Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Polisi wetu wa ajabu kweli yaani wamejaa jazba muda wote , .... ebo? sisi raia ndiyo tunatoa ushirikiano mpaka mnafanikiwa lakini sasa mmejaa vitisho matamko kibao. badilikeni jifunzeni kwa mzee tibaigana.
 
Tatizo ni mfumo mbovu wa Elimu sio yeye,huwa nafikiri nakosa majibu inakuaje watu kama Chriss Hani,Joe Slove au Oliver Tambo Elimu zao zilikua za kawaida lakini walikua vichwa sana kuriko hawa wameudhuria shule lakini kila kukicha matamko kama hata shule hawakupita..
 
Washauriwe waache kutoa matamko yenye ladha ya kisiasa wala kuonekana kuwa na mwelekeo huo bali wawatafute na kupambana na wahalifu. Wasijenge mazingira ya kuwatishia wananchi vinginevyo watakosa ushirikiano wao katika kutekeleza wajibu wao!
 
Mwigulu Nchemba unadhani mkifanya hivyo ndiyo raiya watalipenda jeshi la polisi?
Pia mtafanya hivyo kwa sheria ya Tanzania au sheria ya Korea Kaskazini??
 
Washauriwe waache kutoa matamko yenye ladha ya kisiasa wala kuonekana kuwa na mwelekeo huo bali wawatafute na kupambana na wahalifu. Wasijenge mazingira ya kuwatishia wananchi vinginevyo watakosa ushirikiano wao katika kutekeleza wajibu wao!
Ushirikiano baina ya jeshi la police na raia ni lazima udumishwe. Hii itasaidia amani ya nchi kuzidi kwenda mbele.
 
Ananikumbusha korea ya kaskazini alipokufa kim jong il,pale kwenye msiba lazima ulie kwa juhudi na kuonekana una hudhuni sana,ole wako shushushu wakukute haulii,
wanakuweka kizuizini wewe na family yako yote na haurudi uraiani ng'o..

Umeniwahi aisee!

Nilitaka kusema kidogo kidogo tunaanza kuwa kama Korea Kaskazini!
 
Ukimya una ufanisi katika mapambano kuliko maneno au kelele.
Hata hivyo, kelele mara nyingi huashiria hali kutodhibitiwa, iwe kwa wanyama au binadamu.
 
Ninavyofahamu kulia au kucheka ni vitu ambavyo huwezi kuvizuia. Ni hisia ambazo hutokea bila kutarajia. Wakati mwingine ni vigumu kupima kiwango cha hisia kutoka MTU mmoja had I mwingine.

Ndo maana watu wawili Wa tumbo moja wanapokea kwa utofauti taarifa za kifo cha ndugu yao ya karibu. Mwingine unaweza muona anacheka kumbe ni kinyume chake!

Hivyo basi haiingii akilini watu wrote wakawa na mtizamo mmoja kama Wa mgombe kupata asilimia 100 ya kura. Ukiona una jumuiya ya a in a hiyo hilo sio eneo salama.

Haiwezi kufika wakati Jumuiya ikawa kama yenye kuishi kwenye gereza kubwa kwa kukabidhi haki zenu kwa wengine.

Vinginevyo kitendo cha kutaka watu wote walie hakina tofauti na kutaka wote wacheke kwa wakati maalum! Utaenda mbele utawataka hao watu wazungumze, wavae, wasali, waimbe nk kama wewe. Hakuna jamii kama hiyo ndio maana Korea kaskazini RAIA wake wanajitahidi kutoroka kadri wanavyoweza.
 
Ukiwakamata uwapeleke mahakamani. Si polisi kama mnavyofanya. Wapeleke mahakamani ili mkajieleze wote.wewe mlalamikaji na yeye mshitakiwa. Hata hivyo ni ajabu kudhani kuwa kwenye msiba watu wote watalia! Wapo watakaofurahia kufa kwako, watakaosikikitika, na ambao wapo wapo kujaza msiba. Na huwezi kuwalazimisha watu kusikitika. Hilo ni suala la hisia za moyo. Na nakuhakikishia utaishia kuwatesa tu kwenye vituo vya polisi. Hawashitakiki.

Mawakili wa serikali wana kazi nzito kipindi hiki hasa kwa suala la kumtia hatiani mtu aliyefurahia masahibu ya polisi. Ngoja tuone.
 
Tatizo hakuna sheria inayohukumu watu wanaocheka,kutaniana ama kutabasamu misibani,itabidi bunge lijalo itungwe.
Kasema kuwahoji sio kuwahukumu,yah wataitwa kuhojiwa.ni kuhojiwa tu si kuhukumiwa.
Tuambie watafanyaje?,weka hoja hapo. unakuta mtu kafungua email fake, namba ya simu fake kwanza alishaitupa miezi sita iliyopita, akaunt jf fake, jina lake halijulikani, uhalifu kafanyia internet cafe sio kwenye simu yake, unampataje mtuhumiwa?

Hawa ambao wanatapeli pesa katika makampuni kama mpesa,aitel nk hawpatikan wote,anatumia line na kutupa hawapatikani. juzi tu kuna mtu nilimwona ofisi ya vodacom anaomba msaada ametapeliwa fedha kupitia mpesa wakamwambia hawawezi kum trace mhalifu coz wanatumia line na kuzitupa ,
Sasa ukitiririka kwa style hii ya kutumia jina fake na kisha kutupa line ndio unakuwa umefanya upuuzi gani????.maana unawaogopa.

Just flow mpaka nukta katika uhalisia wako.mbona lissu hahangaiki na hayo yeye yakimfika anatapiga, just do it.utawaelewa tu.

Inamaana hata km hapo Police wakifanya madudu ktk utekelezaji wa majumu yao bas tuwashangilie? Jeshi la police la Tanzania baaado saana ktk ufanisi wa utekelezaji wa majukumu yao na kulinda uhuru, haki na amani katika nchi hii...Kabla ya kuogopa kutupiwa maneno au kubezwa wajiangalie kwanza kwa jicho la tatu na kujirekebisha...

Matter of fact, I got no love for them!!!!

Yaani mkuu kuwachukia polisi ni upuuzi.

Ni upuuzi kama wao wanavyopiga watu mkwara kwa lengo la kulazimisha heshima.

So pande zote mbili hazielewi zinafanya nini.
 
Polisi wetu wanafanya kazi nzuri sana. Nawashangaa sana wale wanaolibeza
Usishangae wakibezwa, unapaswa kijiuliza kwanini wanabezwa?, pia sina hakika kama kubeza jeshi ama hata mtu mmoja mmoja ni kosa, kama kubeza huko hakujafikia kiwango cha kuwa kashfa ama matusi.
 
Back
Top Bottom