Ruttashobolwa
Kwa mtazamo wangu hiyo ni kweli kabisa na wengi wenye mtazamo tofauti nadhani ni ama wako kwenye denial au wanasumbuliwa na ujinga (ujinga si tusi btw, ni ile hali ya kutojua au kutokufahamu jambo au kitu fulani tu).
Na tusiende mbali. Tuanze na humu humu Jamii Forums.
Ni wanandoa wangapi humu ambao wenza wao wanajua kuwa wamo humu?
Na kama wapo wanaojua, ni wangapi hata wenye access na PMs za wenza wao?
Kama wana access, wana access ya accounts ngapi ukizingatia mambo ya multiple IDs?
Ni wanandoa wangapi humu huwa wanapinga wenza wao kushika simu zao (a dead giveaway in my opinion)?
Kwa nini hawataki waume au wake zao washike simu zao? Kuna nini humo kwenye simu?
Eti wanaonyeshana nyeti zao lakini ikija kwenye simu hapana, kila mtu ashike yake,Vichekesho tupu.
Ni wanandoa wangapi waliomo humu Jamii Forums ambao huwa wana flirt flirt na members wengine, iwe kwenye threads au kwenye PM?
Ndoa nyingi zimejaa unafiki na wanafiki tu.