Ubuntu trusty tahr
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 326
- 228
hata kama we ni kipenzi changu ndo ushike simu yangu??..habari za leo wanajamvi.....jamani leo nimestaajabu.Leo nikiwa nimetolewa dinner na shemeji yenu mtarajiwa huku tukibadilishana mawazo ya hapa na pale nikapata simu ya msiba sasa kwa kua sina salio la kutosha nikasema nichukue simu ya shem wenu ili nipate kujua zaidi juu ya msiba lakini mwenzenu Ile nimeshika simu tuu nikashangaa ghafla nimevutwa mkono yani mkono umenyongorotwa kidogo nitoe damu...Ile nataka kukimbia nayo nikavutwa mpaka mkono kidogo nivunjike. Hivi jamani wanaume mna nini ni vitu gani au siri zipi ambazo hampendi zijulikane naombeni kujuzwa