uko sahihi na Yesu hakuwahi kujiita Mkristo, hilo neno Mkristo lilikuja baadaye kabisaa⦠na Kwa mara ya kwanza, wanafunzi wa Yesu waliitwa Wakristo huko Antiokia ukisoma katika (Matendo 11:26), miaka kadhaa baada ya kifo na ufufuko wa Yesu. Hii ilikuwa kama njia ya kuwatofautisha wafuasi wake na Wayahudi wengine., nadhani ukiwa msomaji mzuri wa biblia utayaoata mengi huko
Kwa hiyo, Ukristo ni harakati au njia ya maisha iliyoanzishwa na Yesu,lakini jina Ukristo lilitolewa baada ya yeye kuondoka duniani. Ni wafuasi wake waliomfuata wakaitwa Wakristo kwa sababu waliishi kama Kristo kwa kuyafata matendo yake na kumkubali kuwa Beana namwokozi wa maisha yao, hivyo neno ukristo kwetu ni utambulisho wa kututifautishwa na wasiomuamini, ndio maana ata nyinyi hamjakosa jina la kutuita mnatuita hawa wakristo wajinga e.t.c
All in all Yesu hakuwa Mkristo, alikuwa Myahudi, Ukristo ulianzia kwake kupitia mafundisho, kifo na ufufuo wake.
Wakristo ni wale wanaoishi kwa mafundisho ya Yesu Kristo.
Kwa hiyo, kumuhusisha Yesu na Ukristo si kwa sababu alikua Mkristo, bali kwa sababu yeye ndiye msingi wa Ukristo.
Hope i made it clearš