Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,328
- 24,211
John Malecela
Salim Ahmed Salim
Mrisho Kikwete
Balozi Mahiga
Liberata Mulamula
Balozi Asha Rose Migiro( kunradhi balozi)
Prof Anna Tibaijuka( kunradhi Prof)
Kuna wakati Tanzania tulikuwa na hazina kubwa ya wanadiplomasia waliokubuhu kutetea maslahi ya nchi na Afrika kwa ujumla.
Kizazi hicho sasa kimeanza kutoweka kwa kasi.
Wana Diplomasia wanaoteuliwa sasa kuwa Mabalozi ni wale waliostaafu kazini na kiukweli hawana nguzu za kuendesha diplomasia kikamilifu.
Tulikuwa na Career Diplomats, Diplomats waliokulia, kufundishwa na kutekeleza kazi za kidiplomasia kwa weledi mkubwa.
Walikuwa wana uwezo wa kudiffuse diplomatic tiffs ktiya nchi na nchi, na kati ya nchi yetu na nchi nyingine duniani.
Hili limenijia kichwani baada ya sherehe ya juzi kumuenzi Dr Salim Ahmed Salim , mwana Diplomasia aliyebobea na kujulikana duniani pote.
Je leo tunaweza kupata mwana diplomasia mwenye CV utendaji na kuthubutu kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UN auo Umoja wa Afrika?
Serikali ingefaa kuliona hili kwa uzito wake.
UPDATE
Asante sana mama Samia, kwa tamko lako la kuirudishia Tanzania umaarufu uliokuwa nao kidiplomasia.
Nakushukuru Mama Samia kwa kuwa msikivu, kwa michango chanya kwa Taifa.