Wanafunzi wa advance Chamwino wamnunulia mwalimu wa hesabu baiskeli kwa kutambua mchango wake!

ngebe

JF-Expert Member
Jun 8, 2020
1,789
5,105
Wanafunzi wa Kidato cha sita Shule ya Sekondari Chamwino wamempa FURAHA YA KUSHTUKIZA mwalimu wao wa HESABU/ADVANCED MATHEMATICS, MR. EMANUEL GEORGE KIPAHO kwa kumnunulia usafiri wa Baiskeli kwa kutambua mchango wake na juhudi zake anazozitoa kufundisha darasani na muda wake wa Ziada.

Shule hii ina michepuo miwili ya EGM NA CBG mwalimu huyu amekuwa mhimili sana kwa wanafunzi hawa.

Matokeo ya kidato cha sita kwa shule hii yamekuwa yakiongozwa na mchepuo wa EGM.

Nafikiri CHAMA CHA WALIMU pamoja na Serikali tuendelee kutoa motisha na Hamasa kwa walimu kama hawa kwani licha ya kutimiza majukumu yao lakini wanatumia muda wao wa ziada kuhakikisha wanapata kizazi Bora.

Leo hawa wanafunzi wametoa Baiskeli kulingana na uwezo wao kuna siku watatoa zawadi ya gari.

Chama kinaweza kuwatambua hata kwa kuwapa vyeti vya uwajibikaji Bora hii itapelekea Walimu kujituma zaidi.

Mwalimu Kipaho pia ni Mwalimu wa Nnidhamu. Mungu amjalie afya pamoja na Walimu wote wanaotumia muda wao wa ziada kuhakikisha Wanafunzi wanafanya vizuri.💪
FB_IMG_16907100669025496.jpg
 
Kuna mwalimu mmoja alikuwa anaitwa Mwl.Ibambasi hata mimi nilitamani siku moja nimpe zawadi kubwa sana,alikuwa anafundisha chemistry na biology,huyu mwalimu alikuwa anajituma sana,yaan alitufanya tukawa kama makinda ya ndege yaan anatafuna sie ni kumeza tu

Alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kufundisha na kuchambua notice kuzifanya ziwe simple
 
Kuna mwalimu mmoja alikuwa anaitwa Mwl.Ibambasi hata mimi nilitamani siku moja nimpe zawadi kubwa sana,alikuwa anafundisha chemistry na biology,huyu mwalimu alikuwa anajituma sana,yaan alitufanya tukawa kama makinda ya ndege yaan anatafuna sie ni kumeza tu

Alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kufundisha na kuchambua notice kuzifanya ziwe simple
Hongera kwa moyo huo
 
Hongera Mwalimu wangu wa shule ya msingi ulinifanya nitishe sana kwenye Hilo somo, mpaka kujukikana katani na wilaya. Mwisho nikitandika Banda "A" A level pale special school Tabora miaka hiyo. Nilipopata kazi nilitia kwako Zawadi ndogo. Ngoja nijipapatue Tena katika kuuenzi huu Uzi.
 
Wanafunzi wa Kidato cha sita Shule ya Sekondari Chamwino wamempa FURAHA YA KUSHTUKIZA mwalimu wao wa HESABU/ADVANCED MATHEMATICS MR. EMANUEL GEORGE KIPAHO kwa kumnunulia usafiri wa Baiskeli kwa kutambua mchango wake na juhudi zake anazozitoa kufundisha darasani na muda wake wa Ziada. Shule hii ina michepuo miwili ya EGM NA CBG mwalimu huyu amekuwa mhimili sana kwa wanafunzi hawa. Matokeo ya kidato cha sita kwa shule hii yamekuwa yakiongozwa na mchepuo wa EGM. Nafikiri CHAMA CHA WALIMU pamoja na Serikali tuendelee kutoa motisha na Hamasa kwa walimu kama hawa kwani richa ya kutimiza majukumu yao lakini wanatumia muda wao wa ziada kuhakikisha wanapata kizazi Bora. Leo hawa wanafunzi wametoa Baiskeli kulingana na uwezo wao kuna siku watatoa zawadi ya gari. Chama kinaweza kuwatambua hata kwa kuwapa vyeti vya uwajibikaji Bora hii itapelekea Walimu kujituma zaidi. Mwalimu Kipaho Pia ni Mwalimu wa Nidhamu. Mungu amjalie afya pamoja na walimu wote wanaotumia muda wao wa ziada kuhakikisha wanafunzi wanafanya vzr.💪
View attachment 2702939
Kwamba mwalimu hana hata pikipiki?
 
Huo mda wa ziada ungekuwa na duka lako na mitego mingine,usingesubiri motisha.Mwalimu anayetafuta huwezi kumkuta anajikomba eti apewe nafasi ya kusimamia pepa ili apate laki sita wala kusahihisha necta,atafanya kazi kulingana na mwongozo basi.Mtu unapata mda wa kushinda na wanafunzi baada ya mda wa kazi huyo mtu atafanya maendeleo yake sa ngapi?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Huo mda wa ziada ungekuwa na duka lako na mitego mingine,usingesubiri motisha.Mwalimu anayetafuta huwezi kumkuta anajikomba eti apewe nafasi ya kusimamia pepa ili apate laki sita wala kusahihisha necta,atafanya kazi kulingana na mwongozo basi.Mtu unapata mda wa kushinda na wanafunzi baada ya mda wa kazi huyo mtu atafanya maendeleo yake sa ngapi?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Madam, umeongea point sana. We unafaa kuwa mke, nikaribishe PM tuyajenge.
 
Huo mda wa ziada ungekuwa na duka lako na mitego mingine,usingesubiri motisha.Mwalimu anayetafuta huwezi kumkuta anajikomba eti apewe nafasi ya kusimamia pepa ili apate laki sita wala kusahihisha necta,atafanya kazi kulingana na mwongozo basi.Mtu unapata mda wa kushinda na wanafunzi baada ya mda wa kazi huyo mtu atafanya maendeleo yake sa ngapi?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Wito.
 
Huo mda wa ziada ungekuwa na duka lako na mitego mingine,usingesubiri motisha.Mwalimu anayetafuta huwezi kumkuta anajikomba eti apewe nafasi ya kusimamia pepa ili apate laki sita wala kusahihisha necta,atafanya kazi kulingana na mwongozo basi.Mtu unapata mda wa kushinda na wanafunzi baada ya mda wa kazi huyo mtu atafanya maendeleo yake sa ngapi?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Sio kila mtu motivation ya akifanyacho ni kuwinda pesa tu ingekuwa ni hivyo tusingekuwa na masista au mapadre

Bill Gates aliwahi hojiwa siri ya mafanikio yake nini hadi.kuwa bilionea namba moja duniani akasema siri moja penda kitu chako kifanyie kazi kwa nguvu akili na juhudi zote pesa na shukrani zitakuja baadaye

Akasema yeye anapenda sana kazi zake za Microsoft products na hulala masaa matatu kwa siku akasema kupenda kazi yangu kumesaidia watu kunipa pesa kwa kununua bidhaa zangu

Akasema penda unachofanya utafanikiwa

Huyo mwalimu yuko vizuri anapenda anachofanya na matunda yanaanza kuonekana

Sasa mwalimu hupendi ualimu.mitoto haielewi unachofundisha matokeo yakija ma FFF kibao unataka nani aku reward?

Unatakiwa kuwa na concentration kama umeamua kuwa Mwalimu concentrate kwenye ualimu utalipa tu sio uko darasani unawaza duka lako au bodaboda yako .Utafundisha chini ya kiwango na kuzalisha matokeo mabovu mno ambayo ungekuwa shule za private wanakufukuza kazi

Narudia sio kila umuonaye kazini motivation yake ni pesa kama wewe ndio maana ualimu unaotwa wito

Huyo mwalimu ana wito halisi wa ualimu
 
Wanafunzi wa Kidato cha sita Shule ya Sekondari Chamwino wamempa FURAHA YA KUSHTUKIZA mwalimu wao wa HESABU/ADVANCED MATHEMATICS MR. EMANUEL GEORGE KIPAHO kwa kumnunulia usafiri wa Baiskeli kwa kutambua mchango wake na juhudi zake anazozitoa kufundisha darasani na muda wake wa Ziada. Shule hii ina michepuo miwili ya EGM NA CBG mwalimu huyu amekuwa mhimili sana kwa wanafunzi hawa. Matokeo ya kidato cha sita kwa shule hii yamekuwa yakiongozwa na mchepuo wa EGM. Nafikiri CHAMA CHA WALIMU pamoja na Serikali tuendelee kutoa motisha na Hamasa kwa walimu kama hawa kwani richa ya kutimiza majukumu yao lakini wanatumia muda wao wa ziada kuhakikisha wanapata kizazi Bora. Leo hawa wanafunzi wametoa Baiskeli kulingana na uwezo wao kuna siku watatoa zawadi ya gari. Chama kinaweza kuwatambua hata kwa kuwapa vyeti vya uwajibikaji Bora hii itapelekea Walimu kujituma zaidi. Mwalimu Kipaho Pia ni Mwalimu wa Nidhamu. Mungu amjalie afya pamoja na walimu wote wanaotumia muda wao wa ziada kuhakikisha wanafunzi wanafanya vzr.
View attachment 2702939
Vizuri

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom