Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

Wanaowabeza Polisi mitandaoni ‘kushughulikiwa’

hayo ni maneno ya wazir wa mambo ya ndani..mh Mwigulu kuwa kwa wale wote watakaoonyesha kufurahia jambo hili wataitwa kwenye vyombo vya sheria kujieleza..

my take,kabla ya kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kujieleza...kwa nn serikali isijiulize kwa nn imefikia hatua mpaka polisi kuuwawa wananchi wanashangilia..nn tatizo mpaka inatokea hivi??

Najiuliza swali namna ya kuwapata coz ID feki ndo kanuni za jf, mtu alienda internet cafe ndo akaandika maoni yake ambayo hayakuifurahisha serikali na akaunt iliyotumika asiitumie tena, watampataje?
 
CHADEMA wameungana na Mafisadi kupigania maandamano badala ya kupigania maendeleo .!!!

Aliyewaambia watanzania wanahitaji maandamano na siyo maendeleo ni nani?

Shame to you all
 
Mwigulu pole pole kaka..... mpigie simu T.B.Joshua usali nae n kupata maoni yake.... nafasi uliyo nayo ni kila kitu Tz..... waweza jenga au bomoa nchi.... kwa kusali na T.B.JOSHUA utaweza......
 
najiuliza swali namna ya kuwapata coz ID feki ndo kanuni za jf, mtu alienda internet cafe ndo akaandika maoni yake ambayo hayakuifurahisha serikali na akaunt iliyotumika asiitumie tena, watampataje?
Hapo ndipo mnapokosea.
 
Mbona kila saa anatoa matamko ya vitisho?? Why???
Mimi Kwa Maoni Yangu, Mwigulu Ni mojawapo ya watu ambao Kwa Tukio Hili wanafaa wachunguzwe, Hili tukio lina Kila dalili ya Kuwa Lilipangwa kwa siasa. Masikini Watoto wa Watu, Askari wale wanne wanaweza Kuwa walitolewa Kafara na Watu waovu sana Kisiasa. Mungu Sii Mwanadamu Ukweli Utajulikana!
 
Mwigulu teach Tanzanian's how not to think. Sote tuwe mazuzu ya kuchezewa akili na chama tawala.
 
wasikosolewe wao kama kina nani? acha watu waongee wana haki ya kuongea chochote
kama kila siku unataka kusifiwa tu mapungufu lazima yasemwe tu
Hajasema wasikosolewe,kasema wale wote wanaoonyesha KUFURAHIA MAUAJI,soma vzr uelewe hapo mkuu
 
Nguvu hazijawahi kufaulu sehemu yoyote duniani, waendelee kuwatisha tu, bora watu waendelee kuropoka hata siku kuna tukio wataropoka tu,ukiwafumba midomo sijui hata upelelezi mtaanzia wapi
 
Siku hizi kuna misiba inakosa waombolezaji mpaka vinakodiwa vikundi vya kulia mwanzo mwisho.
Huwezi kulazimisha mtu aomboleze jambo ambalo halija mgusa, kama anataka hivyo naye atafute makundi ya kulipwa kuomboleza roho yake ifurahi.
 
Hayo ni maneno ya Waziri wa Mambo ya Ndani mh. Mwigulu Nchemba kuwa kwa wale wote watakaoonesha kufurahia jambo hili wataitwa kwenye vyombo vya sheria kujieleza.

My take: Kabla ya kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kujieleza kwanini serikali isijiulize kwanini imefikia hatua mpaka polisi kuuawa wananchi wanashangilia?
Serikali ndiyo inawachonganisha wananchi na polisi
 
Majizi Chadema wameungana na Mafisadi kupigania maandamano badala ya kupigania maendeleo .!!!

Aliyewaambia watanzania wanahitaji maandamano na siyo maendeleo ni nani ??

Shame to you all
Umeshawahi kuandika kwa kufikiri au hapo ndio unetumia akili kufikiri?
 
Damu za polisi waliouawa ambao hawana hatia zinawalilia ndomana wanaweweseka
 
Back
Top Bottom