials???
My jiangalie, kuna watu mapovu yanawatoka humu, mie sitii neno. ha ha haaa haaa.
kuna haja gani ya kuandika instagram, fb, twitter etc kwa mtu mzima kama gadna.
kuna umri ukifika mambo ya mitandao unayaweka pembeni. unafanya maisha kimya kimya.
Do l care?
Ukweli lazima usemwe...
Usijali, niko huku Tanga kwenye mapango, wakisumbua tu nalipua....
pure heart
Akili yangu inakataa kuwa GGH alikuwa mario kwa JD. Wakati wanaoana JD hakuwa na hela - alikuwa maarufu tu. Mafanikio ya JD yamechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na GGH kwa sababu GGH kazi ya umeneja aliiweza vizuri, biashara ya starehe anaijua vizuri na kwa kutumia ujuzi wake huo aliweza kumtengenezea JD njia. Kwa hiyo waliunganisha vipaji.
Kama kuna mtu mwingine ukiacha GGH aliyekuwa anasimamia kazi za JD naomba kufahamishwa. Sasa kama GGH alikuwa anaendesha "magari ya JD" alikuwa anaendesha magari ambayo ameyatolea jasho kwa kuandaa show za mkewe, kusimamia miradi n.k. Ni magari yao. Kama JD ataamua kujimilikisha mali zote kwa sababu GGH hakuchangia itakuwa ni dhuluma ya wazi wazi.
Na hapa ndipo ninapowaonea huruma wanaume wanaochuma mali na wake zao ambao usoni ndo walionekana wakifanya kazi kisha ndoa zikabumburuka. Akidai haki yake ataitwa a.k.a mario. Hata kama JD alikuwa akimlipa GGH kwa umeneja wake na GGH akawa na mali zake, naamini zipo mali zao kama wanandoa. Wao wanajua vizuri zaidi. GGH anaweza kuwa mario kwa wanawake wengine ila si kwa JD. Kaka alikuwa anajituma.
Kuhusu tabia zilizosababisha JD kumuacha mumewe mi naona ni sawa alivyofanya. Swali ni je, ndo kajua leo tabia za mumewe? Hapana. Alijua kabla hata hawajafunga ndoa ila kwa kuongozwa na wimbi zito la mahaba lililomfanya aone chongo la GGH kuwa kengeza. GGH ni kunguru asiyefugika. Ana tatizo la kihaiba. Naogopa kumhukumu kwa tabia zake mbaya maana siamini kama anazifurahia.
Atafurahia nini ndoa ya kwanza imemshinda-hayuko na mkewe wala m/wanae, mahawara ndo leo kwa huyu, kesho kwa huyu, ndoa ya pili imemshinda anajidhalilisha kwa kuvulia wanawake nguo hovyo ingawa hii inaonekana si tatizo kwa wanaume pombe nyingi Ndani kabisaa GGH hana furaha. Ni binadamu gani awe wa kike au wa kiume hapendi utulivu, upendo na amani? Nampongeza JD kuwa ameweza kutoka kwenye kifungo cha utumwa wa kihisia alichokaa muda mrefu. Namuombea GGH naye afike mahali aweze kutoka kwenye kifungo alicho nacho.
Kitendo cha kuropoka hadharani si cha kiungwana ila wenzi wengi wa kike kwa kiume huwa wanafanya hivi katika kutafuta faraja na huruma sema ndo hivyo mambo mabaya huwa ni ya kike, mazuri ya kiume.
Kwetu uchagani unatengwa na ukoo.
there you are mkuu...mimi tangu zamani nawaambia wana kuwa JD hajui kunakomfaa...taarabu taarabu taarabu..na kwa mtu yeyote mwenye ufahamu wa wastani anajua JD needed that marriage kuliko GadnaAmkaushie tu yule mwanamke ni bingwa wa malumbano na akiona anaelekea kushindwa anakimbilia huruma ya wana jamii.
Kukaa kimya ni jibu tosha.
kuachwa kunauma.... ata akimjibu ndo kishaenda hivyo, ataendelea kuendesha vits yake mambo ya vogue atabaki kusimulia
#IshakuwaHistoria