Wanaume mamwinyi

Wanaume mamwinyi

Wanaohudumia wapo wachache. Wengine wanahudumiana
Usilazimishe kuhudumiana.
Inategemeana na mtu, kama unaona ni lazima mme wako akuhudumie na hataki basi achana nae utafuta atakayekuhudumia.

Mimi namsaidia mke wangu kazi ninapokua na muda, ila akiweka akilini kwamba ni lazima nimsaidie ajue ndo naacha simsaidii tena na sipangiwi.
Akitaka usawa nayeye apeleke posa kwetu.
 
Usilazimishe kuhudumiana.
Inategemeana na mtu, kama unaona ni lazima mme wako akuhudumie na hataki basi achana nae utafuta atakayekuhudumia.
Binafsi silazimi kuhudumiwa. Ni jukumu lake na kama akishindwa atasaidiwa tu hakuna namna.
Nilikuwa namjibu huyo ambae amesema hizo ni kazi za mke wakati kazi yake ya kuhudumia familia financially mkewe anaifanya pia.
 
Tabu yote ya nini si utafute mjakazi akufanyie yote hayo?
Unadhani ingekuwa unaweza kupata mtoto bila ndoa na haya madini yetu yazingekuwepo,mi nisingeoa nipo unique sana yan mi nkishafanya ngono nikamaliza uwaga sioni ht umuhimu wa mwanamke zaid ya kupikiwa,kufuliwa,kuonyewa vyombo...mpaka nakua mkubwa style yangu ya mapenzi ni kuitana weekend kubanduana then kila mtu anapita njia yake...naamini mi ni mtu wa ajabu sana sababu nikiwa mwenyewe ndo nakuwa na furaha sn

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi ya mwanamke ni kumhudumia mwanaume wape nafasi wenzio walihudumie njemba,trust me watalichukua jumla
Mkuu umeegemea upande.
Kazi pia ya mwanaume ni kumhudumia mkewe. Vise veser, tunahudumiana na kutegemeana katika maisha.
Mwanamke kwa kazi za nyumbani, mwanamme kwa kazi za nje,50/50.
Sasa maisha ukiyaangalia kwa jicho la makengeza hupelekea kuuona upande mmoja tu wa shilingi.
Nini kupeleka maji bafuni, nini kukarangiza jikoni na kuandaa meza?
Ushawahi kufika machimboni ukaona jinsi mwanamne anavyoisaka pesa kwa jasho jingi kuliko hiyo ya kuchemsha maji ya kuoga?
 
Unadhani ingekuwa unaweza kupata mtoto bila ndoa na haya madini yetu yazingekuwepo,mi nisingeoa nipo unique sana yan mi nkishafanya ngono nikamaliza uwaga sioni ht umuhimu wa mwanamke zaid ya kupikiwa,kufuliwa,kuonyewa vyombo...mpaka nakua mkubwa style yangu ya mapenzi ni kuitana weekend kubanduana then kila mtu anapita njia yake...naamini mi ni mtu wa ajabu sana sababu nikiwa mwenyewe ndo nakuwa na furaha sn

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoto bila ndoa inashindikana vipi mkuu? Sidhani km ni sahihi kuingia kwenye taasisi ambayo unatambua kabisa huiwezi. Not fair kwa mwenzako na kwako pia maana utapata stress sizizo na sababu maisha yako yote
 
Kuna wanaume wanapenda u-mwinyi bwana, yaani anaamka anaenda kuoga wakati anaoga unatandika kitanda na kuweka mazingira ya chumba vizuri. Unakwenda jikoni kuandaa chai, anatoka bafuni na taulo kiunoni anatafuta atavaa boxer na kama atakumbuka mafuta basi itakuwa kwenye viganja vya mikono. Taulo atakuachia juu ya kitanda si tatizo lake tena.

Mezani umeandaa chai na vitafunio hata kama chumvi haisikiki mfano kwenye mayai atakuita ukamchukulie jikoni hapo ni baada ya kukuita umletee maji ya kunawa na tissue ya kujikaushia.

Yaani ameshindwa kabisa kwenda kunawa jikoni au bafuni au kwenda jikoni kuchukua chumvi. Na akimaliza kula hataondoa hata kijiko mezani anaacha kila kitu pale anakwenda kukaa kwenye sofa anaangalia mpira, kusoma gazeti au anachat kwenye simu. Hiyo ni weekend.
Na kuna wanawake wasipompata bwana wa kumhudumia hivyo hawafurahi, wanaona wamenyimwa sehemu yao ya kumhudumia bwana.

Cha msingi wewe tafuta/kuwa na wako unayemtaka na hao mamwinyi waachie wenyewe wanaowataka.
 
Kwani lazima uolewe?
Maana kila siku mada zako ni kulalama tu.

Ukiona uko sawa na mmeo basi nawewe oa mke akuhudumie.


Labda kama wewe sio mwanamke, kama wewe ni mwanamke na umeolewa basi ndoa huiwezi maana unalalama sana.

Mada yako nyingine hii hapa ukilalama

Ewe mwanaume, zama zimebadilika, upikiwe? Kwanini wewe hupiki?
Haka kamwanamke sijui kamevurugwa na nini. Kama ndo kamke kangu nyumbani narudi kulala tu, nakuwa nishakula, kuoga na kila kitu huko nilikotoka tuone kama ujinga utaendelea
 
Binafsi silazimi kuhudumiwa. Ni jukumu lake na kama akishindwa atasaidiwa tu hakuna namna.
Nilikuwa namjibu huyo ambae amesema hizo ni kazi za mke wakati kazi yake ya kuhudumia familia financially mkewe anaifanya pia.
Yaani ni jukumu la mume wako kukuhudumia kwa maana ya kazi za ndani?

Huyo mwanaume mnayewekeana hayo shukuru kua nae, ukinipangia majukumu ya jikoni ujue ndoa utaiacha, hayo mambo naweza kuyafanya ninapotaka mimi mwenyewe sio mke anipangie.

Kama una misimamo huo jua mume wako ni kati ya wanaume maboya kule kwetu kanda maalumu.

Hata hivyo nakusifu kwa kuoana na mume wako.
Mimi nimemuoa mke wangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom