#COVID19 China imejizatiti kurejesha hali ya kawaida kama ilivyo kabla ya kuibuka kwa janga la COVID-19

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
Caroline Nassoro

12342424.jpg
Hivi karibuni, serikali ya China ililegeza masharti na hatua za kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19), na hii inatokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kudhibiti kuenea na vifo vinavyotokana na virusi hivyo. Binafsi, hatua hii imenipa matumaini makubwa kuwa janga hili ambalo limeitikisa dunia, linaelekea kumalizika.

Januari 23, mwaka 2020, ambao ulikuwa ni usiku wa mkesha wa Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina, serikali kuu ya China ilitangaza kufunga safari zote za ndani na nje ya nchi kutokana na mlipuko wa virusi ambavyo vilikuwa vinasababisha homa kali, matatizo katika mfumo wa kupumua, na vifo.

Ghafla, katika Sikukuu hiyo ambayo huwa imejaa shangwe na nderemo, kulikuwa na ukimya ulionishangaza, maana baada ya kuishi Beijing, mji mkuu wa China kwa miaka 10, ilikuwa ni jambo la kushangaza na kushtua kuona mji ukiwa kimya na hakuna watu wanaotembea mtaani wala magari barabarani, isipokuwa mabasi machache ya usafiri wa umma na teksi.

353535353.jpg


Hatua kali zilizochukuliwa na serikali kuu ya China, ikiwemo kufunga safari za kuingia na kutoka mji wa Wuhan ambapo kesi ya kwanza iligunduliwa na mikoa mingine, kufunga usafiri wote wa umma na wa binafsi, na kuvaa barakoa pamoja na kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka zilisaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza maambukizi na vifo vinavyotokana na virusi hivyo ambavyo baadaye vilipewa jina la COVID-19.

Jambo lingine ambalo lilinigusa ni jinsi ambavyo wananchi walivyoonyesha kuunga mkono juhudi za serikali na kutekeleza maelekezo yote tena kwa ufanisi. Baadhi ya watu waliokuwa na uwezo wa kufanya kazi kutoka nyumbani walishauriwa kufanya hivyo ili kupunguza msongamano na kuweka umbali wa kijamii, na shule pia zilifungwa na wanafunzi kutakiwa kusoma nyumbani kupitia mtandao (online).

Pia serikali kuu ya China kwa kushirikiana na kampuni za simu, zilianzisha APP ambazo zilikuwa msaada mkubwa katika kudhibiti maambukizi, moja ikiwa ni ile ya kuonyesha hali ya afya (health kit) na nyingine ambayo binafsi niilipa jina la mshale wa kijani, ambayo ilikuwa inaonyesha kuwa mtumiaji wa simu alikuwa na hali nzuri, na hajalazwa ama kwenda hospitali kutokana na homa kali.

Watumiaji wote wa simu janja walilazimika kuwa na APP hizo ambazo zimetoa mchango mkubwa sana katika ufuatiliaji wa watu waliowasiliana kwa karibu na mtu aliyekuwa na maambukizi.

3546456464.jpg


Kutokana na umakini wa serikali na uungaji mkono wa wananchi kwa serikali yao, China ilipata mafanikio makubwa katika kudhibiti maambukizi ya COVID-19. Miezi sita baada ya janga hilo kuibuka na shughuli zote za kijamii na uzalishaji kusimamishwa ili kudhibiti maambukizi, hatua kwa hatua, serikali ilifungua tena shughuli za kijamii na uzalishaji, lakini kwa kufuata mwongozo maalum uliotolewa na mamlaka husika za afya.

Shule zilifunguliwa na watoto wakaanza tena masomo darasani badala ya kupitia mtandao, wafanyakazi wakaenda makazini, na biashara pia zikafunguliwa, lakini yote haya yalifanyika kwa kufuata taratibu na kanuni zilizotolewa na serikali kuu na mamlaka husika.

Licha ya kwamba mafanikio makubwa yamepatikana katika kudhibiti maambukizi, lakini katika miaka hii mitatu mawimbi ya hapa na pale yamekuwa yakitokea, lakini hatua za ufanisi na za haraka zilizochukuliwa zimesaidia kuhakikisha kwamba maambukizi hayo yanadhibitiwa katika maeneo husika.

Mwaka 2021, virusi vya Corona vilivyobadilika ikiwemo Delta vilishambulia nchi mbalimbali, na kusababisha vifo vya watu milioni 3.5 kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO). Katika nusu ya pili ya mwaka huo, Marekani, nchi iliyopata pigo kubwa zaidi katika janga hilo ilishuhudia maambukizi mapya zaidi ya laki moja kwa siku na vifo elfu moja vilivyotokana na ugonjwa huo kwa siku. Wakati huohuo, ni watu wawili tu waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini China katika mwaka huo.

Mwezi April mwaka 2022, wimbi jipya la COVID-19 liliibuka mjini Beijing, na hivyo kuwalazimu wakazi wa jiji hilo kupima COVID-19 kila baada ya siku kadhaa. Lakini haya yote yanafanyika wakati shughuli za kijamii na uzalishaji zikiendelea, isipokuwa katika maeneo ambako maambukizi ni mengi, na hivyo hatua stahiki kuchukuliwa na mamlaka za sehemu husika.

Sasa, baada ya takriban miaka mitatu ya mapambano dhidi ya janga hili, China imekuwa na utaratibu bora wa matibabu na udhibiti wa magonjwa, na ina tiba yenye ufanisi na dawa, haswa dawa za jadi za Kichina, kiwango utoaji wa chanjo kamili kimefikia zaidi ya asilimia 90%.

Pamoja na hayo, ufahamu na ujuzi wa umma kuhusu afya umeboreshwa kidhahiri, na uwezo wa virusi vya Corona aina ya Omicron kupungua.

Mwanzoni mwa mwezi huu, serikali kuu ya China iliamua kulegeza zaidi hatua za udhibiti wa maambukizi ya COVID-19, ikiwa ni pamoja kuruhusu watu kusafiri nje ya maskani zao bila ya kutakiwa kuonyesha hali ya afya zao, na hata APP ya kuonyesha hali ya afya pia haitumiki tena katika baadhi ya sehemu.

Naibu Waziri Mkuu wa China Bibi Sun Chunlan Jumanne wiki hii alisisitiza kuwa, kwa sasa kipaumbele cha kazi kinahamishwa kutoka kuzuia maambukizi hadi matibabu, kwa lengo la kulinda afya za watu na kuzuia watu walioambukizwa kupata dalili kali zaidi ili kuhakikisha muda huu wa mpito unakuwa shwari.

Amesema kanuni ya kutoa kipaumbele kwa watu na maslahi yao inatakiwa kufuatwa ipasavyo, na vilevile kuna haja kubwa ya kuratibu ipasavyo hatua za kukabiliana na COVID-19 na maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Hatua hizi zimeonyesha kuwa China ina uwezo wa kukabiliana na janga hili, na imejizatiti kuona hali mpya ya kawaida kama ilivyo kabla ya mwaka 2019 kwa kuendana na mahitaji ya wananchi wake.
 
Sauti za watu/wananchi lazima zisikilizwe na zizingatiwe kwa kua wao ndio wanao toa dhamana ya kuongoza nchi , bado Iran lazima nao watimize matakwa ya wananchi wao ili usalama wa nchi usiharibike.

Pongezi kwa serikali ya China kwa kusikiliza malalamiko ya wananchi wake kwa haraka zaidi na kuya timiza pasipo kuharibu usalama wa nchi.

Serikali ya Tanzania inapaswa kubadilika na kukubali kuwajibika pale baadhi ya mambo yanapo lalamikiwa na wananchi wake kuto kutimizwa.
 
Back
Top Bottom