Wanamshangilia lakini wana mashaka!

Wanamshangilia lakini wana mashaka!

JERUSALEMU

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2012
Posts
3,156
Reaction score
3,626
Habarini wanajamvi!

Nimekuwa nikifuatilia mikutano ya Magufuli, kuna kitu kimoja kiko dhahiri. Wanao mshangilia kuna wakati wanaonesha mashaka nadhani wanapo kumbuka ugumu Wa maisha mtaani. Washangiliji Wa kweli Ni rahisi kuwatambua! Hawa Wa Magufuli wanafanana sana na walio kuwa wanamshangilia IDD Amini.unafiki mtupu.Wanachama na viongozi ndani ya chama chao hawana amani ya moyo! Ku a kitu wanatafakari.
 
Habarini wanajamvi!

Nimekuwa nikifuatilia mikutano ya Magufuli, kuna kitu kimoja kiko dhahiri. Wanao mshangilia kuna wakati wanaonesha mashaka nadhani wanapo kumbuka ugumu Wa maisha mtaani. Washangiliji Wa kweli Ni rahisi kuwatambua! Hawa Wa Magufuli wanafanana sana na walio kuwa wanamshangilia IDD Amini.unafiki mtupu.Wanachama na viongozi ndani ya chama chao hawana amani ya moyo! Ku a kitu wanatafakari.
Kuna ukweli mwingi tu kwenye hii habari
 
Habarini wanajamvi!

Nimekuwa nikifuatilia mikutano ya Magufuli, kuna kitu kimoja kiko dhahiri. Wanao mshangilia kuna wakati wanaonesha mashaka nadhani wanapo kumbuka ugumu Wa maisha mtaani. Washangiliji Wa kweli Ni rahisi kuwatambua! Hawa Wa Magufuli wanafanana sana na walio kuwa wanamshangilia IDD Amini.unafiki mtupu.Wanachama na viongozi ndani ya chama chao hawana amani ya moyo! Ku a kitu wanatafakari.
Kilichopo ni kwamba wale wenye maisha ya chini wanadhani kwamba rais atawashusha wote wenye maisha mazuri ili wawe level moja,km unavyojua watz tunapenda mtu akianguka cyo akipanda/akifanikiwa,niamini niyasemayo chief,hayo ndiyo mawazo ya watz wa hali ya chini wengi..

HAKUNA ANAYEFOCUS KUHUSU MIPANGO YA BAADAYE TITANEEMEKA VIPI LAA HASHA,WENGI WANATAKA RAIS AENDELEE KUFUKUZA WATU KWAKUWA WAO WANADHANI WALIKUWA WANAJIDAI SANA MITAANI..

Nini wanachoshangilia?
Mfano mtu usiyejua alikuwa anafanya kazi gani,wala hujawahi kumsikia,hata hujui amekosa nini hlf mbele ya jukwaa unaulizwa nimtumbueeeee wewe unaitikia mtumbueeee,inawezekana kweli?

HAYA MAKOFI NA VIGELEGELE VYA WATZ NI VYAKIPUMBAVU,NA WENGI HATUJUI MWELEKEO WA HUKU TUENDAKO,NI MATUKIO YASIYOTUNUFAISHA SS WATZ,BALI NI KAMPENI ZA KISAICOLOGY KWA WATZ MAMBUMBUMBU,NA SASA HATA KUHOJI TENA NGUMU,TUPOTUPO TUU,NAKUMBUKA MANENO HAYA:-

ANAANDIKA jenerali ulimwengu



''Tunachagua kama vipofu,kisha tunalalama kama Vichaa. Sasa tuamue; ama tuchague Viongozi wetu kwa umakini au tukae kimya wakati wakitunyanyasa''.........
 
Habarini wanajamvi!

Nimekuwa nikifuatilia mikutano ya Magufuli, kuna kitu kimoja kiko dhahiri. Wanao mshangilia kuna wakati wanaonesha mashaka nadhani wanapo kumbuka ugumu Wa maisha mtaani. Washangiliji Wa kweli Ni rahisi kuwatambua! Hawa Wa Magufuli wanafanana sana na walio kuwa wanamshangilia IDD Amini.unafiki mtupu.Wanachama na viongozi ndani ya chama chao hawana amani ya moyo! Ku a kitu wanatafakari.
Uliingia kwenye roho zao ukakuta hawana amani?

Hivi hizi shule za kusomea ujinga zinapatikana wapi ambako wengine hatuzipati?
 
Habarini wanajamvi!

Nimekuwa nikifuatilia mikutano ya Magufuli, kuna kitu kimoja kiko dhahiri. Wanao mshangilia kuna wakati wanaonesha mashaka nadhani wanapo kumbuka ugumu Wa maisha mtaani. Washangiliji Wa kweli Ni rahisi kuwatambua! Hawa Wa Magufuli wanafanana sana na walio kuwa wanamshangilia IDD Amini.unafiki mtupu.Wanachama na viongozi ndani ya chama chao hawana amani ya moyo! Ku a kitu wanatafakari.
It is very true.

Unapokuwa na Mkuu wa nchi wa aina ya JPM, hakuna mtu ambaye ndani ya moyo wake anaweza kuwa na amani kwa asilimia 100.

Kwa kuwa Mkuu ameamua kuiendesha hii nchi kwa staili ya ONE MAN SHOW, na bila kuzingatia Katiba ya nchi inamuelekeza vipi na kwa staili ya kutoa matamko ya majukwaani........

Kwa hiyo hakuna anayeweza kutabiri kuwa kesho Mheshimiwa ataibuka na tamko gani......

Tumeshuhudia matamko mengi sana yenye utata mkubwa.

Nitatoa mfano wa matamko hayo yenye ukakasi mkubwa.

1. Ni mimi pekee ambaye ninapaswa kuzunguka nchi nzima na kuwaeleza watanzania ambacho Serikali yangu inachotegemea kuwafanyia watanzania, wanasiasa wengine wa vyama vya upinzani nawapa likizo hadi mwaka 2020.......

2. Nasikia kuna watu wanasema bandari yetu ya Dar haina tena meli zinazoleta mizigo TZ, niwaambie waTz kuwa tunataka meli zinazolipa kodi, hao waliokimbiza meli zao ni wale waliokuwa hawalipi kodi, waache waende kwenye hizo bandari za nchi nyingine wanakoruhusu ukwepaji kodi.......

3. Nasikia watalii wanatishia kutokuja nchini kutokana na Serikali yangu kuintroduce VAT kwa watalii, nami nasema hao watalii na waende zao, mimi nataka watalii wenye pesa zao wenye uwezo wa kulipa kodi........

4. Watumishi wote wa Umma wahamie Dodoma haraka iwezekanavyo, wakiendelea kubaki Dar wajue kuwa nyumba zote za serikali zilizoko Dar nitaziuza na zigeuzwe kuwa Hoteli, kwa hiyo hao watumishi watakaobaki Dar watakuwa wamejifukuzisha kazi na itabidi watafute nyumba zao za kuishi......

5. Nitawashusha wale waliokuwa wanaishi kama Malaika na hivi sasa waishi kama mashetani.......

Hakika TZ hivi sasa tunapita katika kipindi kigumu sana ambacho huwezi kutabiri Mkuu wa nchi ataibuka na tamko gani kesho..........

Hivi sasa nakumbuka maneno ya busara aliyowahi kutamka baba wa Taifa katika moja ya hotuba zake miaka ile ya 90 kuwa watanzania ni lazima tuchague Rais ambaye ataiheshimu na kuitii Katiba ya nchi yetu, kama tutapata Rais ambaye hatataka kuitii na kuiheshimu Katiba yetu ya nchi, Mwalimu aliongea kwa msisitizo mkubwa kuwa Rais wa aina hiyo HATUFAI.............
 
Yaani usiku na mchana mnavyomsema mh raisi vibaya utadhani huyo wa kwenu ni mkamilifu. Sio fair. Semeni pia kazi nzuri anazofanya.
 
Yaani usiku na mchana mnavyomsema mh raisi vibaya utadhani huyo wa kwenu ni mkamilifu. Sio fair. Semeni pia kazi nzuri anazofanya.
Tatizo sio kuwa mkamilifu, bali ni ule ubabe na Udikteta wa kutokuwa tayari kukosorewa, kushuriwa na kuwasikiliza wengine wenye mawazo tofauti.
 
Yaani usiku na mchana mnavyomsema mh raisi vibaya utadhani huyo wa kwenu ni mkamilifu. Sio fair. Semeni pia kazi nzuri anazofanya.
Atasifiwa mwishoni sio sasa...ukosoaji wa sasa usitafsiriwe vibaya kuna ukweli mwingi tu kwenye huo ukosoaji na unamkumbusha yeye ni nani yuko wapi na anatakiwa afanye nini kwenye nini. ...
Jamiiforum iko hapa ilipo kwakuwa ilivumilia ukosoaji na kujisahihisha pale ilipopotoka, sasa hivi ni mojawapo ya mitandao bora kabisa Tanzania
 
Uliingia kwenye roho zao ukakuta hawana amani?

Hivi hizi shule za kusomea ujinga zinapatikana wapi ambako wengine hatuzipati?

mkuu ni kweli kutumbua ni vyema, je maisha uetu yameboreka kwa kiwango gani? viwanda.ambavyo ndio vilihubiriwa viko wapi? kuhamoa Dodoma kutaboresha vip maisha yetu?
 
Sijasema mumsifie. Hata ukisoma nilichoandika sijasema mumsifie. Na sijasema tusimkosoe. Nachosema ni kuwa museme pia kazi nzuri anazofanya ndio fairness hiyo. Yaani watu wanakaa usiku na mchana kuona wapi mh raisi anakosea hii sio sahihi. Huyo wa kwenu 2 years tu kashfa na katolewa na kamati halali ya BUNGE iliyoundwa.
 
Tulieni,tuliwaambia mapema mkatuona wajinga ! Sisi wengine na akili zetu hatushangai haya bali tunashangaa wanaonshangilia...
 
mkuu ni kweli kutumbua ni vyema, je maisha uetu yameboreka kwa kiwango gani? viwanda.ambavyo ndio vilihubiriwa viko wapi? kuhamoa Dodoma kutaboresha vip maisha yetu?
Mkuu;
Waliokaa na kuamua utawala wa kidemokrasia utapimwa baada ya miaka mitano au saba hawakuwa wajinga.

Kuanza kuuliza kwa sasa kuwa maisha yako yameboreka vipi ni kama unaonyesha hufahamu maana ya kipimo cha utendaji wa serikali.

Hata serikali ina mpango wa kiuchumi wa mwaka mmoja na mitano. hakuna mpango wa kiuchumi wa miezi miwili.

Hata mwaka haujaisha, unaanza kuuliza maisha yako yameboreka vipi.
 
Haya maisha watz hamkuzoea alipokuwa wazir kauli zake hizi mliziona poa, watz unafiki utawaua sasa nami natoa kauli km ya mkuu " hii Ngoma mpaka 2025 asiyemtaka ahame nchi"
 
Kuna zaidi ya kusomesha. Ana uhakika ataendelea kutawala milele wakati si tuna mpango wa kumpiga chini 2020
 
Back
Top Bottom