Siku za hivi karibuni kumekuwa na kundi kubwa la watu waliojipambanua kuwa wao ni wakosoaji wa Nyerere na hata baadhi yao wamethubutu kumwita dikteta ingawaje kwa miaka mingi Nyerere amekuwa akiheshimiwa sana miongoni mwa wananchi wa kawaida wa Tanzania.
Mara nyingi ukosoaji huwa umekuwa ukifanywa na vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na magazeti, blogs na wakati mwingine wanasiasa na watu binafsi mpaka sasa sitakosea nikisema ukosoaji dhidi ya Nyerere umekithiri kwa siku za karibuni.
Kwa bahati mbaya mimi nimezaliwa miaka ambayo Nyerere ameshastaafu ingawaje nilifanikiwa kusoma vitabu vyake na hata kumwona. Kupitia maandiko yake sijaona jambo baya lakini bado sishawishiki kuwa alikuwa anapatia kila kitu.
Hivyo ndugu wadau naomba kufahamu juu ya Nyerere, sihitaji sifa zake tu abadani sihitaji udhaifu wake pekee bali nahitaji kumfahamu Nyerere zaidi ya yale yaliyoandikwa vitabuni, nataka kumjua kiundani ili mwisho wa siku nifahamu je wanaompinga Nyerere wana hoja za msingi au wanatafuta umaarufu ama kutoka?
NAWASILISHA