Wanandoa na extended family

Wanandoa na extended family

my house.... My rules.......

Muishi na ndugu mwenye uhitaji haswa na awe na shughuli ya kufanya. Ukiishi na ndugu ambaye yupo yupo tu mtaishia kugombana.

Akifika mkae na mumeo mumpe abc utaratibu wa nyumba yenu hawezi mwambieni wazi milango iko wazi

kama ana ugonjwa unaohitaji attention au masharti fulani aseme siku ya kwanza kabisa msije kwazana mbeleni

unajua ndugu zako mwanamke ni rahisi kuwakemea na kuwapiga biti sasa ndugu wa mwenzio wanaweza wakuone una roho mbaya

pia mke jifunze kuchukulia easy baadhi ya vitu na kumbuka hao ni wapitaji tu

mwisho watendee vile wewe ungependa kutendewa



word !
 
Hahahahah, hivi unajua kuwa ukiwaeleza ndugu kwamba huna hawakuamini?

Ushauri wangu ni kwamba wanandoa wakubaliane jinsi ya kusaidia ndugu wa pande zote. Sisi baada ya majaribio ya zaidi ya miaka 20, tumeshaamua kutoka hi na mtu zaidi ya mfanyakazi. Na huko mbele ya safari tunaweza kuishi peke yetu pale watoto wakishapata makazi yao.

Inconvinience za ndugu hazivumiliki.

Hili ni kweli kabisa ndugu ukimwambia huna haamini kabisa,kwangu mimi kama sina kweli aongee tu awezavyo na wala sitachukia kwa maneno yake.

Mimi naomba unisaidie hapa,mfano wewe babu DC baba yako anaumwa huko kijijini aliko,wewe wakaa DSM,ukaamua baba yako aje DSM ili umsaidie matibabu na bila hiyana lazima akae kwako,na umekuja kugundua matibabu yake yanachukua muda sana,na umejitahidi kufanya kila liwezekanalo mgonjwa akae sawa,siku 2 mzima siku 2 mgonjwa , na tabia ya baba yako kiasili ni mtata,kiasi fulani kwa miezi kadhaa aliyokaa kwako ni kero kwa mkeo. Utafanyaje juu ya hili swala?
 
Mtambuzi nimekusoma kaka na michango mingine

Wengi kama unavosema tumesaidiwa na ndugu kufikia hapa tulipo

Lakini pia hatukuendelea kukaa kwao pale tulipojiweza

Tatizo apa ninkwamba kuna ndugu wanakuja hawana plan na ukiwapa hawaitaki maadam wanakula wanalala basi apo ndo wameweka kambi..hao ndio wanaoibua masimango..kabila letu hatuna utamaduni wa kupiga kambi..siku mbili tatu umeondoka tena usipoangalia wazee wako kuwaomba waje kukutembelea ni mtihan maana wana majukumu pia mengi na wanaheshim privacy..watakuja kwa lets matibabu na kutimua

Kuna makabila mengine anaenda na magarage na mahindi kilo tatu na watoto 3 anakaa miezi mitatu!
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi nimekusoma kaka na michango mingine

Wengi kama unavosema tumesaidiwa na ndugu kufikia hapa tulipo

Lakini pia hatukuendelea kukaa kwao pale tulipojiweza

Tatizo apa ninkwamba kuna ndugu wanakuja hawana plan na ukiwapa hawaitaki maadam wanakula wanalala basi apo ndo wameweka kambi..hao ndio wanaoibua masimango..kabila letu hatuna utamaduni wa kupiga kambi..siku mbili tatu umeondoka tena usipoangalia wazee wako kuwaomba waje kukutembelea ni mtihan maana wana majukumu pia mengi na wanaheshim privacy..watakuja kwa lets matibabu na kutimua

Kuna makabila mengine anaenda na magarage na mahindi kilo tatu na watoto 3 anakaa miezi mitatu!

Well said,kabila gani hilo unalolisemea hawaweki kambi?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mangatara naomba unitake radhi, mwenzio mie bado anda eitin, hata harufu ya ndoa bado sijaanza kuisikia.

Nimeyaona hayo kwa marafiki zangu ndio maana nikalileta hapa ili tuhadili tatizibhuwa ni nini??

Kwa upande wangu hata mie nimelelewa kwenye extended family, tuliishi vizuri na ndugu wa kwao baba yangu na wa kwao mama yangu. Nina imani hata mie nitakuja kuishi vizuri na ndugu wa mume mtarajiwa.

Charminglady, Loh! Pole sana. Kweli tusiangalie picha au umbo la mwili kwani Pilato hataangalia umbo bali cheti cha kuzaliwa.
Kaushauri kangu kwako Charminglady, tembea na cheti cha kuzaliwa wakuda wakikuona mwili huo ulio nao hawatasita kutupia chambo unaswe.
Pia, anda eitiini unatafuta nini humu JF? Umemaliza Homuweki yako??
 
binafsi nimekulia kwenye extended family, ndugu wa pande zote mbili na watu wengine baki wasiopungua wanne, lakini wote ilikuwa sheria moja, shuleshule, kazikazi, kilizo kijijini kusaidia kulima, wote tulikuwa respect na hakuna muda wa kupiga pelepete zisizo na msingi. kwangu mimi extended family haiepukiki, kikubwa ni misingi tu, hakuna upendelleo wa ndugu wa upande wowote, wote ni sawa, na mwanamke anatakiwa ajue hilo.

Well said kama familia mnajitambua na amuishi kea maoni hakuna ndugu wa kuvuruga.
 
ugomvi wote huu ktk familia ni chakula!!! cjui kwa nn wanawake kwao chakula wanaona dili sana!!! alafu mbaya sana ndugu wa mwanamke akija kunakuaga hakuna shida ataishi na hata atasomeshwa fresh tu lakini ngoja aje ndugu wa mwanaume tabu mtindo mmoja!!!
 
Well said,kabila gani hilo unalolisemea hawaweki kambi?

Hahahaa everlenk kwanza tumepotezana pili huo mtego wa kutaja kabila huninasi ng'o maana utaniuliza na makabila/kabila linaloweka kambi
 
Last edited by a moderator:
ugomvi wote huu ktk familia ni chakula!!! cjui kwa nn wanawake kwao chakula wanaona dili sana!!! alafu mbaya sana ndugu wa mwanamke akija kunakuaga hakuna shida ataishi na hata atasomeshwa fresh tu lakini ngoja aje ndugu wa mwanaume tabu mtindo mmoja!!!


Unajua ndugu wa mwanamke ni rahisi sana kuwacontrol.......akifanya kosa ukamgombeza anakuelewa .......sasa afanye kosa ndugu wa mume halafu umgombeze lazima awapigie simu ndugu zake wote na kuanza kukunanga kwamba una roho mbaya!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kuna ukweli kuna ndugu ni visirani balaa asione kaka yake kaja na kimfuko,utasikia"anamdekeza sana mkewe,mwanamke mwenyewe sura kama kiazi kitamu sijui alikua kafumba macho"
na upande wa pili mke/mume anaweza akawa ndiye mbaya.
Changamoto ni kubwa kama kuibuka chuki na maneno ya ugomvi kati ya ndugu na mwanandoa mmojawapo.

Teh Teh dah umenichekesha! Kiukweli kuna mawifi hatari tupu yaani umkute ni mswahili anaishi kwa kaka yake afu wewe Uwe vizuri dah utajuuuuuta!!
 
Inahitaji hekima ya Mungu na busara ya hali ya juu kuishi na ndugu. Pia mentality tuliyojiwekea kuwa kuishi na ndugu ni shida inatucost pia. Kila mtu anaconcentrate kuangalia mabaya ya ndugu yake instead of kuwa positive.
Uchoyo na ubinafsi unachangia sana kuzifanya extended family zionekane ni ngumu. Kuna mtu anamchukulia ndugu aliyeenda kwake ana shida, hata kama mtu ameenda tu kusalimia. Utataka umtreat utakavyopenda eti tu kisa yupo nyumbani kwako. Mwingine atataka tu ndugu ndo wafanye kazi, huku watoto wake wakiwa wamekaa tu, kweli ni haki na unakuta watoto wake ni wakubwa kuliko huyo ndugu. Kweli tutafika kwa mtindo huu?
Haya ndugu na wewe umefika kwa watu, badala ya kuishi kama wanavyoishi uliowakuta, unataka uishi kama unavyoishi kwenu aisee. Ukienda kwa watu, fuata sheria zao, kama huziwezi basi rudi kwenu tu, usichumie watu dhambi. All in all tujifunze kuishi kwa kuvumiliana madhaifu yetu. Kama tukikosea basi tukubali kuonywa na kufundishwa pia. Hakuna mtu mkamilifu
 
Umesema;
Kwa upande mwingine kama mwanaume una kuwa sio makini Ndugu wanaweza vunja ndoa maana Kuna wengine kabisa na ni ukweli ni wakorofi na wana gubu hivyo kuishi nao ina hitaji kifua na uwe mtu wa kupuuza na hili lina washinda wana wake wengi!

Kuna baadhi ya wanawake wanafikiri wanaweza kuwatenganisha ndugu wa mume na mume wake anasahau kabla ya kuolewa hao ndugu walikuwepo na wengine wana diriki kwenda hadi kwa waganga kuhakkisha Mume ana wachukia ndugu zake!

Hivyo katika mitihani ambayo wanawake wengi wanafeli na wengine walishajitolea kufeli ni kuishi au jinsi ya kuishi na ndugu hasa wa Mume!

Mwanamke ana hitaji kifua,uvumilivu na busara kuishi na ndugu hasa wa Mume!

Ruttashobolwa;
Naomba uelewe kuwa, mwanamke aliye na uhakika na mume wake hana wasiwasi wowote ule. Mwanamme ndiye humsababisha mkewe akose udhabiti wa nyumba yake.
Fikiria, mwanaume umetoka kazini au kwenye shughuli yako, mtu wa kwanza kusema na kukaa naye sebuleni ni ndugu yako awe dada au kaka. Hujamsalimu mkeo aliye jikoni au chumbani kwa shughuli maalum, unaketi sebuleni na watu wengine, mnasogoa nusu saa nzima ndo unaanza kuita, We, ma flani, unajua nishakuja?? Mbona hujaja nisalimu. Huo ni utumwa wa kizamani saana. Usimwone mkeo ati ni roboti. Labda ndo alikuwa ameweka unga kwa maji, akiacha na kuja mbio kukupokea, kweli atakuwa amekuonesha hishima lakini ugali tayari ushakuwa mabonge. Aibu ya nani hapo?
Ingia jikoni/chumbani, mwone, mkeo akusalimu na weye usogee karibu naye mpe neno la kumtia moyo. Nenda basi sebuleni kasemezane na hao walioko huko.
Kama ni dadako, angalia sana, sikubali mke wangu awe boi wao, hapana. Sintapiga soga na dadangu wakati mke wangu yuko bize akihudumia na dada anakaa kupiga soga sebuleni. Asinieleze udhaifu aliouona kwa mke wangu. Yeye angojee aolewe au aende kwao ajichunge asiufanye udhaifu kama huo kwao ndipo atukaribishe kwao atuoneshe ufundi wake huko kwao. Tukiuona ni wa kuridhi tutauchukua, sio aje kuiongoza nyumba yangu na mke wangu. Unakuta wanaume wengi wanawaunga mkono hao wambeya ati sijui nilimpata wapi huyu mwanamke! Loh! Hapa mjinga ni nani ka si weye?
Mwanamke mwenye inda tangu kwao, utamkomesha pale pale mwanzoni kwa kumfundisha awaheshim ndugu zako ili wao pia wamheshimu. Ila wasivuke mpaka.
Nimeona kwa jamaa fulani; ati, wadogo zake wanawaleta masela home na kukaa nao juu ya kitanda cha kaka yao, wanapiga stori ati hakuna taabu tumekaa tuu juu ya kitanda. Nikija miye nawatoa nduki wala singojei mke aniambie.
Mwanamke anayefeli hapo, ni kibri chake kwa mumewe wala si sababu nyingine. Mme amsikilize mkewe na mke amsikilize mmewe. Nyumba itadumu
 
Nilikuja kujua kumbe kweli Mdigo Mzigo shemeji yangu alipokuja kuishi nasi pamoja na mke na watoto wanne.Mie Karucee lo!

Karucee; Hukopeshi?? Sio mzigo ila ni upendo wa kuzidiiiii. Usiogope, nawe funga mizigo, hamia kwa shem mkubwa. Hayo ndo maisha. Ngoja sasa, atoke, Ba mkwe na ma mkwe wanahamia. Hawajali una chumba cha pili au la.
Rafiki yangu mmoja aliletewa Ba mkwe na ma mkwe wote wanasema wanaumwa. Akawapokea, akadhani watamwonea huruma, vyumba viwili naye ana watoii wawili. Mshindo ulishuka kwani baada ya siku mbili wakaja shemeji zake 2 wa kiume na dada yao ati tunakuja kuwahudumia wazazi. Nilichokaaaa
 
Charminglady, Loh! Pole sana. Kweli tusiangalie picha au umbo la mwili kwani Pilato hataangalia umbo bali cheti cha kuzaliwa.
Kaushauri kangu kwako Charminglady, tembea na cheti cha kuzaliwa wakuda wakikuona mwili huo ulio nao hawatasita kutupia chambo unaswe.
Pia, anda eitiini unatafuta nini humu JF? Umemaliza Homuweki yako??

Nipo likizo mkuu, ndio maana unaona niko JF 24/7..
 
Back
Top Bottom