mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Charles Mbuge, amepiga marufuku mikusanyiko yote isiyokuwa ya lazima na kuwataka wananchi kuzingatia kanuni za afya ili kuzuia kasi ya maambukizi ya virusi vya Corona.
Meja Jenerali Mbuge amesema hatua hiyo inatokana na mkoa wa Kagera kupakana na nchi nne ambazo tayari zimeathirika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa wa covid-19.
Aidha amewaagiza watendaji wa halmashauri zote nane za mkoa wa Kagera kuhakikisha wanasimamia maagizo ya Serikali juu ya kujikinga na ugonjwa wa corona.
Mbali na mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Charles Mbuge, pia Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Muhandisi Robert Gabriel na mkuu wa mkoa wa Iringa, Queen Sendiga nao tayari wameshatangaza kupiga marufuku kwa mikusanyiko isiyokuwa ya lazima ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona kwa wananchi wake.
Meja Jenerali Mbuge amesema hatua hiyo inatokana na mkoa wa Kagera kupakana na nchi nne ambazo tayari zimeathirika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa wa covid-19.
Aidha amewaagiza watendaji wa halmashauri zote nane za mkoa wa Kagera kuhakikisha wanasimamia maagizo ya Serikali juu ya kujikinga na ugonjwa wa corona.
Mbali na mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Charles Mbuge, pia Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Muhandisi Robert Gabriel na mkuu wa mkoa wa Iringa, Queen Sendiga nao tayari wameshatangaza kupiga marufuku kwa mikusanyiko isiyokuwa ya lazima ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona kwa wananchi wake.