Cha kufanya baada ya kupokea last warning kutoka kwa muheshimiwa Blackmamba, kumbuka wakati huu mtakuwa mmetenganishwa umbali wa either mita mbili au tatu..Kwa kuongezea tu, black mamba ni nyoka mtulivu sana ila ukimchokoza ndio utaona balaa lake!!
Kabla hajakushambua atakupa warning kwa kujikunja na kufungua kinywa chake chenye rangi nyeusi, ukiendelea kumsumbua baada ya hiyo warnng kinachofwata hapo ni kifo chako!!
Ukifika hatua hiyo jua una choices mbili tu either umshambulie afe tena bila kumkosa, au ukimkosa basi jua shambulio lake ni moja tu na baada ya hapo unadakika 20 za kusali na kuandika wosia kabla hujafa!!
1- Usithubutu kuinama kuokota chochote kwa lengo la kumshambulia.
2- Kama unafimbo na hunahakika na shambulio lako endelea kujikausha huku ukiomba sana dua.
3- Huku ukimuangalia kwa makini kwa utulivu kabisa rudi nyuma taratibu kuongeza umbali baina yako na muheshimiwa.
Ukionesha nidhamu kwa hatua hizo tatu juu, unaweza kutoka salama..!!! hapo sasa nenda dukani, kanunue soda baridi sana uipendayo na ujipooze maana mpaka kufikia hapo utakuwa umesweat vya kutosha sana!!!
