Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 18,881
- 29,382
Rais wa TLs Wakili Boniface Mwabukusi amesema Jiji la Mbeya linaonekana tofauti na majiji mengine nchini kutokana na shughuli nyingi za kijamii na kiuchumi kumalizika mapema usiku, kauli ambayo imezua mjadala miongoni mwa wakazi wa jiji hilo na watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Akizungumza katika mahojiano yaliyorushwa kutoka kupitia Mkataba ya Mawio Online TV, Mwabukusi alisema Mbeya ni miongoni mwa maeneo ambayo shughuli nyingi husitishwa mapema kiasi cha kufanya mitaa kuwa mitulivu mapema usiku.
“Mbeya ndiyo sehemu pekee panaitwa jiji lakini watu wote wanalala saa mbili kamili. Ukimkuta mtu anatembea ujue ni mlevi alipotea njia anajitahidi kurudi nyumbani,” alisema Mwabukusi.