Wanaume tukutane hapa tumshauri Captain Gardner

Wanaume tukutane hapa tumshauri Captain Gardner

Ndoa na watu wenye majina tz ni ndoa ngumu mifano haoi ni mingi.Huu ni ushauri wangu kwa hasa wanawake.

Mwanaume kuishi na mwanamke kwa kumtegemea yeye ni kinyume na maandiko na ni kinyume na akili za kibinadamu.Uzuri wa sura au umaarufu sio kigezo cha wewe kutunzwa na mwanamke.Huu ni ushauri wangu kwa wanaume hasa watoto wa mama
 
jibu la kumpa ni asante then pole..........the endelea na maisha captaiiiiiin....
 
@ Nyani Ngabu

Uzoefu wako ni kwa kuangalia ukiwa nje au ndani?
 
Mke wa Gadner alishaolewa kitambo sana, tena ilibidi abadili dini mdada wa watu, yuko anaendelea na maisha yake Mwanza

Mimi ni mwanaume lakini siwezi kuwa upande wa Gadner hata siku moja.Nakumbuka alivyomuacha mkewe akiwa na watoto wadogo.Masononeko ya mkewe ndiyo yaliyomfikisha hapo.Arudi kwa mkewe aombe msamaha ili mkewe akunjuwe nafsi la sivyo kila siku atakuwa mtu wa majuto na kuomba ushauri mitandaoni.
 
Mkuu na hicho kitafanyika kama hata captain alikuwa anaenda tu kusimamia mafundi hata hatoi mia huo ni mchango tosha na ana haki yake hapo!captainiiiiiiiiiiii

Kwanin asimamie tu bila hata kutoa mia? Atakuwa alichangia kidogo bhana inatakiwa wagawane,ila wanaume wajifunze kupambana bila kutegemea wake zao
 
Huyo gadna aachane na maneno yaelekea jd ameumia ndio maana kaamua kuongea ujinga akidhani atamdhalilisha g kumbe anajidhalilisha mwenyewe. Janamke jinga Sana Hilo.
 
Toka hawa watengane kumekuwa minong'ono na uvumi mwingi kuhusu sababu zilizopelekea ndoa yao kusambaratika.. Kwangu mie nadhani kwa kuwa hawa ni ma-celebrity wetu ingekuwa vema wakaweka wazi sababu za wao kutengana ili jamii sasa iache kuamini minong'ono na rumours.. Na kwa vile Jide ameshaweka wazi sababu basi na Le Captain nae aandike tu sababu zake wafunge mjadala..

Hii mihemko yetu hapa imejengwa na hisia na mapenzi binafsi kwa Le Captain na Jide maana wachangiaji wengi hapa wamegawanyika.. pro Jide wanamkandia Le Captain na pro Le Captain wanamponda Jide..
 
pure heart
Akili yangu inakataa kuwa GGH alikuwa mario kwa JD. Wakati wanaoana JD hakuwa na hela - alikuwa maarufu tu. Mafanikio ya JD yamechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na GGH kwa sababu GGH kazi ya umeneja aliiweza vizuri, biashara ya starehe anaijua vizuri na kwa kutumia ujuzi wake huo aliweza kumtengenezea JD njia. Kwa hiyo waliunganisha vipaji.

Kama kuna mtu mwingine ukiacha GGH aliyekuwa anasimamia kazi za JD naomba kufahamishwa. Sasa kama GGH alikuwa anaendesha "magari ya JD" alikuwa anaendesha magari ambayo ameyatolea jasho kwa kuandaa show za mkewe, kusimamia miradi n.k. Ni magari yao. Kama JD ataamua kujimilikisha mali zote kwa sababu GGH hakuchangia itakuwa ni dhuluma ya wazi wazi.

Na hapa ndipo ninapowaonea huruma wanaume wanaochuma mali na wake zao ambao usoni ndo walionekana wakifanya kazi kisha ndoa zikabumburuka. Akidai haki yake ataitwa a.k.a mario. Hata kama JD alikuwa akimlipa GGH kwa umeneja wake na GGH akawa na mali zake, naamini zipo mali zao kama wanandoa. Wao wanajua vizuri zaidi. GGH anaweza kuwa mario kwa wanawake wengine ila si kwa JD. Kaka alikuwa anajituma.

Kuhusu tabia zilizosababisha JD kumuacha mumewe mi naona ni sawa alivyofanya. Swali ni je, ndo kajua leo tabia za mumewe? Hapana. Alijua kabla hata hawajafunga ndoa ila kwa kuongozwa na wimbi zito la mahaba lililomfanya aone chongo la GGH kuwa kengeza. GGH ni kunguru asiyefugika. Ana tatizo la kihaiba. Naogopa kumhukumu kwa tabia zake mbaya maana siamini kama anazifurahia.

Atafurahia nini ndoa ya kwanza imemshinda-hayuko na mkewe wala m/wanae, mahawara ndo leo kwa huyu, kesho kwa huyu, ndoa ya pili imemshinda anajidhalilisha kwa kuvulia wanawake nguo hovyo ingawa hii inaonekana si tatizo kwa wanaume pombe nyingi Ndani kabisaa GGH hana furaha. Ni binadamu gani awe wa kike au wa kiume hapendi utulivu, upendo na amani? Nampongeza JD kuwa ameweza kutoka kwenye kifungo cha utumwa wa kihisia alichokaa muda mrefu. Namuombea GGH naye afike mahali aweze kutoka kwenye kifungo alicho nacho.

Kitendo cha kuropoka hadharani si cha kiungwana ila wenzi wengi wa kike kwa kiume huwa wanafanya hivi katika kutafuta faraja na huruma sema ndo hivyo mambo mabaya huwa ni ya kike, mazuri ya kiume.
 
Last edited by a moderator:
Mwanamke mwenyewe mpapai dume, mnataka Gadner azeeke akiwa na mtoto wa nje ya ndoa tu? Oa mwingine upate uzao Gadner, maana ingekuwa wewe ndiyo mwenye matatizo wangejazana humu kukashifu wanaume....
 
grafani
Hujafa hujaumbika Mtoaji wa kila kitu ni mungu unaweza ukazaaa watt Saba lakni likatokea la kutokea ukajikuta Huna hata mmoja na Huna uwezo wa kupata wengine Kila kitu ni mapenzi ya Mungu.
 
Last edited by a moderator:
jisanja
Hilo tunalijua hata Kipunguni A limetokea wiki mbili zilizopita. Hoja iliyopo ingetokea kwa mwanaume kukosa uzazi je upande wa pili ungevumilia?
 
Last edited by a moderator:
Mke wa Gadner alishaolewa kitambo sana, tena ilibidi abadili dini mdada wa watu, yuko anaendelea na maisha yake Mwanza

Yule ndo alikuwa mke huku mshkaji alifata kutunzwa na jde
 
Hii inafurahisha sana, yaani leo hii Jaydee anaumuita Gadner malaya kwa kumkuta na wanawake wengine, ingekuwa Gadner si umalaya yeye Jaydee pale Mwanza angempata vipi mwanaume huyo wakati alikuwa na familia yake yenye (mke na mtoto).
Alichokifanya Jaydee ni kumchukua Malaya mwenzie kutoka kwa mwanamke mwengine aliyetulia nyumbani kwake, na alipopata alichokipata Jaydee akaamua kutulia. Lakini alisahau tabia haina dawa.....
 
Mimi nitamtafuta JIDE numshawishi tufunge ndoa,,, niko tayari kulima hata kurina asali ili walau niwe nikirudi na shina la karanga au kikombe cha asali nikilambisha na kumuambia hiki ndicho nimeweza kupata mke wangu!!!
 
Binafsi sioni kama ni busara kwa huyo bwana kuingia katika vita vya maneno kupitia mitandao ya kijamii na huyo mwanamke.

Huyo mwanamke rekodi yake ya inda, unyambi, na ushari inajulikana.

Na ni kweli si malaika hata kidogo na watu tulio na utanabahi wa haki na usawa hatuamini mazima yale yote yaliyozungumzwa naye juu ya huyo bwana.

Kwa sasa ampotezee tu.

Duh! Sikuiona hii comment ilipotoka. Yaani mkuu NN pamoja na kuwa na "ngeli" inayotisha unatesa pia kwenye Kiswahili? Ndio maana nazidi kuamini kuwa wanaosingizia Kiingereza kama sababu ya kuanguka kwa elimu ni wababaishaji wanaotaka kuwanyima Watanzania fursa ya kutanua ulimwenguni.
 
Back
Top Bottom