JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Wananchi wa Kijiji cha Sunuka, Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma wameshirikiana na Serikali ya Kijiji kuchukua Waganga wa Jadi zaidi ya 10 kutoka Sumbawanga ili kukagua wachawi waliomo ndani ya kijiji chao wakidai ndicho chanzo cha utitiri wa vifo vya vijana katika mazingira ya kutatanisha.
Baadhi wa Wananchi walikusanyika na kuandama barabarani wakiimba “Tumechoka na uchawi” huku wakisapoti kile kinachofanywa na Viongozi wao.
Hata hivyo operesheni hiyo imepingwa vikali na Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Dinah Mathamani ambaye amezuiwa kuingia kijijini hapo ikiwa yupo kinyume cha mpango huo.
DC Dinah Mathamani amesema “Tumejadili na viongozi kuhusu suala hili, wale wanaojiita Waganda wanatakiwa kuondoka katika wilaya yetu, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na viongozi wanaoshirikiana nao.
Chanzo: UFM