KERO Masoko ya M'buyuni na Manyema ya Moshi Mjini hamna parking ya magari

KERO Masoko ya M'buyuni na Manyema ya Moshi Mjini hamna parking ya magari

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

backbenchers

Member
Joined
May 9, 2024
Posts
59
Reaction score
30
Katika pitapita zangu mjini hapa, nimegundua kuwa kuna kero moja inayofumbiwa macho na Manispaa ya Moshi Mjini, masoko ya hapa Moshi mjini, hususani soko la M'buyuni na Soko la Manyema, yana ufinyu au hayana kabisa maegesho ya wateja kuegesha magari yao ili wakapate huduma sokoni.

Kero hizi zinazidi kila siku kwasababu mbili kubwa:

1. Wafanyabiashara wadogowadogo kuweka bidhaa zao sehemu zilizotengwa kwa maegesho ya magari. Hii ipo sana kwenye soko la Manyema, kwenye soko la M'buyuni kuna barabara ya magari imefungwa kabisa na wafanyabiashara wadogowadogo ambayo haiwezi kupitika hata kwa pikipiki kirahisi.

2. Madereva wa bajaji hususani bajaji zinazoelekea eneo linaloitwa Shabaha kubadili eneo ya maegesho kuwa stendi bubu ya bajaji zao. Hii ipo sana kwenye soko la M'buyuni.

Swali langu nalielekeza kwa viongozi wa masoko ya M'buyuni na Manyema, mkurugenzi wa manispaa ya Moshi mjini, hvi jamani hii kero nyie hamuioni au labda kwenu nyie hii sio kero? Watu tutaegesha wapi magari yetu wakati wa.kwenda masokoni kama maeneo yakuegesha magari kumevamiwa na wafanyabiashara wadogowadogo na madereva wa bajaji?
 
Bajaji ni kama wamekuwa wenye mji kwa sasa.

Ndugu yangu siku hizi bajaji sio usafiri Tena, zimekuwa nimojawapo ya kero kubwa sana kwenye miji yetu, na ukizingatia inasemekana nyingi zinamilikiwa na mapolisi basi hata kusimamishwa wakat zikivunja sheria ni nadra sana, naadreva wengi wa bajaji hawajui sheria za barabarani, basi kerooo kupitiliza
 
Back
Top Bottom