Mgomo Baridi CHADEMA: Heche Kizingiti?

Mgomo Baridi CHADEMA: Heche Kizingiti?

Zack Abdul

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2026
Posts
505
Reaction score
487
#KURASA
Hivi karibuni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, waligomea kwenda mahakamani kusikiliza na kufuatilia kesi ya uhaini inayomkabili mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu.

Kukataa kwao kwenda mahakamani haikuwa bahati mbaya, ni kuanza kuweka mgomo baridi dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho John Heche, anayekabiliwa na tuhuma za wizi na ufisadi ikiwemo kukwapua pesa za michango ya tonetone.

"Katibu Mkuu, watu ni wachache huku" alisikika Tundu Lissu akiongea kuonesha masikitiko kutokana na wafuasi wa CHADEMA kususia kufika mahakamani.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinasema wana CHADEMA hao walisusia kwenda mahakamani ikiwa ni hatua ya kukerwa na tuhuma za ufisadi na wizi zinazomkabili John Heche wakitaka chama chao kichukie hatua stahiki dhidi yake huku hali halisi ikionekana chama hicho kutaka kumlinda.

Jambo hili CHADEMA na Heche wanatakiwa kujifunza kwani linaonekana wazi linaenda kuleta tafrani kubwa katika chama hicho, kwani panapofuka moshi tambua moto unakuja, ngo
IMG-20260723-WA0033.jpg
ja tuone.
 
Umeandika hadithi ya kusadikika, hakuna solid evidence hata moja ya huo mgomo unaouzungumzia hapa.

Unalazimisha dhoruba kwenye kikombe cha chai, CHADEMA ipo imara sana.
 
Sasa Heche akikubali kutoa namba zake binafsi Ili wananchi wamchangie hela vizuri,nyie mbogamboga mtajinyonga kabisa.
 
wakaenda mpaka kukasafisha meno lakini wapiiiiiii, eti sasahivi nacho kinapora hadi wake za watu. Ingekua mie ndio mwenye mke nakafumania na nakala tigo wala hamna kitu katafanya kashenzi kabisa.
Kapuuzi sana hako kajamaa..
Halafu bado kana ule ushamba wa kijijini..
 
#KURASA
Hivi karibuni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, waligomea kwenda mahakamani kusikiliza na kufuatilia kesi ya uhaini inayomkabili mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu.

Kukataa kwao kwenda mahakamani haikuwa bahati mbaya, ni kuanza kuweka mgomo baridi dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho John Heche, anayekabiliwa na tuhuma za wizi na ufisadi ikiwemo kukwapua pesa za michango ya tonetone.

"Katibu Mkuu, watu ni wachache huku" alisikika Tundu Lissu akiongea kuonesha masikitiko kutokana na wafuasi wa CHADEMA kususia kufika mahakamani.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinasema wana CHADEMA hao walisusia kwenda mahakamani ikiwa ni hatua ya kukerwa na tuhuma za ufisadi na wizi zinazomkabili John Heche wakitaka chama chao kichukie hatua stahiki dhidi yake huku hali halisi ikionekana chama hicho kutaka kumlinda.

Jambo hili CHADEMA na Heche wanatakiwa kujifunza kwani linaonekana wazi linaenda kuleta tafrani kubwa katika chama hicho, kwani panapofuka moshi tambua moto unakuja, ngoView attachment 3635381ja tuone.
Achana na CHADEMA wewe au una ugonjwa wa akili. Jali familia yako inapataje Elimu Bora na Afya Bora achana na akina Lema.
 
Acha uongo kesi ya Lissu ipo mahakama ya Rufaa. Kesi ya Sasa sio ya uhaini.
 
Back
Top Bottom