Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Tukio limetokea muda gani ambao aliweza kubadili nguo na kutilia magwanda ya polisi na kwenda kwenye tukio? au alikuwa amevaa ametoka nayo ofisini?
Wachambuzi wa mambo wanasema magwandwa yalishapigwa pasi na mpiga picha alikuwa standby kwa ajili ya tukio.
 
Ni jambo la ajabu katika ulimwengu wa wastaarabu kushabikia ushenzi. Tukio lililotokea Mbande ni la kulaaniwa na wapenda Amani na watu watoe ushirikiano mkubwa kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha hao washenzi wanakamatwa na kufikishwa katika mkono wa sheria . wewe unayefurahia na kushabikia, hizo bunduki na risasi zilizoporwa zikitumika katika familia yako au biashara yako itakuwaje? Kuna haja kweli hao washabiki wakamatwe na Jeshi la polisi waieleze jamii ya watanzania na dunia kwa ujumla sababu ya ushabiki wao huenda itakuwa na faida katika kuweka hatua madhubuti kukomesha uhalifu huo.
 
Ifikie tuache kuwa panya we are men not mice-Tujifunze jambo linapotokea badala ya kutoa vitisho na matamko ambayo mwisho wa siku hayatatui tatizo na mbaya zaidi tatizo hilo hilo kujitokeza mbeleni.

Mkuu, kwa bahati mbaya hiyo ndiyo staili ya uongozi wa lumumba. Inasikitisha.
 
Yule msemaji wa Polisi,
Mara anasema majambazi hawajapora kitu, mara anasema kuwa wamepora bunduki mbili.

Polisi acheni siasa, fanyeni kazi, hii kazi ya usalama wa watu na mali zao inawashinda kwa ajili ya kujipendekeza kwa CCM.

Huyu CP NSATO, anajaribu kulihusisha tukio la kuuwawa kwa polisi na Operesheni UKUTA, hili halitakiwi kuwa tamko ya Polisi aliyesomea Intelligency, bali ilikuwa kazi ya propagandist wa CCM!

Akiongea kiongozi wa Polisi, na akiongea msemaji wa CCM, maneno ni yale yale!

Jirekebisheni!

Kwa kinachoendelea chini ya utawala wa Magu, mimi nimelazimika niishi katika hali ya kukandamizwa kama raia wa North Korea. Matamko ya kubambikiziwa na vitisho yamezidi uwezo wa fikra zangu Lol!
 
Walau wewe utakuwa kipenzi cha awamu hii. Kama Mungu atakujalia nguvu ya kudumu kuitetea serikali hii, ambayo wengi wanaona katiba inasiginwa nina imani utateuliwa kuwa mkuu wa wilaya. Sidhani kama utaitwa polisi kutolea maelezo.
Walau wewe utakuwa kipenzi cha awamu hii. Kama Mungu atakujalia nguvu ya kudumu kuitetea serikali hii, ambayo wengi wanaona katiba inasiginwa nina imani utateuliwa kuwa mkuu wa wilaya. Sidhani kama utaitwa polisi kutolea maelezo.
 
My Poor Tanzania.

Haya sawa basi! Hongereni sana Jeshi la Polisi mlipambana kiume bahati mbaya wazee wa boxer wakawazidi nguvu.
 
My Poor Tanzania.

Haya sawa basi! Hongereni sana Jeshi la Polisi mlipambana kiume bahati mbaya wazee wa boxer wakawazidi nguvu.
Kunapotokea hali ya sintofahamu ktk nchi ni vzr makundi hasimu wakae pamoja ili kuleta amani na utulivu hapa Tanzania.
 
Bado kuna muda na nafasi ya kuongelea haya masuala ya kudumisha amani hapa Tanzania. Nchi hii tujaribu sana kuilinda na kuitunza amani tuliyonayo.
 
Haya mauaji ya Polisi yachunguzwe kwa kina...kuna kitu hapa...sio bure......yachunguzwe kwa makini sana
 
Mimi Kwa Maoni Yangu, Mwigulu Ni mojawapo ya watu ambao Kwa Tukio Hili wanafaa wachunguzwe, Hili tukio lina Kila dalili ya Kuwa Lilipangwa kwa siasa. Masikini Watoto wa Watu, Askari wale wanne wanaweza Kuwa walitolewa Kafara na Watu waovu sana Kisiasa. Mungu Sii Mwanadamu Ukweli Utajulikana!
Sure Ayseee......Sirikali.
 
CHADEMA wameungana na Mafisadi kupigania maandamano badala ya kupigania maendeleo .!!!

Aliyewaambia watanzania wanahitaji maandamano na siyo maendeleo ni nani?

Shame to you all
Ndiyo mada tunayojadili hapa au?
 
Nguvu hazijawahi kufaulu sehemu yoyote duniani, waendelee kuwatisha tu, bora watu waendelee kuropoka hata siku kuna tukio wataropoka tu,ukiwafumba midomo sijui hata upelelezi mtaanzia wapi
Watanzania naomba tukae chini kama taifa na tujadili kuhusu amani yetu. Tusijaribu kuipoteza hii tunu tuliyoachiwa na waasisi wa taifa letu.
 
Unaweza kulazimisha hisia? Maana kuna wanaocheka, wanaohuzunika wanaoshangaa na pia wanaolia
 
Kwa comments za huu uzi ni wazi mapolisi wanatakiwa wajiulize wapi wamejikwaa. Huwezi kunilazimisha niwe rafiki yao na kuwapenda wakati wao wanaona ufahari kutisha na kunyanyasa wenzao kama hivi wameanza kutusaka. Poa nikamateni.
 
Inamaana hata km hapo Police wakifanya madudu ktk utekelezaji wa majumu yao bas tuwashangilie? Jeshi la police la Tanzania baaado saana ktk ufanisi wa utekelezaji wa majukumu yao na kulinda uhuru, haki na amani katika nchi hii...Kabla ya kuogopa kutupiwa maneno au kubezwa wajiangalie kwanza kwa jicho la tatu na kujirekebisha...

Matter of fact, I got no love for them!!!!
 
Hayo ni maneno ya Waziri wa Mambo ya Ndani mh. Mwigulu Nchemba kuwa kwa wale wote watakaoonesha kufurahia jambo hili wataitwa kwenye vyombo vya sheria kujieleza.

My take: Kabla ya kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kujieleza kwanini serikali isijiulize kwanini imefikia hatua mpaka polisi kuuawa wananchi wanashangilia?
Ukiwakamata uwapeleke mahakamani. Si polisi kama mnavyofanya. Wapeleke mahakamani ili mkajieleze wote.wewe mlalamikaji na yeye mshitakiwa. Hata hivyo ni ajabu kudhani kuwa kwenye msiba watu wote watalia! Wapo watakaofurahia kufa kwako, watakaosikikitika, na ambao wapo wapo kujaza msiba. Na huwezi kuwalazimisha watu kusikitika. Hilo ni suala la hisia za moyo. Na nakuhakikishia utaishia kuwatesa tu kwenye vituo vya polisi. Hawashitakiki.
 
Back
Top Bottom