MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,607
Kwa ushauri tu, kabla ya kuingia ndani kabisa ya mahusiano, ni vyema kujua dhamiri ya mwanamume na dhamiri yako. Ikiwa dhamiri yako ni kupata mwenza wa kudumu, haifai kujiingiza kichwa kichwa, msome na yeye ana dhamiri gani na sio kwa maneno tu. Kwa kutumia msemo wa "Hakuna anayeiona asali kuwa ni chungu", wanaume wengi huwa tuna tabia ya kuonja-onja halafu tunapotea. Vile vile, kuna baadhi ya wanaume kadiri unavyomfatafata kwa simu, barua n.k. ndivyo anavyojiona ni muhimu sana na ndo mana honesha nyodo. Uamuzi wa mwisho, usisubiri mpaka mwanamue anakuchunia, anza kumchunia wewe.