Wahenga tujuane hapa..

Wahenga tujuane hapa..

Niliwahi kuokota kitita cha shilingi elfu moja na mia tano.. aisee, pale nyumbani tulitrend hadi watu wakaanza kudhani sisi ni wafujaji wa mali za umma
Mwaka 1993 tukiwa na rafiki yangu siku ya Christmas tukamuibia binti wa watu shilingi 100 ili tukanywe soda na biscuits, ile kesi ilifika home nikapewa dawa yangu ya uhakika.
 
Niliwahi kuokota kitita cha shilingi elfu moja na mia tano.. aisee, pale nyumbani tulitrend hadi watu wakaanza kudhani sisi ni watakatishaji wa fedha za umma
Nilimwibia marehemu bibi sh 2000 nilikula wiki nzima na haikuisha nikanunua na saa 😂😂😂

Mwaka 1996 hiyo std 2 mpaka nilikamatwa hela nilikuwa naficha kwenye majani ya viazi vitamu shambani nyuma ya nyumba
 
Ni kweli uliukuta huo wimbo ila huna huo uhenga. Tuliimba kwa wivu mkubwa sana.
Mwaka kati ya 1982 au 1983 hilo shairi lilitoka kwenye mtihani wa darasa la saba sambamba na usemi wa "majuto ni mjukuu"
Wanyakyusa huko kwao kuna ndege aliendana na hizo rangi zote, kwa hiyo jibu likawa ni ndege KISUPE.
Swali la "majuto ni mjukuu" walimalizia wa MWAISUMO maana alikuwepo kijana anaitwa Majuto kwenye ukoo huo.
 
Mkuu ntadondosha chozi.. yalifanyika mambo makubwa ambayo kwa sasa huwezi kuitaja hata elfu kumi kwenye mambo yale
Hahaa.

Unanikumbusha kuna mshua alinunua viwanja kama 15 vya laki laki mwaka 1991.

Tukawa tunamshangaa, wewe mshua mbona unanunua viwanja huku mbali sana na mjini?

Vile viwanja sasa hivi bila milioni 100 kila kimoja hugusi.
 
Nakumbuka soda yangu ya kwanza kunywa naenda kununua dukani mwenyewe ilikuwa fahari kama sijakosea
Kijijini soda tulikuwa tunazipeleka long (kisima) zipate baridi 😅😅😅 makreti yalikuwa ya mbao na chupa zilikuwa na shape mbayaaa , sh 30 tu lakini kuipata sasa hiyo hela mpaka atoke mgeni mjini.

Kuna Marehemu Baba mdogo alikuwa kiwanda cha Williamson Diamond akija alikuwa anatugawia noti za sh 50 tukanywe soda
 
Back
Top Bottom