Wanaume mna nini na simu zenu?

Wanaume mna nini na simu zenu?

Nakumbuka wakati nimempeleka mchumba wangu home Bi mkubwa alituambia ni marufuku kushika simu ya mwenzako bila ridhaa yake ili muishi kwa amani, mpk leo hii kila mtu anaheshimu simu ya mwenzake
 
habari za leo wanajamvi.....jamani leo nimestaajabu.Leo nikiwa nimetolewa dinner na shemeji yenu mtarajiwa huku tukibadilishana mawazo ya hapa na pale nikapata simu ya msiba sasa kwa kua sina salio la kutosha nikasema nichukue simu ya shem wenu ili nipate kujua zaidi juu ya msiba lakini mwenzenu Ile nimeshika simu tuu nikashangaa ghafla nimevutwa mkono yani mkono umenyongorotwa kidogo nitoe damu...Ile nataka kukimbia nayo nikavutwa mpaka mkono kidogo nivunjike. Hivi jamani wanaume mna nini ni vitu gani au siri zipi ambazo hampendi zijulikane naombeni kujuzwa
Kuwa naye kwenye mahusiano hakuondoi neno NAOMBA toka kwako kwenda kwake..... HUKUOMBA NDO MAANA...
 
habari za leo wanajamvi.....jamani leo nimestaajabu.Leo nikiwa nimetolewa dinner na shemeji yenu mtarajiwa huku tukibadilishana mawazo ya hapa na pale nikapata simu ya msiba sasa kwa kua sina salio la kutosha nikasema nichukue simu ya shem wenu ili nipate kujua zaidi juu ya msiba lakini mwenzenu Ile nimeshika simu tuu nikashangaa ghafla nimevutwa mkono yani mkono umenyongorotwa kidogo nitoe damu...Ile nataka kukimbia nayo nikavutwa mpaka mkono kidogo nivunjike. Hivi jamani wanaume mna nini ni vitu gani au siri zipi ambazo hampendi zijulikane naombeni kujuzwa
Ni ruksa kushikana na si kushikiana simu,,,......
 
Badala ya kuomba vocha/salio, wewe unakimbilia simu. Ulikuwa na lako jambo.
 
Yeye mwenyewe utakuta wala hajihangaishi na yako, kwanini usiombe akuongezee salio, na shida yako sidhani kama ilikua kupiga simu, ilikua ni kukagua simu,
 
Hakuna uhuru usio na mipaka.na hakuna mapenzi yasiyo na mipaka.Ata kama mnapendana kufa kuzikana bado kuna mambo yanabaki kua private kwasababu mapenzi sio sababu yakumuamin mtu asilimia 100.Na simu zinatunza mambo mengi mengine ni mambo binafsi.Inawezekana mwanaume hakawa hana michepuko ila kwa mwanaume anayejitambua hawez kumruhusu mwanamke wake ajue kila kitu chake maana kumwamin sana mwanamke nako ni shida.Kwaiyo usishangae sana ndo ivyo ilivyo.
 
Kwa sababu wanawake wenzenu wanatutongoza sana huko kwa ofisi facebook shoga yako yule jiran pale saloon naye ananitumia msg za kimahaba
 
Si ungeomba ukuongezee salio kwenye simu yako ?
Sasa kwenye simu yake ulikua unataka nini ?

Ningekua mimi ningekuvunja mkono kabisa ili siku nyingine usirudie maana hamkawii kupeperusha ndege wetu....
 
ni kweli mkuu...tena roho inaacha mwili mchana kweupe[/QUOTE. Achana nao kabisa... Ukifanikiwa sasa kuikagua. Utajutraa utayokutana nayo. Kama hujapata ugonjwa wa kupooza ni kifo cha moja kwa moja
 
kwan kipind naenda kusajili line tulisajili wote? nikiambiwa naingia jela kisa simu tutaenda wote? we tulia baki na simu yako na mim nibak na yangu
Ndio uzuri wenu yaani hukosi sababu umefika mbaaali kote lengo likiwa moja tu simu isiguswe.
 
Binamu wewe sio wa mchezo mchezo.

Huko radhi kumimina risasi kisa simu daah inaelekea simu yako ni kama bomu.
ha ha ha ha binamu ndio maana kila mtu ana simu yake angetaka tungetumia simu moja tu wote wawil
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom