Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,124
Wana CCM wajipanga 'kuikomboa' Moshi Mjini
Na Heckton Chuwa, Moshi
BAADHI ya wanachama wa CCM wanadaiwa kuunda timu maalumu ya siri ndani ya chama hicho, kijulikanacho kama Tuikomboe Kilimanjaro (TUKI), chenye nia ya kulikomboa jimbo la Moshi Mjini na kulinda yanayoshikiliwa na wabunge wa CCM.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka ndani ya chama hicho, hali hiyo imeleta hofu kubwa ndani ya chama hicho wakiwamo wabunge walioko madarakani sasa hivi.
Timu hii inadaiwa kujumuisha makada wenye majina katika medani ya siasa mkoani Kilimanjaro na ambao wajumbe halali wa kura za maoni ndani ya chama hicho katika wilaya zao.
Imeelezwa kujitokeza kwa kikundi hiki ambacho viongozi mbalimbali wa CCM wamesema hakina uhalali wowote umeanza kuleta chuki miongoni mwa wana CCM wakiwamo wakongwe wa siasa mkoani hapa.
Hata hivyo, uongozi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro na wa Moshi mjini, umekanusha kukijua au kuhusika na kikundi hicho.
Majimbo yanayodaiwa kulengwa na timu hiyo na majina ya wabunge wake kwenye mabano, ni Hai, (Fuya Kimbita); Vunjo (Aloyce Kimaro); Moshi Vijijini (Dkt. Cyril Chami); Rombo (Basil Mramba); Mwanga (Profesa Jumanne Maghembe) na Same Magharibi (Dkt. Mathayo David), Moshi Mjini (Bw.Philemon Ndesamburo) CHADEMA.
Majimbo ambayo yanaonekana kutolengwa na timu hiyo ni ya Siha la Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Bw. Aggrey Mwanri na Same Mashariki la Bibi Anne Kilango-Malecela, kwa madai kuwa wabunge wake wamejitahidi kutekeleza sera ya CCM kiasi cha wananchi kukosa sababu za kutowarudisha bungeni.
Uchunguzi uliofanywa na Majira umebaini kuwa kuna baadhi ya watu tayari wanatajwa kuwa wagombea katika baadhi ya majimbo.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, wahusika katika timu hiyo wamekuwa wakifuatilia kwa njia moja au nyingine, mienendo ya wabunge waliopo sasa wakiwamo wa CCM yenyewe kuangalia kama kazi walizofanya katika majimbo yao zinaweza kuwauza wakati wa kampeni zijazo.
Unajua hatutaki kupata matatizo ambayo tumeyapata mwaka 2000 na 2005 katika kuuza wagombea wetu, alisema kada wa CCM, ambaye alikiri kuwa mmoja wa wanatimu hiyo.
Alisema tayari wana ripoti za utekelezaji wa Ilani ya CCM ya wabunge wote wa chama hicho na kwamba ripoti hiyo itakuwa ndiyo dira yao kuamua wamrudishe mbunge mhusika au la, na pia kuwa wamekuwa pia wakifuatilia maoni ya wananchi wa jimbo husika.
Pamoja na timu hiyo kuonekana kulenga kukiimarisha chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2010, lakini baadhi ya wana CCM walisema kwa upande mwingine, huenda ikaleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho na hatimaye kuzaa makundi, jambo ambalo walisema linaweza hata kupunguza idadi ya majimbo ambayo CCM inayashikilia.
Ugonjwa huu wa makundi wakati wa uchaguzi mkuu mbalimbali ndiyo umeimaliza CCM hapa Moshi mjini na kuna hatari ya ugonjwa huu kuenea katika majimbo mengine mkoani hapa na hii ni hatari kwa chama chetu, alisema kada huyo.
Akizungumzia suala hilo hivi karibuni, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bibi Vicky Nsilo Swai, alisema CCM haina na wala haiundi vikundi vya namna hiyo.
"Uongozi wa CCM mkoa hauna habari na kikundi hicho na watu wa namna hiyo ni agents of confusion (wanatumika kuchanganya watu)," alisema.
Alisema chama mkoani humo kingependa kuwafahamu wale waliounda kikundi hicho na waeleze ni nani aliyewatuma kukianzisha na kwamba kama kuna mtu mwenye uchungu na CCM hana budi kushirikiana na uongozi wa chama hicho katika azma ya kukiendeleza.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Moshi Mjini, Bw. Godfery Mwangamilo, pia alikanusha kukifahamu kikundi hicho ambapo alisema CCM ina utaratibu wa kuteua wagombea na kwamba wakati ukifika ndio utakaotumika
Source.Majira.
NB: Upinzani mmejipanga vipi kuhakisha mmeongeza majimbo na kushikilia mliyo nayo? Mzee Ndesa hatutaki kusikia mafisadi wanalichukua hilo jimbo.Jimbo la Moshi mjini pamoja na kwamba mzee Ndesa amekua akiwekewa mtimanyongo na CCM ya huko lakini ameweza kabisa kulibadili lile jimbo.Natamani hii spirit kama ingekua kwa majimbo angalao 60 ya Tanzania.
Jimbo la Rombo CCM hata wasiahangaike ninarudi very soon kuongeza kasi ya mapambano,nimejiandaa vya kutosha.Hilo tumeshawapokonya.Na warudi baada ya miaka mitano waje waangalie maisha ya Warombo
Na Heckton Chuwa, Moshi
BAADHI ya wanachama wa CCM wanadaiwa kuunda timu maalumu ya siri ndani ya chama hicho, kijulikanacho kama Tuikomboe Kilimanjaro (TUKI), chenye nia ya kulikomboa jimbo la Moshi Mjini na kulinda yanayoshikiliwa na wabunge wa CCM.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika kutoka ndani ya chama hicho, hali hiyo imeleta hofu kubwa ndani ya chama hicho wakiwamo wabunge walioko madarakani sasa hivi.
Timu hii inadaiwa kujumuisha makada wenye majina katika medani ya siasa mkoani Kilimanjaro na ambao wajumbe halali wa kura za maoni ndani ya chama hicho katika wilaya zao.
Imeelezwa kujitokeza kwa kikundi hiki ambacho viongozi mbalimbali wa CCM wamesema hakina uhalali wowote umeanza kuleta chuki miongoni mwa wana CCM wakiwamo wakongwe wa siasa mkoani hapa.
Hata hivyo, uongozi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro na wa Moshi mjini, umekanusha kukijua au kuhusika na kikundi hicho.
Majimbo yanayodaiwa kulengwa na timu hiyo na majina ya wabunge wake kwenye mabano, ni Hai, (Fuya Kimbita); Vunjo (Aloyce Kimaro); Moshi Vijijini (Dkt. Cyril Chami); Rombo (Basil Mramba); Mwanga (Profesa Jumanne Maghembe) na Same Magharibi (Dkt. Mathayo David), Moshi Mjini (Bw.Philemon Ndesamburo) CHADEMA.
Majimbo ambayo yanaonekana kutolengwa na timu hiyo ni ya Siha la Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Bw. Aggrey Mwanri na Same Mashariki la Bibi Anne Kilango-Malecela, kwa madai kuwa wabunge wake wamejitahidi kutekeleza sera ya CCM kiasi cha wananchi kukosa sababu za kutowarudisha bungeni.
Uchunguzi uliofanywa na Majira umebaini kuwa kuna baadhi ya watu tayari wanatajwa kuwa wagombea katika baadhi ya majimbo.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, wahusika katika timu hiyo wamekuwa wakifuatilia kwa njia moja au nyingine, mienendo ya wabunge waliopo sasa wakiwamo wa CCM yenyewe kuangalia kama kazi walizofanya katika majimbo yao zinaweza kuwauza wakati wa kampeni zijazo.
Unajua hatutaki kupata matatizo ambayo tumeyapata mwaka 2000 na 2005 katika kuuza wagombea wetu, alisema kada wa CCM, ambaye alikiri kuwa mmoja wa wanatimu hiyo.
Alisema tayari wana ripoti za utekelezaji wa Ilani ya CCM ya wabunge wote wa chama hicho na kwamba ripoti hiyo itakuwa ndiyo dira yao kuamua wamrudishe mbunge mhusika au la, na pia kuwa wamekuwa pia wakifuatilia maoni ya wananchi wa jimbo husika.
Pamoja na timu hiyo kuonekana kulenga kukiimarisha chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2010, lakini baadhi ya wana CCM walisema kwa upande mwingine, huenda ikaleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho na hatimaye kuzaa makundi, jambo ambalo walisema linaweza hata kupunguza idadi ya majimbo ambayo CCM inayashikilia.
Ugonjwa huu wa makundi wakati wa uchaguzi mkuu mbalimbali ndiyo umeimaliza CCM hapa Moshi mjini na kuna hatari ya ugonjwa huu kuenea katika majimbo mengine mkoani hapa na hii ni hatari kwa chama chetu, alisema kada huyo.
Akizungumzia suala hilo hivi karibuni, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bibi Vicky Nsilo Swai, alisema CCM haina na wala haiundi vikundi vya namna hiyo.
"Uongozi wa CCM mkoa hauna habari na kikundi hicho na watu wa namna hiyo ni agents of confusion (wanatumika kuchanganya watu)," alisema.
Alisema chama mkoani humo kingependa kuwafahamu wale waliounda kikundi hicho na waeleze ni nani aliyewatuma kukianzisha na kwamba kama kuna mtu mwenye uchungu na CCM hana budi kushirikiana na uongozi wa chama hicho katika azma ya kukiendeleza.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Moshi Mjini, Bw. Godfery Mwangamilo, pia alikanusha kukifahamu kikundi hicho ambapo alisema CCM ina utaratibu wa kuteua wagombea na kwamba wakati ukifika ndio utakaotumika
Source.Majira.
NB: Upinzani mmejipanga vipi kuhakisha mmeongeza majimbo na kushikilia mliyo nayo? Mzee Ndesa hatutaki kusikia mafisadi wanalichukua hilo jimbo.Jimbo la Moshi mjini pamoja na kwamba mzee Ndesa amekua akiwekewa mtimanyongo na CCM ya huko lakini ameweza kabisa kulibadili lile jimbo.Natamani hii spirit kama ingekua kwa majimbo angalao 60 ya Tanzania.
Jimbo la Rombo CCM hata wasiahangaike ninarudi very soon kuongeza kasi ya mapambano,nimejiandaa vya kutosha.Hilo tumeshawapokonya.Na warudi baada ya miaka mitano waje waangalie maisha ya Warombo