Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Hivi kwa akili za kawaida tu polisi inayo rasilimalima ya kuzuia maandamano vitongoji vyote vya dar es saalam tu achilia mbali Tanzania nzima.
 
Kiongozi mkuu wa nchi ndie mwenye kutoa taswira ya nchi, kama anapenda kusifiwa basi utaona hata taasisi zote zitahitaji kusifiwa, nimeona bandari walikanusha kuwa hakuna upungufu wa mizigo, maana yake wananchi waseme tu kumejaa, wakaja crdb, sasa polisi. Ni sifa tu vyovyote itakavokua.
 
Na mkifanye huo msako mtazidosha chuki dhidi yenu,
Bora mjirekebishe kimya kimya
 
Sasa ni mwendo wa kusifia tu...ngoja na mie nianze kwa kulisifia jeshi letu tukufu la polisi kwa kuonyesha kwa vitendo mazoezi na utayari wao wa kukabiriana na uhalifu.

Hakika Tanzania tumejaaliwa kuwa na jeshi imara la polisi lenye intelijensia makini kabisa duniani.

Hongera sana kamishina wa operation na mafunzo Nsato Marijani hakika wewe ni kiongozi wa mfano. Usisite kuwachukulia hatua kali wale wote wanaobeza mafanikio ya jeshi letu tukufu la polisi.
 
Aisifuye mvua imemnyea. Mkuu Lizaboni anawasifu polisi kwa kuwa imewasaidia kwa kiasi cha kutosha kuwadhibiti UKAWA na kuistawisha CCM...na hii ndio furaha ya kila mwanaCCM...kuhakikisha kwamba upinzani unadhibitiwa kwa gharama zozote zile.

Unajua mkuu, ni kama vile utawala wa CCM umekamia kuadhirisha taasisi zetu za umma kwa kuzigeuza wapambe wake badala ya nyenzo thabiti za kushughulikia majukumu yake. Ona sasa, polisi badala ya kusifika na kuheshimika kwa udhibiti makini wa uhalifu, wanajulikana zaidi kwa kutisha na kupambana na vyama vya upinzani, wanahabari, raia na wanaharakati wanaokosoa serikali na chama tawala. Na kusanya rushwa, kubambikia watu kesi, n.k.

Wanapokabiliwa na wahalifu wa kwelikweli wanaishia kujikanyagakanyaga na kutoa matamko ya kisiasa. Tunataka kuona heshima ya jeshi letu la polisi inarudishwa. We need to look at the guys with pride not embarrassment!
 
unajua kama huishi na watu siku ukifiwa msiba wako utakuwa na watu wachache, hivyo tuishi kwa kupendana. hakikisha hauonei mtu tenda wajibu wako usimkandamize mtu yyt. vinginevyo ndio hivyo ukifa watu wanafurahia. ni somo mjifunze.
 
Bado inaonyesha wazi jinsi gani polisi wanakosa weledi na uvumilivu. Waache watu waeleze hisia zao. Kilichofanyika ni uzembe wa hali ya juu. Polisi wasitumie defensive mechanism kuficha udhaifu wao. Tumewaona mitaani wakitamba na silaha nzito, tumesikia mara nyingi wakisema wana intellejensia kali, inakuwaje intellejensia ya polisi ishindwe kubaini mipango ya waharifu waliyotekeleza tukio la jana usiku? Kuwashambulia wanaotoa maoni siyo suluhisho la matatizo. Wao polisi wapambane na waharifu. Kugeukia wananchi wanaotoa maoni yao na kuelezea mawazo yao kuhusu utendaji wa kiwango cha chini cha jeshi la polisi na kuacha kushughulikia kiini cha tatizo ni kuonyesha jinsi gani jeshi la polisi halina uwezo wa kukabiriana na matukio ya kiharifu kama lile lilotokea jana.
Ukweli mara nyingi unauma ndugu yangu.
 
Jivu lenye moto hata kama halifuki moto linachoma tu, suala muhimu kujua kosa liko wapi na kurekebisha kuliko kuweka jivu lenye moto ukafikiri halitachoma
 
nimezungumza na watu juu ya jambo hili maelezo yao yamenisikitisha sana nilichogundua ni kua wanawanchi kwa kiasi flani wanachuki na askari wakidai askari ni waonevu ila kwa MTU mzalendo kabisa na mwenye ajili zinazomsaidia katika kufikiri huwezi simama upande wa mhalifu dhidi ya askari.
 
JESHI la Polisi limefura. Ni kufuatia watu mbalimbali kulibeza mitandaoni kwa madai kuwa, limejikita katika matamko na mazoezi ya kukabili maandamano ya vyama vya siasa vya upinzani, kuliko kujipanga kukabiliana na uhalifu mkubwa ukiwemo ujambazi, anaandika Pendo Omary.

Askari wanne waliuawa katika tukio la ujambazi lililotokea usiku wa jana, eneo la Mbande, Mbagala jijini Dar es Salaam na kuibua maoni tofauti ya wananchi katika kipindi hiki ambacho polisi wamekuwa wakijitokeza mitaani na kufanya maonyesho kwa madai ya kujiweka tayari kuwakabili wahalifu.

Nsato Marijani, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi hapa nchini amewambia wanahabari hii leo kuwa, jeshi hilo halitavumilia ‘ushabikiaji’ wahalifu unaofanywa na baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii huku wakilibeza jeshi la polisi.

CP Marijani aliwaita wanahabari ili kuzungumzia mazingira ya tukio la kutokea kwa mauaji ya askari wa jeshi hilo siku ya jana, ambapo amesema, kitendo kilichotokea jana sit u ni uhalifu bali ni “tangazo la vita dhidi ya Polisi”.

“Wahalifu walifanikiwa kupora bunduki zetu mbili aina ya SMG na risasi 60 na hawakuchukua pesa wala kuharibu mali yoyote ya benki hiyo. Maana yake wahalifu hao walilenga kuwashambulia askari polisi wetu,” amesema na kusisitiza;

“Inashangaza kuona baadhi ya watu wanashabikia uhalifu kutokea kupitia mitandao ya kijamii na natoa onyo kali kwao, waache kuhamasisha uhalifu maana tunawasaka, tutawakamata na kuwahoji ili sheria ichukue mkondo wake.”

Jeshi hilo limesema, tayari limewakamata baadhi ya watu wakihusishwa na mauaji hayo.

======

Hiyo utakuwa kile kinachoitwa "knee jerk reaction"! Badala ya jeshi letu kuangalia lilipojikwaa linahangaika na lilipoangukia; polisi ni ndugu zetu, ni baba na mama zetu, ni rafiki na majirani zetu, hatuwezi kushangilia wanapoumizwa au kuuwawa kama tunavyolaani mazingira mabovu ya kazi zao wakati watumishi wengine wanaishi kama malaika! Lakini pia hatuwezi kufumbia macho tunapoona vipaumbele vya kazi za jeshi letu la polisi vinakwenda ndivyo sivyo, kutukamata na kutufunga hakutatui tatizo la vipaumbele vya kazi, watatufunga na kutuua lakini kama hawazitumii criticism za mitandaoni kujitafakari labda tatizo litabaki palepale na vizazi vijavyo pia vitawacriticise tu and the cycle continues!


Hiyo utakuwa knee jerk reaction, badalakuangalia ulipojikwaa
 
mie naona watu hao wasakwe, kwa kuws hata kama MTU unamchukia kiasi gani si vema ufurahi kwa yeye kufikwa na baya...kwanza inaonesha kuwa hawa washangiliaji wanahusika kama sivyo basi no watu wenye mihemuko ya siasa bila kujielewa. kwa mfano MTU anahukumiwa kwa kumtukana raising alafu chama Fulani kinajitangaza kupitia watu wake kuwa kitalipa faini hiyo...jibu ni moja tu kuwa chama hicho ndicho kimemtuma atukane...ningekuwa magufuli sijui ingekuwaje!
 
Mimi naona sasa iwe mwisho kwa form four failures kujiunga Na jeshi la police , angalau jeshi la police wachukue form six Na sio failures wa dv zero labda division four mwisho. then wa encourage hawa vijana wetu wanaofeli form four kujiunga Na vyuo vya ujuzi kwanza wakishakua matured enough ndio wajiunge Na jeshi la police , hii itaepusha watu waliopo kwenye late adolescence kupewa mamlaka ya kushika silaha Na kulinda watu , pia mafunzo shallow ya miezi 9 hayatoshi kwa police , iyo miezi 9 wangesoma kwanza somo la saikolojia Na Haki za binadamu Na somo la kujitambua wao binafsi then miez 9 mingine wajifunze mbinu za kijeshi , wajifunze wa police wa nchi zingine , kupiga watu Na kuua sio kazi ya police , nchi zlizopiga hatua police akiua Mtu lazima uyo police atauliwa Na raia au kufungwa kifungo kirefu kwasababu amekwenda kinyume Na misingi ya jeshi la police . kuna haja ya ELIMU ELIMU ELIMU. jeshi la police linapaswa kimlinda raia Na Mali zake Na sio Mali Na raia ni lazima aanze raia kisha Mali ndio patakua Na urafik mzur Kat ya police Na wanananchi , ila wakilinda Mali kisha raia basi hapo hali itakua mbaya sana . haya mambo yanahitaji darasa , Na sio la miez9 , at least 2 years Mtu usome Na afanye mitihani sio mtu anakuaga leo naenda CCP. baada ya miezi kadhaa asharud anakuambia Mimi ni police....... let's be serious.
 
mie naona watu hao wasakwe, kwa kuws hata kama MTU unamchukia kiasi gani si vema ufurahi kwa yeye kufikwa na baya...kwanza inaonesha kuwa hawa washangiliaji wanahusika kama sivyo basi no watu wenye mihemuko ya siasa bila kujielewa. kwa mfano MTU anahukumiwa kwa kumtukana rais alafu chama Fulani kinajitangaza kupitia watu wake kuwa kitalipa faini hiyo...jibu ni moja tu kuwa chama hicho ndicho kimemtuma atukane...ningekuwa magufuli sijui ingekuwaje!
 
Mimi naona sasa iwe mwisho kwa form four failures kujiunga Na jeshi la police , angalau jeshi la police wachukue form six Na sio failures wa dv zero labda division four mwisho. then wa encourage hawa vijana wetu wanaofeli form four kujiunga Na vyuo vya ujuzi kwanza wakishakua matured enough ndio wajiunge Na jeshi la police , hii itaepusha watu waliopo kwenye late adolescence kupewa mamlaka ya kushika silaha Na kulinda watu , pia mafunzo shallow ya miezi 9 hayatoshi kwa police , iyo miezi 9 wangesoma kwanza somo la saikolojia Na Haki za binadamu Na somo la kujitambua wao binafsi then miez 9 mingine wajifunze mbinu za kijeshi , wajifunze Kwa police wa nchi zingine , kupiga watu Na kuua sio kazi ya police , nchi zlizopiga hatua police akiua Mtu lazima uyo police atauliwa Na raia au kufungwa kifungo kirefu kwasababu amekwenda kinyume Na misingi ya jeshi la police . kuna haja ya ELIMU ELIMU ELIMU. jeshi la police linapaswa kimlinda raia Na Mali zake Na sio Mali Na raia ni lazima aanze raia kisha Mali ndio patakua Na urafik mzur Kat ya police Na wanananchi , ila wakilinda Mali kisha raia basi hapo hali itakua mbaya sana . haya mambo yanahitaji darasa , Na sio la miez9 , at least 2 years Mtu usome Na afanye mitihani sio mtu anakuaga leo naenda CCP. baada ya miezi kadhaa asharud anakuambia Mimi ni police....... let's be serious.
 
mie naona watu hao wasakwe, kwa kuws hata kama MTU unamchukia kiasi gani si vema ufurahi kwa yeye kufikwa na baya...kwanza inaonesha kuwa hawa washangiliaji wanahusika kama sivyo basi no watu wenye mihemuko ya siasa bila kujielewa. kwa mfano MTU anahukumiwa kwa kumtukana raising alafu chama Fulani kinajitangaza kupitia watu wake kuwa kitalipa faini hiyo...jibu ni moja tu kuwa chama hicho ndicho kimemtuma atukane...ningekuwa magufuli sijui ingekuwaje!
Wewe adui yako akipatwa na mabaya hutoshangilia? Polisi ni adui wa wananchi kutokana na manyanyaso na uonevu wanaoufanya katika jamii. ndo maana watu wanashangilia pindi polisi wapatapo matatizo.
 
Polisi haina haja kulalama angalieni ni wapi mnakosea na kuwa adui na RAIA Panapofuka moshi zima moto chini siyo kumwagia petrol.

Haya mazoezi yanayoendelea kwaajiri ya UKUTA ingakuwa ni tokomeza ujambazi hakuna hata mdokozi angebaki huru.
 
Hayo ni maneno ya Waziri wa Mambo ya Ndani mh. Mwigulu Nchemba kuwa kwa wale wote watakaoonesha kufurahia jambo hili wataitwa kwenye vyombo vya sheria kujieleza.

My take: Kabla ya kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kujieleza kwanini serikali isijiulize kwanini imefikia hatua mpaka polisi kuuawa wananchi wanashangilia?
 
Back
Top Bottom