Wanaomkosoa Nyerere wana hoja?

Shamu na Gamba la Nyoka naona mpo kundi mojawapo katika makundi aliyoyasema Eng Burton ... hata hivyo kauli ya ninavykumbuka mimi, nilimsikia akionesha dosari ya katiba yetu tuliyo nayo na si kutishia wananchi wake.

Mimi shida kubwa naoiona katika muktadha wa kipimo cha ulinganifu wa sifa za Nyerere na hali duni ya Tanzania ilivyo leo. Nyerere alisifika sana kwa harakati zake za kulikomboa bara la Afrika, kupigana vita na kumng'oa madarakani dictator Idd, umoja alioujenga kwa watu wake, muungano wa Zanzibar na Tanganyika na siasa yake ya pekee duniani. Je kwanini nini leo nchi iliyojaaliwa kuwa na kiongozi mahiri na wa pekee namna hiyo leo iko chini kisiasa na kiuchumi kiasi cha kufananishwa na kichwa cha mwendawazimu? Nchi inayouza ardhi yake kwa nchi za nje! Nchi inayoruhusu ndege za kijeshi kutua nchini na kuiba wanyama hai? Nchi inayofuga ufisadi na mafisadi wakubwa bila kuchukua hatua zozte! Nchi ambayo wageni ndio matajiri na wanapenyeza katika uongozi wa nchi yetu! Je kwanini ? Haya hayakuwepo wakati wa mwalimu...


Ninavyoona ni kuwa hali hiyo ndio inayozaa maswali magumu yaliyopo sasa ndani na nje ya nchi. Lakini kama wazungumzaji wengie walivyosema, (1) huenda udhaifu wa watawala wa sasa unatafuta kisingizio cha kuficha udhaifu "failure" kubwa katika nchi. Kumbuka habari ya Adam kumsingizia Hawa, na Hawa kumsingizia nyoka ili kuficha uhusika wao kwa kosa walilotenda. (2) Kuna baadhi ya watu (wenye lengo lao) ambao uongozi wa Nyerere uliwadhibiti wao au jamaa zao (kuwagandamiza watu wa Tanganyika, wajinga na masikini), sasa wanapata fursa ya kumlaumu Nyerere kwasababu ambazo hawajaziweka wazi. Hawa watu hawawezi kuona uzuri wa nia njema ya Mwalimu na maamuzi magumu kama kutaifisha mabenki, mashule, mashamba, nk. Wao walitamani ubepari uendelee kuwapa fursa ya kushika njia kuu za uchumi ili washike uchumi wa nchi yetu kibinafsi. Na kinachoendelea sasa hivi ktk sera ya ubinafsishaji na ufisadi ni kufufuka kwa mipango ileile ya zamani.

Mwisho nasema hivi: Kama tuna dhamira safi, naomba tukosoe sera za Nyerere kwa kupendekeza sera mbadala zilizo nzuri zaidi kama zipo. Bila kufanya hivyo tutaishia kuonekana ama tuna chuki dhidi ya Nyerere au tuna sababu nyingine. Na tusisahau kuwa, Nyerere hakuiba hata cent moja ya nchi yetu, kwanini yeye ndiye awe chanzo cha kushindwa kwa nchi badala ya hao wezi waliomfuatia? Serikali ya Nyerere haikuwa na pesa nyingi sana, lakini haikuwahi kufikia uamuzi wa kuuza kipande cha ardhi yake kwa wageni, au kuingia mikataba ya kifisadi iliyopo hivi leo kwenye mali asili ya taifa. Serikali ya Nyerere haikuwahi kuruhusu wageni kujichotea maliasili yetu huku wakionesha dharau kwa wananchi wazawa kwa kuwadhalilisha na hata kuuua, rejea tukio la Merelrani, Nyamongo na sehemu zingine. Kwakweli tusifanye kazi ya kumtetea Baraba na kumhukumu Masihi mwema.

Kumbuka hata kama hakuiba hata cent moja, lakini kawafilisi WTZ kwa sababu ya sera zake za Ujamaa.
Hii quote kutoka ktk well said article ambayo inazungumzia pia kuhusu Ujamaa wa Nyerere na Udictator wake.

Three of these factors are pertinent to this discourse. Firstis the argument that the initiative to start Ujamaa villages did not comefrom rural peasants. The scheme failed to gain the necessary ideologicalacceptance among the vast majority of the peasantry. Right from the beginning,the dominant attitudes of the people ranged from skepticism and mistrustto outright resentment and opposition (Lofchie, 1978: 452). Secondly,the use of coercion to ensure mass villagization - from threats of forcedtransportation to short prison sentences under the pretext of tax arrears -militated against the effective operation of Ujamaa villages. Finally, theefforts at building Ujamaa villages were greatly constrained by bureaucratswho held out government aid as incentives to peasants to move into villages.Peasants began to perceive such "free goods" as substitutes for availablelabor resources rather than being complimentary factors for increasedproduction. Promises of official assistance resulted in an over-dependenceof the villages on government initiatives and incentives that left villagesextremely vulnerable when government assistance eventually stopped.However, perhaps the single most adverse limitation of the Ujamaa villagizationprogram was the practice which Shivji (1974) and Raikes (1975)have described as "Kulak Ujamaa". This was a practice in which a numberof rich peasants, having attained positions in Ujamaa village committees orforged links with local bureaucrats, began to use the villages to further theirown interests.



Kwa hiyo ukisoma hiyo article vizuri utagundua haya matatizo yote yalianzia wakati wa Nyerere.
 
Kuna wale waliopinga hoja zake, na walitishiwa na Nyerere mwenyewe.
Hii video clip ni ushahidi tosha.
Films On Demand - View Playlist#
Lakini hawakuandamana. Maandamano yote yalifanywa na wapenzi wa Arusha declaration na ukombozi mpya wa Mtanzania.
Umezungumzia maandamano, nakujibu kuhusu maandamano. Hayo ya kupinga hoja za Nyerere ni suala jingine kabisa. Huwezi kukuta popote pale binadamu wote wakakubaliana 100%. Lete jingine.
 
Nimesoma mara tano hoja zako nikijaribu kuelewa na kufikiri kwa undani juu ya ulichoandika naomba nirejee mambo kadhaa ambayo naamini yatatufanya tujadili kwa mapana zaidi.

Kwanza kabisa nitatumia mfano huu rahisi wa wanafunzi wa shule ya boarding ambao wanavaa sare tufanye shati jeupe na suruali nyeusi, kwa mazingira haya iwapo mmoja wapo anatafuta umaarufu kwa njia rahisi kabisa anachofanya ni kujitahidi kuwa unique/ wa pekee mfano yeye atavaa bukta na shati la kijani, mara moja atajikuta yeye ndiyo anatazamwa sana kutokana na utofauti wake na wenzake.

Halikadhalika tuchukulie mfano wa mapadre wa kanisa katoliki hawaoi ila akitokea mmoja akaoa anajenga umaarufu na anatamkwa sana na watu kutokana na kitendo chake hiko mfano Askofu Emanuel Milingo wa Lusaka Zambia, na labda niweke hoja yangu clear kwa kusema kuwa umaarufu wa hapa siyo tu wa kupongezwa bali wa ushujaa hata ikiwa anakosea mifano ni tabia ya baadhi ya wasanii wa kizazi kipya kutafuta skendo ilimradi wapambe kurasa za magazeti.

Sasa kuhusu NYERERE tayari ipo wazi kuwa watanzania wengi wanamheshimu, sasakumheshimu Nyerere imekuwa common haishangazi lakini anapoibuka mtu ambaye anamkosoa hali inakuwa tofauti mfano anaweza kuonekana shujaa au jasiri huu ndiyo umaarufu ninaosema wanautafuta.

Sasa kuna tatizo pia kuhusu 1995 ambapo Nyerere hakukosolewa hivi mimi siamini kuwa watu wote walimwogopa, nasema hapana hata kidogo hapa tunapaswa tujihoji mara mbili labda nitoe wazo tulifikirie kwa mantiki, mimi nadhani 2005 wakati kikwete anaingia kwa mbwembwe kuna baadhi ya waandishi na wachambuzi mahiri wenye majina makubwa walilewa mbwembwe zake nao wakamuunga mkono sasa kawaangusha sana kiasi kwamba maandiko yao yanawasuta sasa wanaamua kutumia udhaifu wa NYERERE kumjenga kikwete eti wanadai Nyerere ndiyo kaweka misingi mibovu? how? hata huyo KIKWETE si kasoma bure kutokana na sera nzuri za kufuta ujinga za Nyerere sasa mbona yeye katujengea mitambo ya kuzalisha sifuri? hizi shule za kata na bado kuna watu wanamuunga mkono? kuna nini hapa?

Utawala wa Nyerere unaangaliwa kwa sababu Azimio la Arusha lilikuwa ni KUFELI kwa Nyerere. Soma article niliyoipost ili uelewe vizuri mfumo wa Vijiji ulivyofeli kwa sababu ya idea za Nyerere.
 
Kumbuka hata kama hakuiba hata cent moja, lakini kawafilisi WTZ kwa sababu ya sera zake za Ujamaa.
Hii quote kutoka ktk well said article ambayo inazungumzia pia kuhusu Ujamaa wa Nyerere na Udictator wake.

Three of these factors are pertinent to this discourse. Firstis the argument that the initiative to start Ujamaa villages did not comefrom rural peasants. The scheme failed to gain the necessary ideologicalacceptance among the vast majority of the peasantry. Right from the beginning,the dominant attitudes of the people ranged from skepticism and mistrustto outright resentment and opposition (Lofchie, 1978: 452). Secondly,the use of coercion to ensure mass villagization - from threats of forcedtransportation to short prison sentences under the pretext of tax arrears -militated against the effective operation of Ujamaa villages. Finally, theefforts at building Ujamaa villages were greatly constrained by bureaucratswho held out government aid as incentives to peasants to move into villages.Peasants began to perceive such "free goods" as substitutes for availablelabor resources rather than being complimentary factors for increasedproduction. Promises of official assistance resulted in an over-dependenceof the villages on government initiatives and incentives that left villagesextremely vulnerable when government assistance eventually stopped.However, perhaps the single most adverse limitation of the Ujamaa villagizationprogram was the practice which Shivji (1974) and Raikes (1975)have described as "Kulak Ujamaa". This was a practice in which a numberof rich peasants, having attained positions in Ujamaa village committees orforged links with local bureaucrats, began to use the villages to further theirown interests.



Kwa hiyo ukisoma hiyo article vizuri utagundua haya matatizo yote yalianzia wakati wa Nyerere.

Mkuu Shamu ningefanikiwa kujua umri wako pengine ningekuwa na mtazamo tofauti na maelezo yako juu ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
 
Duuh! Nyerere kweli ana matatizo yake lakini ukweli wa mambo ni kuwa by far, amejitahidi na alifanikiwa sana kwa yale aliyoyaamini. Hawa jamaa tulionao wameshindwa kabisa...ni total failures kwahiyo ili kujinusuru na hukumu ya historia, wanajaribu kuiandika upya historia ya uongozi wetu kwa kutufundisha somo jipya kwamba Nyerere was just like them...alishindwa kutatua matatizo na wao pia yamewashinda....what a waste of resources kuwachagua hawa vilaza kutuongoza??? wanafikiri ukubwa ni kutumia polisi kuwasafishia njia halafu na kutumia hela za walipa kodi kujitajirisha.
 
Lakini hawakuandamana. Maandamano yote yalifanywa na wapenzi wa Arusha declaration na ukombozi mpya wa Mtanzania.
Umezungumzia maandamano, nakujibu kuhusu maandamano. Hayo ya kupinga hoja za Nyerere ni suala jingine kabisa. Huwezi kukuta popote pale binadamu wote wakakubaliana 100%. Lete jingine.


Soma vizuri hii article. Nazumgumzia Udictator wa Nyerere na utumiaji wake wa power ya Udictator dhidi ya WTZ.

the Ujamaa villagization scheme (Ujamaa vijijini) wasadopted for the rural sector. Indeed villagization was a central goal ofUjamaa. According to the policy statement of Ujamaa Vijijini - "Socialismand Rural Development" - the aim of the scheme was to initiate the transformationof rural society to create "rural economic and social communitieswhere people would live together for the good of all" (Nyerere, 1968: 337).It advocated the development of Ujamaa villages in which people wouldhave their homes around a common service center - instead of living onscattered homestead plots - and land farmed by cooperative groups ratherthan by individual farmers. Nyerere legitimized the villagization scheme interms of traditional African practices of communal living and social equity.Despite initial enthusiasm and early successes, the Ujamaa villagizationscheme soon ran into difficulties, as people became increasingly reluctant tojoin Ujamaa villages. This, coupled with the rising cost of providing materialincentives for the villages, engendered a move towards forceful methodsof persuading people into collective villages - a method that the regime hadearlier condemned and resolved not to employ. 1970 for instance, saw thestart of "Operation Rufiji" whose idea was to move "by coercion if necessary",the whole population of the lower Rufiji floodplain into Ujamaa villageson higher ground not so near the river. There was also "OperationDodoma" conceived to solve the problem of the Dodoma region by movingall the people in the region into planned villages (Coulson, 1975: 55). In1972, more "operations" were launched in Chuya and Kigoma. In the event,many of these operations turned out to be failures since local peasants, suspiciousof official motives and fearing the nationalization of their land,refused to cooperate. By late 1973, after many of these operations - the militaryanalogy being quite apt
 
Nitarudia tena kusema kwa wote wanaomlaumu Nyerere ni watu ambao hawajui Nyerere alitaka kujenga nini na kikubwa zaidi ni mahuni ambao wametaka kurithi pato la utajiri badala ya rasilimali zilizopo. NI makosa haya haya yalifanywa na Mwinyi Mkapa na leo hii JK kwa sababu hawa wote wameshindwa kuendeleza mirathi walioachiwa..

Labda nirudie tena ktk lugha mnayoifahamu nikifananisha nchi yetu na Kariakoo.
1. Nyerere alitaka kujenga nyumba ya vyumba sita kama makazi bora kwa familia yake kama walivyofanya wazee wetu. Ni makosa makubwa kufikiria vinginevyo kwa sababu kila hatua ya ujenzi wa Taifa letu wakati wa Nyerere ilikuwa ktk fikra za kujenga makazi bora kwa wananchi wake na tutahesabu tu mafanikio ya ujenzi ule kulingana na masterplan yake. Sawa na kupima mafanikio ya wazee wetu waliojenga Kariakoo na nyumba za kifamilia kwamba walifanya makosa makubwa kujenga vibada vya vyumba sita badala ya kujenga maghorofa wakati huna sababu zaidi ya kutazama magofu yale ukilinganisha na nyumba zinazojengwa kisasa bila kutazama uwezo wa mzee wako kifedha wakati ule..

2. Alipongia Mwinyi, ambaye badala ya kujenga ghorofa aliakodisha hiyo nyumba ya vyumba sita na kila mtu ktk familia alipokea pato la kodisho kupitia njia tofauti. Kila mtu alikuwa na fedha mfukoni lakini pasipo kuangalia kwamba kulihitajika ukarabati wa jengo na vifaa vyake..Matokeo yake viwanda vyote vilikufa kabisa na mashirika kufa kwa sababu hapakuwepo na mfumo bora wa kuendeleza jengo zaidi ya kupokea kodi za wapangaji kama kizazi changu waliachiwa urithi wa nyumba za Kariakoo..Katika kipindi cha Mwinyi Nyumba zote za Kariakoo zilikuwa maghofu matupu yasiyotazamika kwa macho lakini kulikuwa na siri kubwa ya thamanai ya eneo hilo kibiashara..Kwa uhalisia ndivyo ilivyokuwa Kariakoo wakati wa Mwinyi.


3. Ujio wa Mkapa ulikuja na mpango wa kuboresha pato hivyo badala ya kupangisha ilikuwa kuuza nyumba hizo kuanzisha mfumo wa kodi ili kuboresha zaidi mfuko wa Taifa kwa sababu nyumba zenyewe zilibakia maghofu. Kosa kubwa la Mkapa ni kutoelewa thamani ya Viwanja Vile na sii kutazama nyumba hizo. Aidha alijua na kufanya aloyafanya kwa makusudi kabisa akijua thamani yake au alikurupuka na ushauri wa vijana wa mtaani madalali wakubwa kina IMF ambao walitazama zaidi ile commission yao ktk mauzo hayo kuliko thaminisho la hilo jengo..

Wakati nyumba za Kariakoo zimefikia hadi millioni 800, Mkapa alikuwa akiuza nyumba za serikali tena Obay. Masaki na Mikocheni kwa millioni moja hadi mbili..Akiuza viwanda kwa thamani ya chini kwa asilimia 500 hadi 1,000, akiuza madini yetu ktk mikataba ya chini isiyotazama hali halisi na thamani ya vitu hivyo kwa sababu tu aliambiwa havina thamani tena. Haya ndio makosa makubwa ya Mkapa na yalimetugharimu zaidi kama wale vijana wa Kariako wakiorithi nyumba wakaziuza kwa bei ya chini, wasiwe na idea ya kibiashara inayoweza kuzalisha fedha hizo, wasijue wataishi wapi, na mwisho wa siku wamejikuta kwamba wameporwa ardhi yao ya urithi kwa kuhadaiwa na madalali uchwara lakini wameshindwa kutazama ujinga wao wenyewe ila kulaumu Makinga na Wapemba waliouziwa ardhi hizo..Kwa uhalisia wa hali hi ndio mpito wa Utawala wa Mkapa yaani tumeuza nchi yetu na sasa hivi sisi wenyewe hatuna makazi tunaanza kupanga ndani ya ardhi tuloachiwa kama urithi na UHURU wa Mtanzania..

4. Ujio wa JK ameyakuta mabaya yote haya yameisha tokea. Hajui pa kuanzia maana nyumba zimekwisha uzwa na hakuna jinsi isipokuwa kuanzisha makao mapya - Bagamoyo!. Labda hii ndio vision yake!
Tatizo linakuja kwamba tumekwisha poteza urithi wote na sii rahisi hata kidogo kuanzisha miradi mipya ikiwa hatuna kitu mkononi. Na nashindwa kabisa kuyaweka makosa ya Kikwete ktk chungu kimoja, zaidi ya Udhaifu wake kiutawala kuendeleza yale ya Mkapa wakati akijua fika kwamba tunazidi kuuza ardhi yetu kipande kwa kipande kama wazee waliobakia Kariakoo na baadhi ya vibanda vya hapa na pale. Udhaifu wa kutoona kwamba hata huko Kariakoo sasa hivi biashara imebadilika kabisa, Ukitaka kununua nyumba aidha utajenga ghorofa ambalo mwenye kiwanja (nyumba) atamiliki na 1/3 ya jengo linalojengwa au mwekezaji atamiliki kwa miaka 10 ya mwanzo akimlipa (akimhudumia) mwenye nyumba fedha za kuishi, ikisha miaka hiyo jengo litarudi ktk miliki ya mwenye kiwanja...

Hivyo nategemea zaidi kuona kwamba Pengine JK atakuja na mpango huu ktk vitu vichache tulobakia navyo, lakini sidhani kama naweza kumlaumu sana kwa kutochukua hatua kali dhidi ya mashirika ambayo tayari yamekwisha ingia mikataba mikubwa ya kununua ardhi na mali chini ya utawala wa Mwinyi na Mkapa isipokuwa JK kashindwa kubuni mbinu mpya za kuhifadhi kidogo tulichonacho ili kipate kuongeza pato na taifa na pengine kuboresha maisha ya wananchi...Tanzania is still under sale na inatisha sana kiasi kwamba wapo watu leo hii Kariakoo wanafikiria mbinu za kurudisha au kudai zaidi ongezeko la pato toka nyumba zao walizouza kwa bei ya chini..Lakini ukweli utabakia kwamba sheria itawabana kama ilivyotubana leo kutokana na mikataba ya Mkapa na mashirika ya nje.

Mwisho wa yote ni kwamba, tumefikia miaka 50 ya Uhuru wetu na karibu asilimia 75 ya Uhuru huo tumekwisha uuza kwa kutofahamu thamani ya ardhi yetu kama vile vijana wa Kariakoo walivyoshindwa kufahamu kwamba kinachouzwa ni kiwanja na sii ghofu waloachiwa urithi. Hivyo hivyo thamani ya kitu ktk dunia hii ya biasdhara na Uchumi - Location comes first before anything thing! na kama tutaendelea kushindwa kutambua umuhimu wa Tanzania kibiashara kutokana na location tulokuwa, na tukashindwa kutumia fursa zinazoweza kupatikana kutokana na location tuliyopo basi UHURU wetu hautakuwa na maana tena kwa sababu tutaendelea kuuza ardhi yetu kwa wageni bila kufahamu kwamba hata hao Marekani waliobobea ktk Ubepari hawajawahi kuuza wala hawauzi nchi yao kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wameuza UHURU wao.

Aslm Aleikum!
 
Kila mtu na abebe mzigo wake ni upuuzi mtupu kutaka kuwasafisha mafisadi wa sasa kwa hoja kuwa NYERERE aliiacha nchi hoi bin taaban kwa hili sikubaliani nalo, Nyerere alikemea ufisadi waziwazi leo hii viongozi wanawapigia magoti mafisadi, wapi na wapi?
 
Zote ni tishio. Vizuri tu anaonesha ni jinsi gani anayoijua kuitumia hiyo bunduki. Kwa hiyo usimfanyie utani, atakuua saa yoyote kwa sababu anajua anachofanya.

Dhidi yako-Anakuambia kabisa hii bunduki ipo tayari kutumika kwa ajili yako.

Kwa hiyo zote ni tishio.

Vizuri sana; hapa nimepata wanafunzi wanzuri.

Mtu akisema:

"Nina sifa zote kwa mujibu wa sheria zetu kuwa mwanasheria" ana maana gani?
 
Kumbuka hata kama hakuiba hata cent moja, lakini kawafilisi WTZ kwa sababu ya sera zake za Ujamaa.
Hii quote kutoka ktk well said article ambayo inazungumzia pia kuhusu Ujamaa wa Nyerere na Udictator wake.

Three of these factors are pertinent to this discourse. Firstis the argument that the initiative to start Ujamaa villages did not comefrom rural peasants. The scheme failed to gain the necessary ideologicalacceptance among the vast majority of the peasantry. Right from the beginning,the dominant attitudes of the people ranged from skepticism and mistrustto outright resentment and opposition (Lofchie, 1978: 452). Secondly,the use of coercion to ensure mass villagization - from threats of forcedtransportation to short prison sentences under the pretext of tax arrears -militated against the effective operation of Ujamaa villages. Finally, theefforts at building Ujamaa villages were greatly constrained by bureaucratswho held out government aid as incentives to peasants to move into villages.Peasants began to perceive such "free goods" as substitutes for availablelabor resources rather than being complimentary factors for increasedproduction. Promises of official assistance resulted in an over-dependenceof the villages on government initiatives and incentives that left villagesextremely vulnerable when government assistance eventually stopped.However, perhaps the single most adverse limitation of the Ujamaa villagizationprogram was the practice which Shivji (1974) and Raikes (1975)have described as "Kulak Ujamaa". This was a practice in which a numberof rich peasants, having attained positions in Ujamaa village committees orforged links with local bureaucrats, began to use the villages to further theirown interests.



Kwa hiyo ukisoma hiyo article vizuri utagundua haya matatizo yote yalianzia wakati wa Nyerere.
Ndugu Shamu, badala ya ku-copy maandiko ya watu wengine, naomba mawazo yako kama kweli ulikuwepo wakati wa utawala wa Nyerere na ulishuhudia hatua alizochukua ikiwa ni pamoja na kuwapanga watu katika vijiji. Haya maandiko ya wanazuoni wakati mwingine huwa yana lengo la ku-highlight hoja na kuchokonoa discussion, au ku-give out their opinions, au kufanya constructive critisism, au vyovyote vile... Je wewe una mtizamo gani? Toa mawazo mawazo yako yaliyo mbadala badala ya kuruhusu watu wengine wakusemee kana kwamba wewe huwezi kufikiri na kupembua ukweli wa matukio ya nchi yako.

Hebu fikiri kama wewe ungepewa kuongoza serikali ya kwanza ya Tz huru, watu ni masikini, hawana elimu, wametoka kwenye ukoloni, hakuna shule, hospital, hakuna umeme, maji, na huduma zingine muhimu... utafanyeje? Assume wewe ndiye Nyerere, ungefanyeje? Possibilities ninazoziona ni
(1) Kwa sababu watu hawa ni wajinga, hawajuwi kitu chochote, na nchi ni kubwa na ina mali nyingi, nitajikusanyia mali niwe tajiri, mimi na ukoo wangu, au kabila langu lote.
(2) Nchi hii ni nchi ya watu wangu, nitaanza kwa kuijenga nchi yangu na kuwatumikia watu wangu wote bila kuwabagua.

Possibilities hizo mbili ni kipimo cha uwezo wa kiongozi yeyote kujikana nafsi. Ukifanya kosa katika kufanya uamuzi au uchaguzi katika senario hizo mbili matokeo yake huwa ni vita ambavyo tumeziona sehemu zingine au matabaka ya watu masikini sana wa kutupwa na wenye mali mf hapo kwa jirani zetu. Nyerere alitumia vizuri sana uwezo wake wa kufikiri na kufikia uamuzi wake huo wa kujenga taifa la kijamaa na kujitegemea. Aliyaunganisha makabila yoete 123 na dini zote bila ubaguzi. Ndio maana amezidi kuheshimika hata akiwa marehem.

Mwisho, Nyerere alikuwa ameanzisha na kuijenga nchi katika misingi mizuri na bora, na kama wafuasi wake wangeendeleza uadilifu na kufanyia marekebisho baadhi ya sera au mfumo, hatimae nchi yetu ingefikia kiwango cha ustawi wa kama South Africa kwa Africa au China kwa nchi za Asia. Kumbe tatizo limekuwa hao waliopokea kijiti. Na kama tusingepata Nyerere kama rais wa kwanza mwenye mtizamo wa kizalendo na maadili, huenda Tanzania, ama Tanganyika isingekuwa nchi moja leo hii....
 
- Tatizo ni kwamba ni vigumu kumkosoa Mwalimu, kwa sababu unahitaji kulinganisha na awamu zilizofuata na hapo ndipo inapokuwa no discussion at all zaidi tu ya majungu!

Es!
 
Despite initial enthusiasm and early successes
Whaat!? initial successes? which one? could somebody name even a single initial initial success? How long were the initial successes? Hawajibu wala kujaribu kujibu.

, the Ujamaa villagizationscheme soon ran into difficulties, as people became increasingly reluctant tojoin Ujamaa villages. This, coupled with the rising cost of providing materialincentives for the villages
,

msomi mzuri anatakiwa kujiuliza kwanini vitu vilikuwa na gharama kubwa ya kuwapatia wananchi material incentives? Well, mtu yeyote anayejua historia yetu anajua world recession ya 1970s na kile kinachoitwa "Oil Shock" ya wakati huo. Je yaweza kuelezea ugumu huo ambao mwandishi anauonesha? OF COURSE NOT- Wakosoaji wa Nyerere watasema; He was Nyerere, he should have been able to do everything as planned regardless of the unforeseen economic situation. Wao ndio wanamfanya mungu fulani.



engendered a move towards forceful methods of persuading people into collective villages - a method that the regime had earlier condemned and resolved not to employ.
Mwandishi anatudokeza kitu ambacho wakosoaji wa Nyerere hawataki hata kutafuta ukweli wake; serikali haikuwa na sera ya kuhamisha na ilishasema haitatumia nguvu kuwahamisha wananchi (siku chache zijazo tutatoa nyaraka za Ujamaa Vijijini- theory na matokeo yake). Swali ambalo linahitaji ni kwanini kuna maeneo nguvu zilitumika kuwahamisha watu? na je ilikuwa makosa kutumia nguvu? Jibu liko hapa chini limepenyezwa kiujanja.

1970 for instance, saw thestart of "Operation Rufiji" whose idea was to move "by coercion if necessary",the whole population of the lower Rufiji floodplain into Ujamaa villageson higher ground not so near the river.

Kwa mtu anayeishi Marekani au nchi ambazo huwa zinapata mafuriko anajua kabisa kuwa hata leo hii serikali kama ya Marekani inaweza kukuhamisha kwa nguvu kutoka kwenye nyumba yako kama kuna tishio la mafuriko au janga kubwa. Kuna kitu kinaitwa "voluntary evacuation" na kama hatari iko imminent basi kuna kitu kinaitwa "forced evacuation".

Serikali zote duniani zina uwezo huu. Kwenye mstari hapo juu tunadokezwa Operesheni Rufiji - ilikuwa na lengo la kuwahamisha watu kutoka maeneo ya kando ya mto ili kuepusha maafa. Mwanzoni ilikuwa ni kwa kihiari lakini mwaka baada ya mwaka eneo la Rufiji lilikuwa linakumbwa na mafuriko. Lipi la kufanya? Kuendelea kutoa misaada ya kusaidia mafuriko au kuwapatia watu maeneo salama kuweza kuishi mbali na mto Rufiji? Je Serikali ingeweza kuwahakikishia usalama wananchi wake kando ya mto Rufiji wakati wa mafuriko na ilikuwa na resources za kurudia zoezi hili kilia mwaka - search and rescue, search and evacuation, or search and recovery? Uongozi ukasema "no we can't".
Kitabu cha
"Tanzania: the limits to development from above, cha Kjell J. Havnevik, kinasema hivi kuhusu suala hili na kukubaliana na ukweli wa kihistoria:

rufijioperation.png

Utaona anasema kitu ambacho mwanahistoria yeyote anaweza kukiona kuwa kuhamisha baadhi ya wananchi kwenye maeneo fulani nchini haikuwa tu kwa ajili ya kutekeleza "Ujamaa Vijijini" bali pia ilikuwa kwa ajili ya kujilinda na majanga ya asili ya ulimwengu ambayo taifa changa lisingeweza kuyamudu.
[h=1]
There was also "OperationDodoma" conceived to solve the problem of the Dodoma region by movingall the people in the region into planned villages (Coulson, 1975: 55). In1972, more "operations" were launched in Chuya and Kigoma. In the event,many of these operations turned out to be failures since local peasants, suspiciousof official motives and fearing the nationalization of their land,refused to cooperate. By late 1973, after many of these operations - the militaryanalogy being quite apt
[/h]
Kwa hiyo utaona kuwa kuwa kusoma historia with bias tayari inakuletea matatizo kwa sababu itabidi usizingatie ushahidi mwingine wowote ili ule uliopo ufit nadharia yako. Hicho kinaitwa "historical revisionism" au "kuandika upya historia". Natoa ushauri watu wakitafute hicho kitabu hapo juu kwa sababu kina mengi ya kusema na ushahidi mbalimbali wa nini hasa kilitokea. Ndio maana sisi wengine tunaomsoma Nyerere, tunawasoma kina Mohammed Said, Njozi na wengine ili kupata a clear more balanced picture. Usomi siyo tu kuuliza maswali bali pia namna ya kutafuta majibu.
 
- Tatizo ni kwamba ni vigumu kumkosoa Mwalimu, kwa sababu unahitaji kulinganisha na awamu zilizofuata na hapo ndipo inapokuwa no discussion at all zaidi tu ya majungu!

Es!
Hii nimeikopi kutoka kwenye post yako moja

- Unaweza kuwa Mwalimu wa University majuu na bado ukawa mbumbu, ukahindwa kujua kwamba Rais wa kwanza wa taifa akiwa mjinga na taifa litakwua la wajinga milele, na kwamba akiwa na akili taifa litakua vile vile, matatizo yako ni kwamba huelewi kwamba zile enzi zenu watu Musoma kututisha tisha wengine ziliisha!

- Na kiongozi kugombea na kivuli ziiilisha pia
 
Ndugu Shamu, badala ya ku-copy maandiko ya watu wengine, naomba mawazo yako kama kweli ulikuwepo wakati wa utawala wa Nyerere na ulishuhudia hatua alizochukua ikiwa ni pamoja na kuwapanga watu katika vijiji. Haya maandiko ya wanazuoni wakati mwingine huwa yana lengo la ku-highlight hoja na kuchokonoa discussion, au ku-give out their opinions, au kufanya constructive critisism, au vyovyote vile... Je wewe una mtizamo gani? Toa mawazo mawazo yako yaliyo mbadala badala ya kuruhusu watu wengine wakusemee kana kwamba wewe huwezi kufikiri na kupembua ukweli wa matukio ya nchi yako.

Hebu fikiri kama wewe ungepewa kuongoza serikali ya kwanza ya Tz huru, watu ni masikini, hawana elimu, wametoka kwenye ukoloni, hakuna shule, hospital, hakuna umeme, maji, na huduma zingine muhimu... utafanyeje? Assume wewe ndiye Nyerere, ungefanyeje? Possibilities ninazoziona ni
(1) Kwa sababu watu hawa ni wajinga, hawajuwi kitu chochote, na nchi ni kubwa na ina mali nyingi, nitajikusanyia mali niwe tajiri, mimi na ukoo wangu, au kabila langu lote.
(2) Nchi hii ni nchi ya watu wangu, nitaanza kwa kuijenga nchi yangu na kuwatumikia watu wangu wote bila kuwabagua.

Possibilities hizo mbili ni kipimo cha uwezo wa kiongozi yeyote kujikana nafsi. Ukifanya kosa katika kufanya uamuzi au uchaguzi katika senario hizo mbili matokeo yake huwa ni vita ambavyo tumeziona sehemu zingine au matabaka ya watu masikini sana wa kutupwa na wenye mali mf hapo kwa jirani zetu. Nyerere alitumia vizuri sana uwezo wake wa kufikiri na kufikia uamuzi wake huo wa kujenga taifa la kijamaa na kujitegemea. Aliyaunganisha makabila yoete 123 na dini zote bila ubaguzi. Ndio maana amezidi kuheshimika hata akiwa marehem.

Mwisho, Nyerere alikuwa ameanzisha na kuijenga nchi katika misingi mizuri na bora, na kama wafuasi wake wangeendeleza uadilifu na kufanyia marekebisho baadhi ya sera au mfumo, hatimae nchi yetu ingefikia kiwango cha ustawi wa kama South Africa kwa Africa au China kwa nchi za Asia. Kumbe tatizo limekuwa hao waliopokea kijiti. Na kama tusingepata Nyerere kama rais wa kwanza mwenye mtizamo wa kizalendo na maadili, huenda Tanzania, ama Tanganyika isingekuwa nchi moja leo hii....


Mwanzo mlikuwa hamtaki personal experience au hali halisi ya maisha kuwa ushahidi. Tumeleta ushahidi wa video bado mnapinga, mnataka documents yenye credible source. Tumeleta ushahidi mnaotaka, Article hiyo ni ushahidi wa credible source. Sasa hivi unataka maoni yangu? Ok utayapata.
 
Ndugu Shamu, badala ya ku-copy maandiko ya watu wengine, naomba mawazo yako kama kweli ulikuwepo wakati wa utawala wa Nyerere na ulishuhudia hatua alizochukua ikiwa ni pamoja na kuwapanga watu katika vijiji. Haya maandiko ya wanazuoni wakati mwingine huwa yana lengo la ku-highlight hoja na kuchokonoa discussion, au ku-give out their opinions, au kufanya constructive critisism, au vyovyote vile... Je wewe una mtizamo gani? Toa mawazo mawazo yako yaliyo mbadala badala ya kuruhusu watu wengine wakusemee kana kwamba wewe huwezi kufikiri na kupembua ukweli wa matukio ya nchi yako.

Hebu fikiri kama wewe ungepewa kuongoza serikali ya kwanza ya Tz huru, watu ni masikini, hawana elimu, wametoka kwenye ukoloni, hakuna shule, hospital, hakuna umeme, maji, na huduma zingine muhimu... utafanyeje? Assume wewe ndiye Nyerere, ungefanyeje? Possibilities ninazoziona ni
(1) Kwa sababu watu hawa ni wajinga, hawajuwi kitu chochote, na nchi ni kubwa na ina mali nyingi, nitajikusanyia mali niwe tajiri, mimi na ukoo wangu, au kabila langu lote.
(2) Nchi hii ni nchi ya watu wangu, nitaanza kwa kuijenga nchi yangu na kuwatumikia watu wangu wote bila kuwabagua.

Possibilities hizo mbili ni kipimo cha uwezo wa kiongozi yeyote kujikana nafsi. Ukifanya kosa katika kufanya uamuzi au uchaguzi katika senario hizo mbili matokeo yake huwa ni vita ambavyo tumeziona sehemu zingine au matabaka ya watu masikini sana wa kutupwa na wenye mali mf hapo kwa jirani zetu. Nyerere alitumia vizuri sana uwezo wake wa kufikiri na kufikia uamuzi wake huo wa kujenga taifa la kijamaa na kujitegemea. Aliyaunganisha makabila yoete 123 na dini zote bila ubaguzi. Ndio maana amezidi kuheshimika hata akiwa marehem.

Mwisho, Nyerere alikuwa ameanzisha na kuijenga nchi katika misingi mizuri na bora, na kama wafuasi wake wangeendeleza uadilifu na kufanyia marekebisho baadhi ya sera au mfumo, hatimae nchi yetu ingefikia kiwango cha ustawi wa kama South Africa kwa Africa au China kwa nchi za Asia. Kumbe tatizo limekuwa hao waliopokea kijiti. Na kama tusingepata Nyerere kama rais wa kwanza mwenye mtizamo wa kizalendo na maadili, huenda Tanzania, ama Tanganyika isingekuwa nchi moja leo hii....


Kwanza inabidi uclarify hiyo statement. Kwanza, WTZ hawakuwa hawajinga wakati Nyerere anachukua nchi. Pili siyo kweli kwamba WTZ hawajui chochote.
WTZ walikuwepo na waliweza kuishi kabla ya Nyerere kuzaliwa. Nenda ktk sehemu zenye historia ili uweze kuona WTZ walivyokuwa wanaishi kabla ya Dictator kuzaliwa. Unapozungumzia walikuwa wajinga unamaanisha nini?
Hawajui chochote? Walikuwa wanaishi vipi? C'mon, Let's be honest.
 
Vizuri sana; hapa nimepata wanafunzi wanzuri.

Mtu akisema:

"Nina sifa zote kwa mujibu wa sheria zetu kuwa mwanasheria" ana maana gani?

Nitatumia sifa as qualifications. Inategemeana anazungumza na nani. Kwanza, kama anazungumza kukuelezea kuhusu maisha yake anamaanisha kwamba yupo kwenye process ya kuwa mwanasheria kamili kisheria.
Pili- Kama umeenda kupata advice au kuongea naye na anakufahamisha jambo linalohosu sheria, unaweza kutumia mawazo yake as credible source.
 
Whaat!? initial successes? which one? could somebody name even a single initial initial success? How long were the initial successes? Hawajibu wala kujaribu kujibu.

,

msomi mzuri anatakiwa kujiuliza kwanini vitu vilikuwa na gharama kubwa ya kuwapatia wananchi material incentives? Well, mtu yeyote anayejua historia yetu anajua world recession ya 1970s na kile kinachoitwa "Oil Shock" ya wakati huo. Je yaweza kuelezea ugumu huo ambao mwandishi anauonesha? OF COURSE NOT- Wakosoaji wa Nyerere watasema; He was Nyerere, he should have been able to do everything as planned regardless of the unforeseen economic situation. Wao ndio wanamfanya mungu fulani. Mwandishi anatudokeza kitu ambacho wakosoaji wa Nyerere hawataki hata kutafuta ukweli wake; serikali haikuwa na sera ya kuhamisha na ilishasema haitatumia nguvu kuwahamisha wananchi (siku chache zijazo tutatoa nyaraka za Ujamaa Vijijini- theory na matokeo yake). Swali ambalo linahitaji ni kwanini kuna maeneo nguvu zilitumika kuwahamisha watu? na je ilikuwa makosa kutumia nguvu? Jibu liko hapa chini limepenyezwa kiujanja. Kwa mtu anayeishi Marekani au nchi ambazo huwa zinapata mafuriko anajua kabisa kuwa hata leo hii serikali kama ya Marekani inaweza kukuhamisha kwa nguvu kutoka kwenye nyumba yako kama kuna tishio la mafuriko au janga kubwa. Kuna kitu kinaitwa "voluntary evacuation" na kama hatari iko imminent basi kuna kitu kinaitwa "forced evacuation".

Serikali zote duniani zina uwezo huu. Kwenye mstari hapo juu tunadokezwa Operesheni Rufiji - ilikuwa na lengo la kuwahamisha watu kutoka maeneo ya kando ya mto ili kuepusha maafa. Mwanzoni ilikuwa ni kwa kihiari lakini mwaka baada ya mwaka eneo la Rufiji lilikuwa linakumbwa na mafuriko. Lipi la kufanya? Kuendelea kutoa misaada ya kusaidia mafuriko au kuwapatia watu maeneo salama kuweza kuishi mbali na mto Rufiji? Je Serikali ingeweza kuwahakikishia usalama wananchi wake kando ya mto Rufiji wakati wa mafuriko na ilikuwa na resources za kurudia zoezi hili kilia mwaka - search and rescue, search and evacuation, or search and recovery? Uongozi ukasema "no we can't".
Kitabu cha
"Tanzania: the limits to development from above, cha Kjell J. Havnevik, kinasema hivi kuhusu suala hili na kukubaliana na ukweli wa kihistoria:

View attachment 33099

Utaona anasema kitu ambacho mwanahistoria yeyote anaweza kukiona kuwa kuhamisha baadhi ya wananchi kwenye maeneo fulani nchini haikuwa tu kwa ajili ya kutekeleza "Ujamaa Vijijini" bali pia ilikuwa kwa ajili ya kujilinda na majanga ya asili ya ulimwengu ambayo taifa changa lisingeweza kuyamudu.
[h=1][/h]
Kwa hiyo utaona kuwa kuwa kusoma historia with bias tayari inakuletea matatizo kwa sababu itabidi usizingatie ushahidi mwingine wowote ili ule uliopo ufit nadharia yako. Hicho kinaitwa "historical revisionism" au "kuandika upya historia". Natoa ushauri watu wakitafute hicho kitabu hapo juu kwa sababu kina mengi ya kusema na ushahidi mbalimbali wa nini hasa kilitokea. Ndio maana sisi wengine tunaomsoma Nyerere, tunawasoma kina Mohammed Said, Njozi na wengine ili kupata a clear more balanced picture. Usomi siyo tu kuuliza maswali bali pia namna ya kutafuta majibu.

Je kama reality also inachangia kusupport unachobelieve, inabidi bado utafute sources ambazo zinamsifia Nyerere?
 
where are you my dear? engineer is a sign of responsibility nothing else, bungeni iliishajadiliwa, mtu hawezi kusimamisha gorofa 100 inayobeba roho maelfu na asiitwe kwa titile yake..ni title ya responsibility na unatakiwa uitwe kisheria, kama haujasajiliwa na serikali ni illegal kujiita engineer so and so!!! na ni kosa kutojiita!!!1 ni sheria, najua utasema imeandikwa wapi, fuatilia sasa baada ya kukupa huu mwanga, siyo ujiko ni responsibility---kwa maana ya liability!
mmh acha zako bwana,viongoz wangapi ni walimu cjasikia wakitumia title ya mwl. Au ualimu sio tittle? then kutumia title eng cyo lazima bana labda kwa wapenda ujiko.
 
Kuna wale waliopinga hoja zake, na walitishiwa na Nyerere mwenyewe.
Hii video clip ni ushahidi tosha.
Films On Demand - View Playlist#

Kuna jambo linamsumbua Shamu.
Anasoma article nyingi sana katika internet, jambo zuri sana. Anavideo clip zinazoelezea madhila ya ujamaa, jambo jema kabisa.
Asichokijua ni kitu kinaitwa 'school of thought' yaani kuna vyuo duniani haya mambo wanayajadili kila uchao, tofauti na Shamu wanaangalia mambo kwa mtazamo mpana bila hisia wala chuki.

Nilishawahi kuona mwalimu wa University ameandika thesis yake marekani kuhusu viongozi wa Afrika akam cite Nyerere na Nkrumah kama mifano.
Alifaulu vema tu, si kwasababu nyingine bali aliweza kueteta hoja zake kwa mantiki.

Shamu, kuna article maelfu zinaelezea Nyerere kwa ujumla wake, nenda China, yaani ujamaa wa Nyerere unaonekana kama role model.
Hizo article unazosoma zimeandikwa na watu kama wewe na hazikiji haja ya kuwa proof kama hazikuwa authenticated na documented.
Video clip uliyoweka ni sawa na prof Jay akiweka video yake ya 'maisha magumu' basi wewe ukaichukulia kama proof ya maisha magumu TZ.

Nina uhakika zipo document nyingi sana kuhusu mwalimu lakini umeamua kuchukua zile zinazokidhi haja ya ushindani wako, ni jambo zuri. Ubaya ni pale unapozibandika na huna mifano unayoijua wewe ya kweli kuthibitisha hayo.
Matokeo yake unasema vijiji vya ujamaa wamekufa watu wengi, swali ni kuwa wengi ni wangapi, je 10 si wengi, 1000 si wengi.

Umeshindwa kutetea neno dictator kama definition yake unabaki kusema alitisha watu. Mkapa aliposema tutawashughulikia wapinzani alikuwa dikteta? Kikwete aliposema serikali imeishiwa na uvumilivu na wapinzani naye dikteta. Kama tutaichukulia kauli yako basi hakuna kiongozi atakayekuwa salama. Obama amesema earmark ikutua mezani kwake ata veto, naye ni dikteta.

Wanaomtetea Nyerere hawatumii majarida, wanakuambia hivi: Nyerere aliacha viwanda Mwatex, Tanganyika packers, Mutex, Urafiki, UFI n.k na waweza kukupa kiwanja namba. Wanasema kaacha hospitali ABC na wanakupa kiwanja zilipo. Wanasema kaacha viwanja vya ndege KIA, JNIA n.k. Watakwambia kaacha shule za kata na si wazo la Lowasa watakupa nyaraka zake mwenyewe (sio video za watu) na shule zilipo na fedha zilizotumika kujenga.
Watakuambia ameacha Mtera na ukitaka watakuletea samaki wa kutoka katika bwawa hilo.
Ninachotaka kusema ni kuwa usitoe nadharia za masimulizi, toa ushahidi kama huo. Hiyo video clip inaweza kutengenezwa na P.funky akaonyesha uzuri wa Nyerere, sijui utaiamini au unataka yenye lafudhi ya kizungu.

Jaribu ku connect unachokijua na reality. Usijadili mada ukiongozwa na chuki na bias, inaondoa thamani ya kitu kinaitwa intellectual.
Hivi hushangai kuna waganda wanamsifia Idd Amin leo na Wazimbabwe wanamsifia Mugabe!! Na kuna wamerekani wanamchukia JF.
Hivi documentary unaweza kuitumia kama ushahidi hata katika mahakama ya mwanzo!!!!!!
 
Nyerere alikuwa "dikteta" ndiyo. Swali ni vigezo vya nani? Maana ukweli ni kwamba asilimia 99 ya mababa na mamama waliyo viongozi (hata wale wa kifamilia) katika jamii ya Tanzania leo hii wana-qualify kuitwa "madikteta" kwa vigezo vya Wazungu. Machifu wa Kiafrika walikuwa madikteta. Na Wafalme na Ma-Emir kwenye nchi za Kimanga na Kiislamu kama Saudi Arabia, Oman, Kuwait, Brunei etc nao wote ni madikteta. JK ni dikteta pia, tena dikteta mkubwa sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom