Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Katika historia ya nchi hii, hakijawahi tokea kipindi cha majaribu ya aina hii, ambayo wanaccm wanapitia hivi sasa
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa, umewavua nguo na hivi sasa mpo uchi wa mnyama
Kitendo cha hao wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada wa CCM kukata majina ya wagombea wa upinzani kwa sababu za kipuuzi kabisa, ambazo hata mtoto mdogo hawezi kuthubutu kuzifanya
Tumeshuhudia hao wasimamizi wa uchaguzi wakikata majina ya wagombea wa upinzani kuwa eti hawajui kusoma na kuandika, ambapo wengine ni diploma holders!
Tumeshuhudia pia wakidai kuwa baadhi ya wagombea wa upinzani wakiwa disqualified kwa madai kuwa hawana shughuli maalum za kujipatia kipato, wakati wanajuliksna na wakazi hizo sehemu wanazoishi kuwa wana shughuli maalum za kuwaingizia kipato.
Lakini hao wasimamizi wa uchaguzi wamelazimika kuyatenda hayo ikiwa ni "maagizzo" maalum baada ya kikao chao walichofanya pale Magogoni!
Tumeshuhudia pia wasimamizi wa uchaguzi wakiwaengua zaidi ya asilimia 90 ya wagombea wa vyama vya upinzani kuwa hawana sifa za kushiriki katika uchaguzi huo wakati wenzao wagombea wa CCM wakipitishwa kwa asilimia 100!
Baada ya vyama makini vya upinzani kutangaza kujitoa, tunamwona Waziri wa TAMISEMI, Suleiman Jafo, akitangaza kuyarejesha majina yote ya wagombea wa vyama vya upinzani yaliyokuwa yamekatwa awali!
Hivi katika mazingira ya aina hiyo bado tu nyinyi maccm mnaendelea tu kung'ang'ania tu ni lazima uchaguzi huo uenddlee kufanyika tarehe 24 mwezi huu?
Ni kwanini basi hamuwi waungwana wa kukiti kuwa ni nyinyi ndipo mliouvuruga uchaguzi huu, kwa hivyo muwaombe samahani wananchi wa nchi hii, kwa kadhia kubwa mliyoisababishia nchi hii na hivyo muahirishe uchaguzi huu hadi tarehe nyingine, ili uandaliwe upya chini ya Tume mpya ya uchaguzi itakayoridhiea na vyama vyote vya siasa.
Kwa kuendelea kuonyesha ubabe na ulevi wa madaraka na kuendelea na UCHAFUZI huu bila kuuahirisha, hakika nyinyi wanaccm mnalipeleka shimoni Taifa letu.
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa, umewavua nguo na hivi sasa mpo uchi wa mnyama
Kitendo cha hao wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada wa CCM kukata majina ya wagombea wa upinzani kwa sababu za kipuuzi kabisa, ambazo hata mtoto mdogo hawezi kuthubutu kuzifanya
Tumeshuhudia hao wasimamizi wa uchaguzi wakikata majina ya wagombea wa upinzani kuwa eti hawajui kusoma na kuandika, ambapo wengine ni diploma holders!
Tumeshuhudia pia wakidai kuwa baadhi ya wagombea wa upinzani wakiwa disqualified kwa madai kuwa hawana shughuli maalum za kujipatia kipato, wakati wanajuliksna na wakazi hizo sehemu wanazoishi kuwa wana shughuli maalum za kuwaingizia kipato.
Lakini hao wasimamizi wa uchaguzi wamelazimika kuyatenda hayo ikiwa ni "maagizzo" maalum baada ya kikao chao walichofanya pale Magogoni!
Tumeshuhudia pia wasimamizi wa uchaguzi wakiwaengua zaidi ya asilimia 90 ya wagombea wa vyama vya upinzani kuwa hawana sifa za kushiriki katika uchaguzi huo wakati wenzao wagombea wa CCM wakipitishwa kwa asilimia 100!
Baada ya vyama makini vya upinzani kutangaza kujitoa, tunamwona Waziri wa TAMISEMI, Suleiman Jafo, akitangaza kuyarejesha majina yote ya wagombea wa vyama vya upinzani yaliyokuwa yamekatwa awali!
Hivi katika mazingira ya aina hiyo bado tu nyinyi maccm mnaendelea tu kung'ang'ania tu ni lazima uchaguzi huo uenddlee kufanyika tarehe 24 mwezi huu?
Ni kwanini basi hamuwi waungwana wa kukiti kuwa ni nyinyi ndipo mliouvuruga uchaguzi huu, kwa hivyo muwaombe samahani wananchi wa nchi hii, kwa kadhia kubwa mliyoisababishia nchi hii na hivyo muahirishe uchaguzi huu hadi tarehe nyingine, ili uandaliwe upya chini ya Tume mpya ya uchaguzi itakayoridhiea na vyama vyote vya siasa.
Kwa kuendelea kuonyesha ubabe na ulevi wa madaraka na kuendelea na UCHAFUZI huu bila kuuahirisha, hakika nyinyi wanaccm mnalipeleka shimoni Taifa letu.