I am Groot
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,734
- 10,041
Walter Elias Disney
Alihamia California mapema miaka ya 1920 na kufungua studio yake 'Disney Brothers studio' kwa kushirikiana na kaka yake aliyeitwa Roy. Mwaka 1928 alitengeneza character wake wa kwanza aliyempa jina la Mickey Mouse, na ndiye aliyempa mafanikio ya mwanzoni. Kadri studio ilivyoendelea kukua, teknolojia pia iliendelea kuimarika, alianza kuboresha kazi yake kwa kuongezea sauti na rangi kwenye katuni alizokuwa akizitengeneza.
Disney anashikilia rekodi ya kushinda tuzo 22 za Oscar kutoka nomination 59, golden global 2, Emmy Awards na nyinginezo nyingi.
Matokeo ya maendeleo ya teknolojia ya animation ilipozidi kukua alitambulisha zake za mwanzo zenye
ubora kama;
Snow white and the seven dwarfs (1937)
Pinocchio na Fantasia (1940)
Dumbo (1941)
Bambi (1942)
Cinderella (1950) na Mary Poppins (1964) zilizompatia tuzo ya Academic Award.
Disney alikuwa mtu wa aibu na mwenye kupenda utulivu. Pamoja na hayo alikuwa ni mvutaji mkubwa wa sigara na inasemekana ndicho kilicho sababisha umauti wake baada ya kugundulika na kansa ya mapafu. Alikufa mwaka 1966.
Amebaki kama alama muhimu katika historia ya animation.Kazi zake za filamu zimeendelea kuonyeshwa, na katika jina lake studio na kampuni zake zimeendelea kusimamia ubora wa hali ya juu katika bidhaa zake hasa zijulikanazo entertainment, Disney park zake pia zimeendelea kukua kiukubwa na wingi wa namba za watembeleaji katika nchi kadhaa alizojiwekeza.