Wanandoa na extended family

Wanandoa na extended family

asikwambie mtu roho mbaya zote unazoziskia kwenye kula
mtu anaekunyima kula muogope kusoma wanasomeshwa na ndgu wengine na ye anachangia pia
binafsi kwangu mimi maneno maneno hayaniumzi na siwezi wafukuza si kwa ndgu yao hata wakijaa maana mi siwezi watesa sijui ntakufa lini
kula ndo kunagombanisha watu mi nakwambia
we fuatlia tu

hahhahaa, doh! ni muhimu kuwa namashamba pia, tena wakiwa wengi ndiyo labor yenyewe wanasaidia japosiku mbilikwa wiki!
 
Kuvumilia tu mradi una privacy ukiwa chumbani kwako...mengine fanya kama hawa exist...keep yourself busy baas...hutakaa usikie kesi wala sijuhi nani kakuteta nini...na mwisho wa siku utaheshimiwa...

Ila ukikaa kuwateta ndugu wa mumeo...tena na house girl umekaribisha vita...maana huyo atakuwa ni media ya kutoa maneno huku kupeleka kule....midomo ndio inatuponza wanawake...zip.....
 
Mada nzuri,changamoto zipo nyingi'ila cha msingi ni wwe kufanya sehemu yako,maanA lawama huwa haziishi.
 
wewe unaongelea "kwingine", tuko hapa ubantuni ongelea mazingira ya hapa. kuna uzi uliwahi kuletwa humu kwamba watu siku hizi hawana shukrani, mtu kasomeshwa na shangazi yake mjomba upande wa bi mdogo lakini toka apate ajira hata kubip ili awajulie hali hakuna, sisi ni waafrika maisha yetu ni ya kuungaunga, tuna jukumu la kuwasuuport walio nyuma yetu kwa chochote kidogo tulichonacho!

Mkuu tumejaribu kila njia ila hadi sasa nadiriki kusema kuwa biashara ya kufuga ndugu wa pande zote haina tija. Kwa babu sasa hivi anakuja mgeni tu. Wengine ni watenda kazi baasi!
 
wewe unaongelea "kwingine", tuko hapa ubantuni ongelea mazingira ya hapa. kuna uzi uliwahi kuletwa humu kwamba watu siku hizi hawana shukrani, mtu kasomeshwa na shangazi yake mjomba upande wa bi mdogo lakini toka apate ajira hata kubip ili awajulie hali hakuna, sisi ni waafrika maisha yetu ni ya kuungaunga, tuna jukumu la kuwasuuport walio nyuma yetu kwa chochote kidogo tulichonacho!
Mkuu, nimekupata lakini hatamimi nimekulia na kulelewa ktk mazingira ya aina hiyo, hudhaani kama wakati umefika tubadilikee?!
 
ni ngumu kwa wanawake wa kisasa kutokana na kutokua na uvumilivu. OVER.
 
Mkuu tumejaribu kila njia ila hadi sasa nadiriki kusema kuwa biashara ya kufuga ndugu wa pande zote haina tija. Kwa babu sasa hivi anakuja mgeni tu. Wengine ni watenda kazi baasi!

unapoongelea "kufuga" unamaanisha nini? kusomesha watoto wa nduguzo ni kufuga, au sijakuelewa vizuri?
 
Mkuu, nimekupata lakini hatamimi nimekulia na kulelewa ktk mazingira ya aina hiyo, hudhaani kama wakati umefika tubadilikee?!

ilipofika zamu yako majukumu ndiyo unataka ibadilike?!! tunatofautiana mkuu, binafsi nina majukumu mazito sana ya kuwang'oa ndugu na jamaa kwenye tope ningali hai, sina uwezo wa kuwang'oa wote lakini naamini niking'oa wawili watatu nao wakaja kutoa wawili watatu muda si mrefu wengi watakuwa vizuri, nina deni mkuu, i just cant play selfish!
 
Nilikuja kujua kumbe kweli Mdigo Mzigo shemeji yangu alipokuja kuishi nasi pamoja na mke na watoto wanne.Mie Karucee lo!
 
Charminglady;
Sikujua kuwa na weye una inda! Loh! Tabasamu loote hilo kumbe ndani moyo korosho! Weye huna hakika na aliye kuoa? Waliokuja woote wawekee full stop. Pale pale mwanzoni, hata kabla hujafua zile nguo ulizotoka nazo kwenyu. Hakikisha wanaijua mipaka yako na mumeo kwao. Uliolewa na mtu mmoja sio ukoo.
Wa kuja kwenu aje lakini akijua kakayao, kijana wao, au baba mdogo wao, kesha oa. Alimwoa Charminglady. Hajaoa kijiji. Ukiisha kuweka misimamo yako hiyo, sasa wale ambao umewakuta kwake, watoto wa kambo, wapende kwani walikutangulia. Waoneshe kuwa, unawapenda, utawaheshimu nao pia wakuheshimu.
Ukianza kuwa nyanyasa, itakula kwako. Waswahili husema; Nkune nami nkukune! Heshima ni reciprocal!
Sikuona sababu ya wewe kum attack mtoa mada wakati kauliza swali na wali hili swala haliitaji mtu kuwa amelifanya ndio alijadili maana kila mtu anajua kabisa kuna ukweli! Pengine hukumsoma vyema!

Back to topic!
Ukweli ni kwamba wanaopata shida kwenye hili ni wanawake hasa wanapo kutana na ndugu wakorofi!
Lakini mara nyingi huwa najiuliza kwanini huwa linawasumbua wanawake hili swala hata kabla ya kuingia kwenye ndoa? Na ni Ukweli ulio wazi wanawake walio wengi hawapendi kuishi na ndugu wa mume hata kama hawakuwai kuwa kosea!

Pengine ni kweli ina hitaji kifua na uvumilivu sana kuishi na ndugu na watu tuna mifano mingi unaona mwanamke wanapo kuja ndugu wa mume anachukia Lakini wa kwakwe hata wakikaa hapo mwaka hana shida!

Wanawake muda mwingine wana sahau kabisa kuwa mtu anajengwa na aina ya familia aliyo kuwa nayo! Na mara nyingi swala la kuishi na ndugu huwa haliwasumbui sana wanaume hata kama wangekuwa wa mwanamke!

Kibaya zaidi baadhi ya wanawake wanakuwa wameshajenga kabisa kichwani kuwa ndugu wa mume wana gubu ,chuki hivyo anaweka kichwani na huwezi kumbadilisha na kweli hataki kuwaona!


Kwa upande mwingine kama mwanaume una kuwa sio makini Ndugu wanaweza vunja ndoa maana Kuna wengine kabisa na ni ukweli ni wakorofi na wana gubu hivyo kuishi nao ina hitaji kifua na uwe mtu wa kupuuza na hili lina washinda wana wake wengi!

Kuna baadhi ya wanawake wanafikiri wanaweza kuwatenganisha ndugu wa mume na mume wake anasahau kabla ya kuolewa hao ndugu walikuwepo na wengine wana diriki kwenda hadi kwa waganga kuhakkisha Mume ana wachukia ndugu zake!

Hivyo katika mitihani ambayo wanawake wengi wanafeli na wengine walishajitolea kufeli ni kuishi au jinsi ya kuishi na ndugu hasa wa Mume!

Mwanamke ana hitaji kifua,uvumilivu na busara kuishi na ndugu hasa wa Mume!
 
Kuvumilia tu mradi una privacy ukiwa chumbani kwako...mengine fanya kama hawa exist...keep yourself busy baas...hutakaa usikie kesi wala sijuhi nani kakuteta nini...na mwisho wa siku utaheshimiwa...

Ila ukikaa kuwateta ndugu wa mumeo...tena na house girl umekaribisha vita...maana huyo atakuwa ni media ya kutoa maneno huku kupeleka kule....midomo ndio inatuponza wanawake...zip.....
Huu ni ukweli kabisaaaa ulonena
 
My house.... my rules.......

Muishi na ndugu mwenye uhitaji haswa na awe na shughuli ya kufanya. Ukiishi na ndugu ambaye yupo yupo tu mtaishia kugombana.

Akifika mkae na mumeo mumpe abc utaratibu wa nyumba yenu hawezi mwambieni wazi milango iko wazi

Kama ana ugonjwa unaohitaji attention au masharti fulani aseme siku ya kwanza kabisa msije kwazana mbeleni

Unajua ndugu zako mwanamke ni rahisi kuwakemea na kuwapiga biti sasa ndugu wa mwenzio wanaweza wakuone una roho mbaya

Pia mke jifunze kuchukulia easy baadhi ya vitu na kumbuka hao ni wapitaji tu

Mwisho watendee vile wewe ungependa kutendewa
 
Heeeeee

Yeye mkewe na watoto wa nne?

Kisa????????????????????????????

Kudadadeki sipati picha



Nilikuja kujua kumbe kweli Mdigo Mzigo shemeji yangu alipokuja kuishi nasi pamoja na mke na watoto wanne.Mie Karucee lo!
 
Ndugu aje ana shida maalum.

Mengine asaidiwe huko aliko

Sio anakuja kutembea hapo mbugani?

Au kaja Kupumzika kwani nyumba yako ni hoteli?

Kuna wageni wengine wapo tu hana hata mpango wa kuondoka. Sasa usiombe ukute ni jeuri utaomba poo

Mwingine anakuja halafu anataka kuleta kanuni sheria na taratibu zake. Wasichana wako wa kazi ndio wanakuwa wake na kugeuza utaratibu wa nyumba yako.

Kuna wale wanaokununia mwenye nyumba.

Wengine wale walale ... hawa hawajisogezi ni wao na tv wao na remoti hata kikombe hasogezi. Sitting room yako inageuka kuwa ni jiko/ bedroom/ library

Kuna wale ambao watakutangaza ubaya hadi mtaa wa saba......

Mwingine atakwambia hali kiporo... hali maharage sababu ameyala sana alipotoka na yeye kaja kubadili upepo. Mwendo wa nyama na samaki utafikiri amekupa hela.

Kuna wale wa kugombanisha......


Mkuu tumejaribu kila njia ila hadi sasa nadiriki kusema kuwa biashara ya kufuga ndugu wa pande zote haina tija. Kwa babu sasa hivi anakuja mgeni tu. Wengine ni watenda kazi baasi!
 
kusaidia ndugu ni muhimu sana maana ni kuikomboa familia yote kwa ujumla na haujui nani atasaidia watoto wako ukiondoka ghafla, ila kuleta ndugu wengi home nayo unatesa mkeo na kuongeza kesi zisizohitajika, weka ndugu wawili tu home ambao wanasoma au wamekuja kwa sababu maalum (sio kukaa) wengine unaweza wasaidia wakiwa huko huko waliko peleka boarding school au unatuma hela. Extended family ni muhimu sema ndio usiwajaze home kwako, kwani msaada lazima waishi na wewe?
 
Sijui kwa nini wanawake wana-make a big deal kwenye chakula, mpaka leo sielewi kwa nini mnakuwa na roho mbaya hasa kwenye chakula...!!

Wakati nasoma nilibahatika kuwa shule mji anaoishi kaka yangu, once in a while nilikuwa napenda kwenda kusalimia na kubadilisha 'ladha', kumbe shem hakupenda ile tabia , msaidizi wao akanitonya kuwa shemeji yako anaongea maneno mabaya kila ukija...kuanzia hapo, hadi leo wanajiuliza kwa nini huyu jamaa haji kwetu tena!!!
 
Charminglady;
Sikujua kuwa na weye una inda! Loh! Tabasamu loote hilo kumbe ndani moyo korosho! Weye huna hakika na aliye kuoa? Waliokuja woote wawekee full stop. Pale pale mwanzoni, hata kabla hujafua zile nguo ulizotoka nazo kwenyu. Hakikisha wanaijua mipaka yako na mumeo kwao. Uliolewa na mtu mmoja sio ukoo.
Wa kuja kwenu aje lakini akijua kakayao, kijana wao, au baba mdogo wao, kesha oa. Alimwoa Charminglady. Hajaoa kijiji. Ukiisha kuweka misimamo yako hiyo, sasa wale ambao umewakuta kwake, watoto wa kambo, wapende kwani walikutangulia. Waoneshe kuwa, unawapenda, utawaheshimu nao pia wakuheshimu.
Ukianza kuwa nyanyasa, itakula kwako. Waswahili husema; Nkune nami nkukune! Heshima ni reciprocal!

Mkuu mangatara naomba unitake radhi, mwenzio mie bado anda eitin, hata harufu ya ndoa bado sijaanza kuisikia.

Nimeyaona hayo kwa marafiki zangu ndio maana nikalileta hapa ili tuhadili tatizibhuwa ni nini??

Kwa upande wangu hata mie nimelelewa kwenye extended family, tuliishi vizuri na ndugu wa kwao baba yangu na wa kwao mama yangu. Nina imani hata mie nitakuja kuishi vizuri na ndugu wa mume mtarajiwa.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom