Wafahamu nyoka hatari Zaidi duniani

Wafahamu nyoka hatari Zaidi duniani

Hakuna nyoka anayekimbiza watu huyo nyoka hayupo duniani labda kwa baadae nyoka wa aina hio atokee .

Mamba kama walivyo nyoka wengine hawapendi usumbufu wakiona unafanya approach kuwasogelea hujiondokea zao

Nyoka mbaya na hatari ni yule hujamuona ukapita jirani yake hapo atafanya striking kama defensive mechanism ila kuhusu kukimbiza hayupo nyoka wa aina hio duniani.
Hapana ninakukatalia....mamba anakimbiza hata gari sembuse binadamu...it is the most aggressive snake of all
 
Nyoka makengeza, huyu akikuuma chini unavimba juu. Yeye huuma zaidi wakati wa giza. Maranyingi haonekani hadharani, na hupendelea kuuma zaidi watu wa jinsia ya K. Nyoka huyu yupo kila mahari duniani na hupendwa na kila mwanamke kwa style yake ya uumaji. Sumu yake inasemekana akiuma maramoja huweza kudhuru hadi wanawake billioni moja. Na hutoa sumu kati ya mills, 150 hadi 200.hana macho ila ana mdomo tu
Anapendwa na wanawake kivipi mkuu? Ama ana hela na sikisi paki?
 
Niliwahi kuskia nyoka wakigombana na mmoja kuuwawa! Mwenzie anakwenda kuchuma dawa na kumuekea mwenzie..kama binadamu utafanikiwa kuiona dawa basi ni dawa nzuri mno kwa mtu alie umwa na nyoka ..ila nyoka akikuona akiwa anachuma umekwisha..
Duu
kwa iyo uyo alie uwawa akiwekewa dawa anafufuka?
 
mqdefault.jpg

Mfalme wa pori mwenyewe kanyoosha na kawa mweusi,wakati koboko mwenyewe bado mdogo tu.
 
Hakuna nyoka anayekimbiza watu huyo nyoka hayupo duniani labda kwa baadae nyoka wa aina hio atokee .

Mamba kama walivyo nyoka wengine hawapendi usumbufu wakiona unafanya approach kuwasogelea hujiondokea zao

Nyoka mbaya na hatari ni yule hujamuona ukapita jirani yake hapo atafanya striking kama defensive mechanism ila kuhusu kukimbiza hayupo nyoka wa aina hio duniani.
Acha kudanganya watu mkuu. Mimi mwenyewe ni shuuda
 
downloadfile-2.jpg

Huyu taipan ninaweza kukaa nae nyumba moja,hata kama anasumu kali lakini siyo mkorofi amezubaa sana wala hana kasi ya mashambulizi.
 
Mimi binafsi mwaka 1994 nilikuwa naelekea Bujiumbura nilipofika katikati ya Bwanga na Runazi (wakati huo naendesha lori la mizigo)nikaona kitu kimekaa barabarani kwa mbali mimi nikafikiria ni ni fito ndeefu imetupwa barabarani,kumbe koboko bhana,kumkaribia akasimama huku amepanua mdomo wake mweusii toba.nikafunga vioo vyote nikajua nimemkanyaga kufika Runazi mwenzangu aliyekuwa nyuma alipofika nikamuuliza kama ameona mzoga wa koboko akasema hajaona chochote.
Dah.. mkuu kitambo sana. Enzi hizo mimi hata dunia sijaiona bado, wewe teyari upo kazini?
 
Dah.. mkuu kitambo sana. Enzi hizo mimi hata dunia sijaiona bado, wewe teyari upo kazini?
Ulikuwa ni mwaka wa balaa,sintousahau, kufika Burundi tu,tukasikia raisi wa Burundi na Rwanda wamepata ajali ya ndege(kumbe walitunguliwa)na wamefariki ndipo mauwaji makubwa yakatokea huko Rwanda.lakini kwangu ulikuwa mwaka wa 'koboko' mkubwa kabisa kuwahi kumuona.
 
Back
Top Bottom