Ngoja nikupe taratibu ya ibada mbali mbali.
Wakristu,
Kundi hili tuna RC, wasabato, anglican, waluteli na waprotestant. Wasabato wao hufanya ibada zao jumamosi, hii siku dunia nzima inajulikana kama ni siku ya MAPUMZIKO!
Kundi la Rc, waprotestant, waluteli na anglican hawa hufanya ibada zao jpili, hii nayo inajulikana kama ni sikj ya MAPUMZIKO!
Waisilamu wao hufanya ibada yao kuu ijumaa, hii si siku ya mapumziko ILA, INAHESHIMIKA na KUTAMBULIKA dunia nzima kama siku ya ibada. Na waajiri wakristu mpaka wahindu wanaitambua.
Hizi ni taratibu zipo na zinatambulika na zimeleta balance duniani ever since.
Kuhusu swala la jumuiya! Ni kukosa weredi na heshima kuingilia mipaka ya mtu kuabudu especially katika siku ya mapumziko! Argument yako ni kuwa wakafanye kazi waache kusali, siku ya jmosi ambayo ni siku ya mapumziko ni watu wangapi huwa wamelala (wamepumzika) katika muda huo.ambao wengine wanasali?! Jiulize ni wangapi wenye MAENDELEO kuliko wewe huwa wamepumzika katika siku hiyo ya jumamosi, maendeleo yako wewe ni yapi mpaka uwabeze wenzako?!
Mfano ndugu zangu waislamu, wao hutakiwa na kitabu chao kitukufu kusali swala tano kila siku (si ujumaa tu), je nao wauvunje amri hiyo kisa tu kufanya kazi?! Nchi ngapi za kiarabu wanasali hadi katikati ya muda wa kazi na wana maendeleo kutuzidi sisi ambao tunasali katika siku maarumu (jmosi, jpili na ijumaa).
Kuhusu eti huko jumuiya watu wanaenda kuchukua namba na kwenda kuvunja amri ya sita, hii ni argument ya kitoto sana!! Hayo mambo ni hulka ya mtu tu, kwani makazini watu hawachukui namba na kwenda kuivunja hiyo amri😱
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, jifunze kuheshimu mambo ya watu wengine, si busara kupayuka katika kila jambo hata lile ambalo hauna maarifa nalo.