Wakuu naombeni mnisaidie mawazo, maana kuna kipindi mtu unakua kwenye wakati mgumu mpaka unaona kila uamuzi unaoufanya hauko sahihi. Wakuu hapa nilipo nina mke na tuna watoto wawili.
Mwaka 2017 niligundua kua kuna jamaa anatoka na mke wangu, nilipopata taarifa nilijaribu kumuuliza mke wangu kwa kuongea nae taratibu tena kwa busara kabisa ili nipate ukweli kuhusu jambo hilo ila matokeo yake alikuja juu sana na kutishia kua angekunywa Sumu kwa sababu namsingizia mambo ambayo hajayafanya.
Baada ya hali ile kutokea sikuendeleza mjadala ila nikamwambia kama hili jambo lina ukweli basi aache maana litatuharibia familia na huyo bwana anaemdanganya hana malengo yoyote mazuri na yeye zaidi ya kumharibia tu maisha kisha anapotea.
Wakati yote hayo yanaendelea mimi nilikua kazini. Na kazi yenyewe haikua na makazi maalumu. Tulikua tunahamishwa sehemu mbalimbali kulingana na project zinazokuepo. Ila nikiwa mbali nilikua najitahidi kufika nyumbani mara kwa mara, na pia nilimwambia awe huru wakati wowote atakapojisikia kuja nilipo, nimkatie tiketi awe anakuja.
September 2018 nikawa nimefika home ghafla nilipofika nikaingia ndani sijakaa hata dk 5 simu yake ikaita, ilikua sebuleni nikaichukua kuangalia namba nikakuta ni yule jamaa ndo kapiga, nikampa mtoto simu nikamwambia ampelekee mama alikua kwenye ofisi zake hapo hapo nyumbani, sikufuatilia walichoongea.
Kuanzia hapo nikawa namfuatilia na nikagundua kuwa tofauti na huyo Jamaa bado ana mahusiano na jamaa wengine wawili, usiku wake nikambana akanieleza ukweli ni kwamba alikua na mahusiano nao ila ameachana nao tayari. Ila nilichobaini si kweli kua ameachana nao maana nilipokua nafuatilia nilikuta mawasiliano bado yapo japo kila napomuuliza anajitetea sana.
Nilimchukua tukaenda kupima VVU nikakuta Mwenyezi Mungu alimnusuru yupo Safi. Baada ya hapo tukaendelea hivyo hivyo na baadae akapata ujauzito, ila kwa kipindi chote hiki alikua anaficha kweli simu yake, akija ndani anaiacha ofisini na usiku akilala anaizima.
Ila wakati mimba ina miezi 7 nikakuta msg ya yule jamaa wa mwanzo kabisa, akimtaka wakutane, nilimhoji tena huyu mwanamama lakini hakunipa jibu la kueleweka.
Baadae alijifungua salama, sema kwa bahati mbaya au nzuri mtoto ametoka copy ya mama yake, kwa kipindi cha uzazi sikuona mawasiliano yakiendelea. Ila sasa hivi mtoto ana miezi mitano na nimekuta mawasiliano yameanza tena.
Kwa hayo machache wakuu naomba mnisaidie mawazo yenu, maana binafsi bado sijaamua chochote. Na kama kuna swali mniulize tu maana nimejitahidi kufupisha.
Mwaka 2017 niligundua kua kuna jamaa anatoka na mke wangu, nilipopata taarifa nilijaribu kumuuliza mke wangu kwa kuongea nae taratibu tena kwa busara kabisa ili nipate ukweli kuhusu jambo hilo ila matokeo yake alikuja juu sana na kutishia kua angekunywa Sumu kwa sababu namsingizia mambo ambayo hajayafanya.
Baada ya hali ile kutokea sikuendeleza mjadala ila nikamwambia kama hili jambo lina ukweli basi aache maana litatuharibia familia na huyo bwana anaemdanganya hana malengo yoyote mazuri na yeye zaidi ya kumharibia tu maisha kisha anapotea.
Wakati yote hayo yanaendelea mimi nilikua kazini. Na kazi yenyewe haikua na makazi maalumu. Tulikua tunahamishwa sehemu mbalimbali kulingana na project zinazokuepo. Ila nikiwa mbali nilikua najitahidi kufika nyumbani mara kwa mara, na pia nilimwambia awe huru wakati wowote atakapojisikia kuja nilipo, nimkatie tiketi awe anakuja.
September 2018 nikawa nimefika home ghafla nilipofika nikaingia ndani sijakaa hata dk 5 simu yake ikaita, ilikua sebuleni nikaichukua kuangalia namba nikakuta ni yule jamaa ndo kapiga, nikampa mtoto simu nikamwambia ampelekee mama alikua kwenye ofisi zake hapo hapo nyumbani, sikufuatilia walichoongea.
Kuanzia hapo nikawa namfuatilia na nikagundua kuwa tofauti na huyo Jamaa bado ana mahusiano na jamaa wengine wawili, usiku wake nikambana akanieleza ukweli ni kwamba alikua na mahusiano nao ila ameachana nao tayari. Ila nilichobaini si kweli kua ameachana nao maana nilipokua nafuatilia nilikuta mawasiliano bado yapo japo kila napomuuliza anajitetea sana.
Nilimchukua tukaenda kupima VVU nikakuta Mwenyezi Mungu alimnusuru yupo Safi. Baada ya hapo tukaendelea hivyo hivyo na baadae akapata ujauzito, ila kwa kipindi chote hiki alikua anaficha kweli simu yake, akija ndani anaiacha ofisini na usiku akilala anaizima.
Ila wakati mimba ina miezi 7 nikakuta msg ya yule jamaa wa mwanzo kabisa, akimtaka wakutane, nilimhoji tena huyu mwanamama lakini hakunipa jibu la kueleweka.
Baadae alijifungua salama, sema kwa bahati mbaya au nzuri mtoto ametoka copy ya mama yake, kwa kipindi cha uzazi sikuona mawasiliano yakiendelea. Ila sasa hivi mtoto ana miezi mitano na nimekuta mawasiliano yameanza tena.
Kwa hayo machache wakuu naomba mnisaidie mawazo yenu, maana binafsi bado sijaamua chochote. Na kama kuna swali mniulize tu maana nimejitahidi kufupisha.