Kijan mwenzangu pole Sana .Wakuu naombeni mnisaidie mawazo, maana kuna kipindi mtu unakua kwenye wakati mgumu mpaka unaona kila uamuzi unaoufanya hauko sahihi. Wakuu hapa nilipo nina mke na tuna watoto wawili.
Mwaka 2017 niligundua kua kuna jamaa anatoka na mke wangu, nilipopata taarifa nilijaribu kumuuliza mke wangu kwa kuongea nae taratibu tena kwa busara kabisa ili nipate ukweli kuhusu jambo hilo ila matokeo yake alikuja juu sana na kutishia kua angekunywa Sumu kwa sababu namsingizia mambo ambayo hajayafanya.
Baada ya hali ile kutokea sikuendeleza mjadala ila nikamwambia kama hili jambo lina ukweli basi aache maana litatuharibia familia na huyo bwana anaemdanganya hana malengo yoyote mazuri na yeye zaidi ya kumharibia tu maisha kisha anapotea.
Wakati yote hayo yanaendelea mimi nilikua kazini. Na kazi yenyewe haikua na makazi maalumu. Tulikua tunahamishwa sehemu mbalimbali kulingana na project zinazokuepo. Ila nikiwa mbali nilikua najitahidi kufika nyumbani mara kwa mara, na pia nilimwambia awe huru wakati wowote atakapojisikia kuja nilipo, nimkatie tiketi awe anakuja.
September 2018 nikawa nimefika home ghafla nilipofika nikaingia ndani sijakaa hata dk 5 simu yake ikaita, ilikua sebuleni nikaichukua kuangalia namba nikakuta ni yule jamaa ndo kapiga, nikampa mtoto simu nikamwambia ampelekee mama alikua kwenye ofisi zake hapo hapo nyumbani, sikufuatilia walichoongea.
Kuanzia hapo nikawa namfuatilia na nikagundua kuwa tofauti na huyo Jamaa bado ana mahusiano na jamaa wengine wawili, usiku wake nikambana akanieleza ukweli ni kwamba alikua na mahusiano nao ila ameachana nao tayari. Ila nilichobaini si kweli kua ameachana nao maana nilipokua nafuatilia nilikuta mawasiliano bado yapo japo kila napomuuliza anajitetea sana.
Nilimchukua tukaenda kupima VVU nikakuta Mwenyezi Mungu alimnusuru yupo Safi. Baada ya hapo tukaendelea hivyo hivyo na baadae akapata ujauzito, ila kwa kipindi chote hiki alikua anaficha kweli simu yake, akija ndani anaiacha ofisini na usiku akilala anaizima.
Ila wakati mimba ina miezi 7 nikakuta msg ya yule jamaa wa mwanzo kabisa, akimtaka wakutane, nilimhoji tena huyu mwanamama lakini hakunipa jibu la kueleweka.
Baadae alijifungua salama, sema kwa bahati mbaya au nzuri mtoto ametoka copy ya mama yake, kwa kipindi cha uzazi sikuona mawasiliano yakiendelea. Ila sasa hivi mtoto ana miezi mitano na nimekuta mawasiliano yameanza tena.
Kwa hayo machache wakuu naomba mnisaidie mawazo yenu, maana binafsi bado sijaamua chochote. Na kama kuna swali mniulize tu maana nimejitahidi kufupisha.
Wewe bado ni kinda humu J.f umejiunga juzi tuu! Nakutaarifu tu wanaume wa humu tunachefuka sana na nyuzi km hizi,kuwa makini utapigwa Ban ya maisha.
Thats my girl, i really love your way of seeing things, AS THEY ARE , not AS WE WISH THEM TO BE, hongera sana dada yanguUkiona mwanamke anakusaliti ujue hupendwi,kama hupendwi unabaki kufanya nini?
Huwa sitoi msamaha kwa msaliti hata siku moja!
Hebu achana na huyo kiwembe asee
Thats my girl, i really love your way of seeing things, AS THEY ARE , not AS WE WISH THEM TO BE, hongera sana dada yangu
asante pia, tell them to serve you with cappuccinno , i am caming to foot the bill my sister. unashangaa mwanaume mzima analeta story kaa hii hapa, yaani mtu uko na 100% evidence that she is cheating on you, and yet you came here asking for advice????? dunia kuna mambo
Umenena vyema mkuu, shida hapo sio jamaa kumuacha huyo mama, shida hapo ni uwekezaji alioufanya na mwanamke, pengine jamaa alikuwa ameweka future yake yote kwa mkewe. Lakini jingine maisha yake na ya watoto baada ya kuachana na mkewe kinampa shida sana au pengine kapenda deadly. Who knows ndoa ni taasisi complicated sana.Jamani mambo ya ndoa magumu sana inaonesha umewekeza sana kwa mkeo na yeye kulitambua hilo pia hilo ni tatizo
asante pia, tell them to serve you with cappuccinno , i am caming to foot the bill my sister. unashangaa mwanaume mzima analeta story kaa hii hapa, yaani mtu uko na 100% evidence that she is cheating on you, and yet you came here asking for advice????? dunia kuna mambo
Ukiona bomba limetoboka na watu wanachota maji. Usianze kugombana na wanaochota maji kwasababu ni wengi na hutawaweza. Utawapiga hawa, kesho wanakuja wengine. Unachotakiwa ni kuziba bomba ili wanaochota maji wasichote. Maana yakeUwezekano ni mkubwa tu kuwa mtoto siyo wa kwangu, ila kwa vile yupo kwenye himaya yangu, na mtoto hana hatia yoyote nitamtunza na kumpatia mahitaji yote ya msingi. Ila wa kushughulika nao ni mama pamoja na wakora zake.
Nishawaza sana kumfanyia jamaa undava ila side effect zake pia zinaeza zikanicost na kuniongezea matatizo badala ya kutatua. Ndo maana nikajitahidi kuwa kimya kwa muda japo naumia ili niangalie uwezekano wa kulitatua bila Mimi kuathirika zaidi ya hapa
AMINA MKUUEeeh Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema.Naomba uninyime moyo wa upendo kama huu.
Better late than neverKingsmann,
Nashukuru kwa ushauri mkuu, kuna kipindi niliwaza hivyo ila hata nisiposhiriki nae INA maana ndo itakua hivyo for the rest of my life??
Because I am 30 now. Maana naona kurudishwa nyuma sana, maana nimejenga akiwepo na kuna miradi nimefanya akiwepo na nikampa yeye kuisimamia kutokana na Mimi kuwepo kwa mkaburu. Na pia gharama/muda wa kuanzisha Familia nyingine tena. Maana hapa Future siioni