Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 4,953
- 4,326
Leo Waziri wa Afya ametangaza virusi hatari vya Corona kuwepo nchini mwetu. Mgonjwa mmoja amethibitishwa kwa vipimo vinavyofanywa kwenye maabara moja tu hapa nchini kwetu.
Maana yake kuna uwezekano wa kuwepo wengine wenye virusi hivyo ambao hawajabahatika kufanyiwa vipimo hivyo au ni carriers.
Cha ajabu, baada ya tangazo hilo, kiongozi wa chama kimoja kikubwa cha siasa katangaza kufanyika mikutano ha hadhara nchi nzima kila siku bila kikomo kuanzia wiki ijayo hadi Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
Tusifanye mzaha na virusi hivi vya Corona. Na vikiendelea kuwepo hata Uchaguzi mkuu wa mwaka huu lazima tutauahirisha.
----
Serikali ipige marufuku machinga mjini
-----
Misongamano kwenye usafiri wa umma idhibitiwe
----
Maeneo ya kufunga na mambo ya kuzuia ili kuepusha coronavirus Dar es Salaam
Maana yake kuna uwezekano wa kuwepo wengine wenye virusi hivyo ambao hawajabahatika kufanyiwa vipimo hivyo au ni carriers.
Cha ajabu, baada ya tangazo hilo, kiongozi wa chama kimoja kikubwa cha siasa katangaza kufanyika mikutano ha hadhara nchi nzima kila siku bila kikomo kuanzia wiki ijayo hadi Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
Tusifanye mzaha na virusi hivi vya Corona. Na vikiendelea kuwepo hata Uchaguzi mkuu wa mwaka huu lazima tutauahirisha.
----
Serikali ipige marufuku machinga mjini
Kwa ugonjwa huu wa Corona mikusanyiko ya na misongamano ni kichocheo kikubwa cha maambukizi, ukiangalia hali ya hewa ya baadhi ya Maeneo ya nchi hasa ukanda wa pwani, mahsusi Dar as salaam.
Vituo vya mabasi vya Kimara mwisho, Ubungo, Ferry, Kariakoo Mbagala, utaona hilo ni bomu linalo Subiri kulipuka, nilipita Kariakoo misongamano ni mkubwa sana, inazidi hata baadhi ya mikusanyiko inayokuwepo wakati wa kuangalia ligi kuu ya mpira.
Kwanini serikali inashindwa kupiga Marufuku machinga kariakoo na wauza bidhaa barabarani kwa sababu wanasababisha misongamano isiyo ya lazima, wamepanga bidhaa zao chini na kusabisha Barabara kuwa nyembamba.
Hivi hatuoni mitaa ya nchi ya wenzetu kwa sasa walivyochukua hatua thabiti, mabasi na madaladala yanajaza kupita kipimo, tumeambiwa ugonjwa huu unaambukiza kwa chafya, kugusana na kupitia jasho
Machinga wanaouza vitu kwenye magari kwenye mataa wanasika kila kitu unaponunua kitu kwa machinga hatujui bidhaa hizo watu Wangapi wanakuwa wameshika! kwa kuangalia au kurudisha wakiwa na nia ya kununua, Machinga wanakuwa wametokwa na majasho kwa kushinda juani na hali ya hewa ilivyo Mungu saidia
Tunalipa pesa kama nauli na tunapokea chenji, tunapeleka nyumbani bidhaa na chenji fikiria kama kuna maambukizi, kesho yake pia tunakwenda kazini, yaani mzunguko ni mkubwa sana
Nafikiri ni busara tuchukue hatua sasa, Ulaya na Marekani ni Marufuku mikusanyiko ya watu zaidi ya 10 kukaa pamoja.
sisi tuna nini hadi tupuuze hayo, piga picha kama Machinga wataondolewa barabarani Kariakoo kutaonekana vipi naomba wahusika wachukue hatua haraka, kuna huduma za lazima kama wauza chakula nk wanaweza kubaki lakini siyo machinga wauza viatu nguo nk. Itabidi waondoke kutusitiri
Machinga wakiondolewa hata usafiri wa wala daladala na mabasi ya mwendo kasi utakuwa na ahueni
-----
Misongamano kwenye usafiri wa umma idhibitiwe
Naomba uzi huu usiungwe...
Natambua hatua ambazo Serikali Inachukua kuepusha kuenea kwa maambukizi ya Virusi wa Corona
Lakini Kuna ushaghalabaghala wa Usafiri wa daladala Dar naona Serikali haisemi chochote na mle tunasafiri watu kibao wana Mafua na wanapiga chafya za hatari...So inakuwaje?
Hivi ukifunga shule, halaf utaratibu wa hovyo wa usafiri wa Umma Dar ukaachwa uendelee kama ulivyo si Serikali inakuwa inajitaabisha tu?
Naona serikali kama imejigusagusa tu lakini inashindwa kuchukua hatua madhubuti kwa ujumla wake..
Daladala na Mwendokasi wanapaswa kuelekezwa wasipakie abiria wa kusimama, na zaidi wadhibitiwe kuhusu usafi wa magari yao maana mengi ni machafu mno.
Na hata sijasikia waseme chochote kuhusu kufunga Viwanja vya Ndege...
IT SHOULD BE A TOTAL LOCKDOWN ...wanahofia kukosa mapato? We cannot prioritize money over lives, Come on guys!
----
Maeneo ya kufunga na mambo ya kuzuia ili kuepusha coronavirus Dar es Salaam
Baada ya Corona kuingizwa Arusha na mrembo na tajiri mwenye shule za binafsi, sasa muda wowote itaingia Dar kupitia wasanii wa Bongo Fleva wanaotoka kupiga Show ulaya.
Ili kuzuia hatua zifuatazo zichukuliwe leo hii:
1. Harusi zote zisitishwe
2. Misiba wahudhurie ndugu tu, wasizidi 20.
3. DART-mwendokasi upigwe marufuku
4. Machinga wote waliozagaa mjini kwa tamko la JIWE waondoshwe na kurudishwa makwao.
5. Mabasi yaendayo nje ya nchi yasitshe safari.
6. JKT WARUDISHWE NYUMBANI.
7. MAHABUSU/wafungwa WOTE NA WALE WALIOPO VITUONI WAPEWE DHAMANA[Iran imeachia wafungwa karibu wote kila mtu akapambane na hali yake]
8. KWARESMA NA NJIA YA MSALABA IPIGWE MARUFUKU
9. BEACH ZOTE ZA UMMA zipigwe marufuku.
10. Betting offices zifungwe
11. Wale makahaba wote wa Sinza, Buguruni walipwe fedha/ruzuku, ili wakae nyumbani.
12. Kupanda daldala iwe LEVEL SEAT, NA KUINGIA KWA FOLENI/MSTARI na kila mtu alipe kwa tigo pesa.
13.Traffic akikukamata hakuna kumpa leseni, wataeneza ugonjwa.
14. Gest houses zote zifungwe na zibaki hoteli tu.
15. CCM LUMUMBA vile vijiwe vya kahawa vifungwe vyote
HATUA ZA KUCHUKUA
1. mawaziri wote watoke ofisini wakapime watu mipakani na viwanja vya ndege
2. Magufuli aaachie zile 1.5 T zinunulie vipimaji uginjwa na sanitisers
3. Serikali imuwajibishe Ummy mwalimu kwa kushindwa kuchukua hatua mapema ilhali alijua huku nguvu kubwa akielekeza kwenye kufungua warsha na semiana na kushinda saluni kujipodoa.
4. Wabunge wote ewaliopinga hoja ya msigwa ya mwezi wa pili mwaka huu kuhusu kujadili Corona wafunguliwe mashitaka ya CCM yyani uhujumu uchumi, maana wangekubali hili jambo lisingekuwa hivi