Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Ni vizuri uka koselewa kupitia weakness zako ukajipima na kujirekebisha,ndio mana kuna sanduku la Maoni hata mortuary .
Police inaposemwa vibaya au vizuri ni jukumu Lao kuchukua mazuri as motivation na Mabaya Kama changamoto,ili wayafanyie kazi kisawasawa for a better police force.
Sasa wao Kama wanataka kusemwa tu vizuri watazijuaje weakness zao .
 
JESHI la Polisi limefura. Ni kufuatia watu mbalimbali kulibeza mitandaoni kwa madai kuwa, limejikita katika matamko na mazoezi ya kukabili maandamano ya vyama vya siasa vya upinzani, kuliko kujipanga kukabiliana na uhalifu mkubwa ukiwemo ujambazi, anaandika Pendo Omary.

“Inashangaza kuona baadhi ya watu wanashabikia uhalifu kutokea kupitia mitandao ya kijamii na natoa onyo kali kwao, waache kuhamasisha uhalifu maana tunawasaka, tutawakamata na kuwahoji ili sheria ichukue mkondo wake.”

Jeshi hilo limesema, tayari limewakamata baadhi ya watu wakihusishwa na mauaji hayo.

======
MH! Nachelea kuamini kuwa Jeshi la Polisi linapinga kukosolewa kwa maana ile dhana ya 'kushirikiana na raia wema' inafutika kwa kasi. Nikiangalia hayo maneno kwenye alama za semi, natumaini mkuu alimaanisha 'kuhamasisha uhalifu' na si 'kukosoa jeshi la polisi'.

Ninaamini sheria zetu zinafafanua zaidi uhalifu ni nini, na hatua za kisheria za kudhibiti uhalifu. Kwa kuwa Polisi wetu wanapaswa kusimamia na kufuata Katiba na Sheria za Nchi, watazizingatia kwenye hatua zozote watakazozichukua.

Tukumbuke Tanzania ni moja na haitatokea nyingine kama hii. Wote ni wananchi kwanza kabla ya taaluma, nyadhifa au madaraka yoyote yale tuliyonayo. Hizi kofia tulizovaa na uwezo tuliojengewa, aidha kwa elimu au ujuzi, ni kutusaidia kuishi vizuri katika nchi hii na siyo kudhuru wananchi wengine. Ni rahisi sana kuharibu kuliko kujenga; hasa kwa maneno.
 
Hii serekali inawafanya wananchi wanalichukia jeshi la polisi, hii inawaweka polisi kwenye hali ngumu sana wakati wa utekelezaji wa majukumu yao! Mwigulu hajiulizi kwamba ukishawahoji ndio wananchi wataanza kulipenda na kuliheshimu jeshi la polisi?

Huwezi mlazimishi binadamu kupenda kitu nje ya utashi wake viongozi waache utoto!

Dawa ya jeshi la police kurudisha heshima yake na kupata uungwaji mkono na wananchi ni kuhakikisha jeshi la polisi halitumiki kisiasa hata kidogo!

Yaani jeshi ambalo lilitakiwa kufanya kazi zake kwa majibu wa sheria na taratibu zilizolianzisha leo linatumikia chama kimoja unadhani wanachama Wa vyama vingine ni vipofu au ni wajinga hawawezi kuona?

Ngoja tuanze kuvuna tulichopanda!
 
Ifikie tuache kuwa panya we are men not mice-Tujifunze jambo linapotokea badala ya kutoa vitisho na matamko ambayo mwisho wa siku hayatatui tatizo na mbaya zaidi tatizo hilo hilo kujitokeza mbeleni.
 
hayo ni maneno ya wazir wa mambo ya ndani..mh Mwigulu kuwa kwa wale wote watakaoonyesha kufurahia jambo hili wataitwa kwenye vyombo vya sheria kujieleza..

my take,kabla ya kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kujieleza...kwa nn serikali isijiulize kwa nn imefikia hatua mpaka polisi kuuwawa wananchi wanashangilia..nn tatizo mpaka inatokea hivi??
Dah yaani kwa kifupi wanofurahia ni wamojawapo watasaidia kujua kwa nini askari wanauwawa.
 
Cha msingi ukiona unakosolewa jichunguze wapi unakosea wapi una mapungufu unachotakiwa ni kukusanya maoni toka kwa watu ili ujipime kuhusu utendaji wako
 
naona una mastress zako.kwakukaza misuli ya shingo, umgeni nini humu JF. familia ya JF huwa tuna uvumilivu, hakuna mtu anawabeza polisi wetu lazima wote tuheshimiane. kuna kitu kinaitwa bill of rights and rule of law
Sasa kati yangu na yako nani anaonyesha hayo "mastress". Unanihukumu kwa tarehe niliyojiunga na JF? Ha ha ha.
 
CCM mnazidi kupuliza moto,i don't know when you will realize you are confusing us ,we want peace,peace! I think kwenye serikali yenu hakuna mtu specially anayekuwa responsible wa KURESOLVE CONFLICTS?

Kama hamna ombeni msaada hata nchi jirani. mkiingiliwa na materrorist je?au God forbid itokee civil war? si tutachinjana kama kuku?

Hata mkizuia maandamano,tayari ukuta imecreate mgawanyo,msidhanie hata wasiokwenda kwenye UKUTA,bado wana ndugu zao ambao wataenda,sie wengine tutabaki kuwaombea tu warudi salama,hamjui wote tutakaobaki na wote watakaoenda siku hio tuko na UNCERTANITIES ???,hamuoni mmeleta machafuko na matamshi yenu ya kibabe.???
 
Back
Top Bottom