Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Sinema juu ya sinema lazima nyeupe itabaki kuwa nyeupe na nyeusi itabaki kuwa nyeusi.
Jamaa analazimisha watu wenye furaha kuwa na huzuni kwa upande wangu atajisumbua. Hatuwezi kutishiwa na Silaha za kivita sisi raia tusiokuwa na hatia na wakati wanashindwa kuzitumia kwa majambazi. Maana yake ni kwamba jeshi la polisi Linatumia techniques za mkurya mwoga anayetishia mtu panga na kama Yule mtu naye akiwa mwoga akimbie na au akijaribu kukimbia amkate na panga. Lakini huyo mtu asipokuwa mwoga yaani mkurya hakukati na panga na badala yake atanywea ili usije ukamshikisha Ukuta... Over
 
Nyie polisi tatizo lenu mmeegemea upande mmoja wa serikali na Chama tawala, hamtendi haki, hamfanyi kazi kwa weledi.. Muheshimiwa amewapa kiburi,.. Eti mnapotubambia kesi na kutaka rushwa, mheshimiwa anasema ni hela ya kubrashia viatu,.. Tukikamatwa kwa Kosa lolote mmepewa makucha ya kutulaza chini, nanyi mkapandishwa cheo,.. Mahakama sasa haina kazi kwa raia wa kawaida, bali polisi anaweza kumaliza kila kitu.
Tangu nimezaliwa, sijawahi kusikia kamanda wa polisi akiamrisha jeshi lake "mtuhumiwa apatikane akiwa hai au MFU" kwa mara ya kwanza ni kwa awamu hii, na kama walikua wakiambiwa hivyo basi cc wananchi wa kawaida tulikua hatusikii kupitia vyombo vya habari. Mmetengeneza mpasuko mkubwa sana kati yenu na wananchi wa kawaida, mmejisahau Kuwa mpo kuwatumikia wananchi.. Matukio ya kubaka, kuwaibia wananchi, kuwapora Mali zao na kuwaua pasipo na hatia yoyote pindi migogoro inapojitokeza,.. Badala ya kutuliza na kulinda amani ya raia na Mali yake, nyie mwatumia nafasi hiyo kuleta balaa zaidi,.. Hayo yashajitokeza Arusha, Dar, Mtwara, Masasi, Tandahimba na mwanza.
Ushauri... Police msilazimishe kupendwa, lazima mujihoji kwann watu wanafurahia mnapopata matatizo? Hakuna mtu ambaye anaweza kuchukia mlinzi wake,. Tunaona hata wenye mbwa, hupenda mbwa wake kwakua anaamini humpa usalama wake na Mali yake, tena humgharamia chakula, malazi na mafunzo ili aweze kutimiza majukumu yake, Iweje kwa police tusiwapende kama wanawajibika na kutenda kwa haki? Lipo tatizo, na lazima kwanza kukubali na sio kuwatishia watu wasionyeshe hisia zao.
 
Mimi Kwa Maoni Yangu, Mwigulu Ni mojawapo ya watu ambao Kwa Tukio Hili wanafaa wachunguzwe, Hili tukio lina Kila dalili ya Kuwa Lilipangwa kwa siasa. Masikini Watoto wa Watu, Askari wale wanne wanaweza Kuwa walitolewa Kafara na Watu waovu sana Kisiasa. Mungu Sii Mwanadamu Ukweli Utajulikana!

Jamaa alienda eneo la tukio akiwa ndani ya gwanda. Najiuliza alipata wapi courage ya kuvaa gwanda usiku ule? Hivi na yy kwani ni polisi? Ana cheo gani? Kwan angeenda na nguo zake za kiraia kama waziri kingeharibika nn? Anyway Mungu anajua kuliko tunavyojua sisi.
 
Tatizo dunia imebadilika lakini binadam hawataki kuamini wapeni watu Uhuru wao kipindi cha kina mkwawa kimepita watu wanajitambua at a uko Libya sirya na kwengine mambo yalianza hivihivi serikali ijiulize LA sivyo watoto hawatasoma wala hakuna ataepata nafasi ya kufanya kazi yeyote
 
Hata yesu alisema awa wakinyamaza mawe yatapiga kelele
 
CHADEMA wameungana na Mafisadi kupigania maandamano badala ya kupigania maendeleo .!!!

Aliyewaambia watanzania wanahitaji maandamano na siyo maendeleo ni nani?

Shame to you all
Walau wewe utakuwa kipenzi cha awamu hii. Kama Mungu atakujalia nguvu ya kudumu kuitetea serikali hii, ambayo wengi wanaona katiba inasiginwa nina imani utateuliwa kuwa mkuu wa wilaya. Sidhani kama utaitwa polisi kutolea maelezo.
 
Mimi Kwa Maoni Yangu, Mwigulu Ni mojawapo ya watu ambao Kwa Tukio Hili wanafaa wachunguzwe, Hili tukio lina Kila dalili ya Kuwa Lilipangwa kwa siasa. Masikini Watoto wa Watu, Askari wale wanne wanaweza Kuwa walitolewa Kafara na Watu waovu sana Kisiasa. Mungu Sii Mwanadamu Ukweli Utajulikana!
Haito kuja kutokea bongo waziri kuojiwa, ila Kenya wameweza jana waziri wa michezo kaojiwa na vyombo vya usalama zaidi ya saa 2 kuhusu yaliyo tokea BRAZIL, chanzo bbc Swahili
 
Kwani ule mpango wa kuboresha usalama wa jamii uliozinduliwa viwanja vya Biafra tarehe 25/06/2016 ambao mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa raisi JP Magufuli uliishia wapi?
 
Hajasema wasikosolewe,kasema wale wote wanaoonyesha KUFURAHIA MAUAJI,soma vzr uelewe hapo mkuu

Tatizo hakuna sheria inayohukumu watu wanaocheka,kutaniana ama kutabasamu misibani,itabidi bunge lijalo itungwe.
 
Wakati jengo la kibiashara 'twin tower' kule Marekani lilishambuliwa na magaidi, kitendo hicho kililaaniwa karibia kona zote za ulimwengu, lakini kuna baadhi ya sehemu watu wengine walishangilia wakiona huo ulikuwa ushindi, je ni kwa nini? Hapa kwetu kitendo cha askari wetu kuuwawa kinalaaniwa na karibu kila mtu, lakini baadhi wanaonekana kufurahia, kwa nini? Cha muhimu kwa police wetu ni kuchunguza kwa undani sababu za watu wengine kushabikia kitendo hicho bila kutumia vitisho wala nguvu kubwa ili waliofanya hivyo watoe yao ya moyoni bila hofu. Uchunguzi huo unaweza kuibua mazito yatakoyosaidia police wetu kurekebisha makosa ya hapa na pale na kujenga uhusiano mzuri na raia.
 
Kuna watu wengi wanadhani hivyo ndivyo, lakini sivyo.

Tuambie watafanyaje?,weka hoja hapo. unakuta mtu kafungua email fake, namba ya simu fake kwanza alishaitupa miezi sita iliyopita, akaunt jf fake, jina lake halijulikani, uhalifu kafanyia internet cafe sio kwenye simu yake, unampataje mtuhumiwa?

Hawa ambao wanatapeli pesa katika makampuni kama mpesa,aitel nk hawpatikan wote,anatumia line na kutupa hawapatikani. juzi tu kuna mtu nilimwona ofisi ya vodacom anaomba msaada ametapeliwa fedha kupitia mpesa wakamwambia hawawezi kum trace mhalifu coz wanatumia line na kuzitupa ,
 
CHADEMA wameungana na Mafisadi kupigania maandamano badala ya kupigania maendeleo .!!!

Aliyewaambia watanzania wanahitaji maandamano na siyo maendeleo ni nani?

Shame to you all
Ukifanya maandamano maendeleo hayaji?
 
Back
Top Bottom