Sekta ya utalii kimataifa kufufuka tena baada ya China kulegeza hatua za udhibiti wa COVID-19

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111415845138.jpg


Jumapili, Januari 8, 2023, China ilitangaza kulegeza zaidi hatua za udhibiti wa virusi vya Corona, na kuondoa masharti ya kuweka wasafiri karantini mara wanapowasili nchini China kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

Tangu mlipuko wa COVID-19 ulipotokea mwishoni mwa mwaka 2019 na kesi ya kwanza kugunduliwa mjini Wuhan, serikali ya China, chini ya uongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ilichukua hatua za haraka na kali kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi hivyo yanadhibitiwa.

Ingawa baadhi ya nchi zilibeza hatua hizo za China, lakini nchi hii yenye watu bilioni 1.4 ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti maambukizi na vifo vinavyotokana na virusi hivyo, hali ambayo ni tofauti na ilivyokuwa katika nchi nyingine, kama vile Marekani.

Mwishoni mwa mwaka jana, China ilianza kulegeza hatua kali za udhibiti wa virusi vya Corona, na tarehe 27 Desemba, nchi hiyo ikatangaza kuwa, sharti la kuwekwa karantini kwa abiria wote wanaoingia nchini China kutoka nchi za nje litafutwa. Pia China ilitangaza kuwa idadi ya ndege za kimataifa za abiria iliyokuwa imewekwa wakati wa udhibiti wa virusi hivyo pia imefutwa, na abiria kuruhusiwa kuingia China bara kupitia usafiri wa anga na majini ukaanza kurejea hatua kwa hatua.

Hatua za udhibiti wa maambukizi ya COVID-19 zilizochukuliwa na nchi mbalimbali zimekuwa na athari kubwa kwa uchumi wa nchi husika, na sekta ambazo zilikuwa zinachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa kwa nchi husika pia ziliathiriwa, ikiwemo sekta ya utalii.

Inafahamika kuwa, idadi kubwa ya watalii kimataifa ni Wachina, hivyo kutokana na hatua za udhibiti wa COVID-19 ndani na nje ya China, sekta hii iliathirika pakubwa.

Lakini, mara baada ya China kutangaza mabadiliko katika hatua za udhibiti wa virusi hivyo, nchi mbalimbali zimepongeza hatua hiyo na kukaribisha watalii kutoka China.

Nchini Misri, wamiliki wa maduka katika eneo maarufu la watalii la Khan el-Khalili mjini Cairo, wameeleza matarajio mazuri ya kupokea watalii kutoka nchini China, hii ni baada ya China kutangaza kuondoka vizuizi vya usafiri kuanzia Januari 8, 2023. Wamiliki hao wanasema, kabla ya janga la COVID-19, biashara ilikuwa nzuri na watalii wengi walikuwa wakitembelea eneo hilo, hususan watalii kutoka nchini China.

Kabla ya mlipuko wa COVID-19, China ilikuwa inachukua nafasi ya nne kwa utalii nchini Misri, huku mamia kwa maelfu ya watalii kutoka China wakitembelea maeneo ya kihistoria na pia kufurahi katika fukwe za kuvutia nchini humo.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii, nchi nyingi zinatangaza vivutio vya utalii kwa ajili ya watalii kutoka China, na hivyo kuonyesha kuwa, hatua ya China kuondoa vizuizi vya usafiri, itachukua nafasi muhimu katika kufufua sekta ya utalii ambayo iliathirika vibaya kutokana na janga la COVID-19.
 
Back
Top Bottom