everlenk
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 11,628
- 15,032
Pole sana ndugu yangu. Naamini hutoi na kujiumiza mwenyewe.
Kwa upande wangu, siwezi kumlaumu mke wangu kwa jinsi yoyote atakavyowatendea ndugu. Hata mimi nilikuwa na mawazo kama wanaume wengine kwamba labda hawapendi ndugu zangu. Ila uzoefu umenifunza kwamba ndugu hawabebeki, hawashibi, hawatosheki.....Kadri unavyojitesa ndivyo wanavyodai zaidi.
Dawa ni kutoa pale unapoweza na kuwahudumia wakiwa kwao!
Asante sana,wewe sasa ni baba kamili,ukikuta mwanaume kaongea haya ujue amekomaa haswaa,nikupongeze kwa hilo.
Haswaa ni kutoa kadri unavyoweza,uchoyo wa nini?kikiwepo ni kutoa tu,kisipokuwepo ndugu aelewe tu hilo halipo na haliwezekaniki.