Waliomdharau Zitto sasa awafunga midomo


Kweli wewe ni Mcha-Mbuzi... Ulitaka Zitto aunganishe nguvu kwa style ipi?
 
Yule mama angegombea ubunge angepita sema ZZK alimcheze mchezo kwa kutumia prof.Mkumbo alafu mama akochomekewa gafla.
Kashindwa kupita Lowassa kwenye urais sembuse huyu dada.
 
Kawasaidia ccm kwa kugawa kura hata wagombea wake wameshindwa loh
.

Alosaidia CCM ni mbowe na Mtei kumkaribisha Lowassa Chadema,Angalia sasa wabongo wanavyoiadhibu UKAWA.Wao walidhani EL ataleta ushindi kumbe kaleta vilio.Zito ni wa kumsifu,chama kipya kimeshinda vyama vikongwe.Ukweli wenyewe ni kuwa wanachadema lazima muelewe mbowe na mtei ndio wanaua chama.Chadema ilikuwa na nafasi mzuri ya kushinda uchaguzi huu lakini walianza kula nyama ya watu kwa kumfukuza Zito mara Slaa huyooo kaingia mtini ingawa na yeye alikuwa mstari wa mbele kumfukuza Zito.Tundu Lissu mnafiki mkubwa chupuchupu huko singida,Mbowe sijui huko hai kama kapona.Hili ni fundisho kuwa katika siasa unafiki sio mzuri leo hii nani ndani ya chadema atazuia chozi la Halima Mdee?.
Angalia watu wanaoona mbele kama Slaa na Prof Lipumba.Je na wao leo wangejificha wapi?
ZIIIIIIIIIIIITOOOOOO Nakupongeza sana na pongezi zaidi kwa mwalimu wako pale chuo keep on man:A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Mkuu kwani Lowassa kapata nini? Mafuriko?
 

Wao walishindwa nini kumuunga mkono yeye Kigoma mjini mpaka yeye awaunge mkono? ACT waliandika barua kutaka kujiunga UKAWA, hawakujibiwa!
 
Bavicha bana sasa Zitto kagawa kura vipi wakati Lowassa alikuwa na mafuriko.
 

Nahisi atajifunza kutokana na makosa maana vinginevyo atajimaliza kisiasa
 

Be analytical my friend. Umri wa ACT ni miezi kadhaa tuuu. Bado wameweza kujitutumua na kupata kiti kimoja. Na hata mgombea wao anaweza kuwa watatu katika kinyang'anyiro. Hii ni achievement kubwa. Mbona watu wako wa Chadema wa wana miaka 23 bado wameomba boost ya Lowassa ili wapate hush???
 

Zito ni jiwe walilolikataa waashi.
 
Ukweli Lazima usemwe tu katika siasa kila mtu anafanya ajualo ili apate Nafasi Yake, wale walio kosa kwa tkt ya ACT bado wana Nafasi kubwa ndani ya chama na chama bado ni kichanga sana hata kama wange ende vyama vingine bado wangekosa tu
 
Hongera Sana Zitto Z. Kabwe... Umetimiza Ndoto Zako..
Hongera Sana Sana Mama Anna E. Mghwira, Umefanikisha Kukitangaza Chama Vizuri...
ACT Wazalendo Daima
 
kina kafulila wakaanza kujiona keki,,,sasa hivi ataisoma
 
kina kafulila wakaanza kujiona keki,,,sasa hivi ataisoma,,escrow,escrow my feet
 
Kusimamisha wagombea ubunge zaidi ya 250 halafu unapata mmoja tu. 1/250.
Halafu eti unakuja kushangilia kwakusuta huku unainuainua sketi mbele ya wanaume ambao wao wameongeza wabunge wengi zaidi ya waliopoteza.

Slogan ya WAHA

UBISHI IS OUR MOTO.
 
Kati ya watu wakusikitika kutorudi bungeni ni Kafulila naomba tisimuseme vibaya hakika huyu ni mzalendo wa kweli
 

Pole sana.
 

Mtu akijitahidi apewe pongezi.ACT hakina miezi 18 tangu kianzishwe.Kina mbunge wakati kuna vyama vilianzishwa tangu 1992 nikiwa Standard 1 havijawahi kuwa hata na mwenyekiti wa mtaa.
 
Keep going Zitto. . . ..

Mwenye uwezo anao tu. . . .Chama kipya kimejitangaza vizuri sana; ndani ya miaka miwili tu habari yake itakuwa nyingine kabisaa

Kazi nzuri sana ACT ni suala la muda tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…