Trainee
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 2,219
- 2,825
Assalaamu àlaykum wa rahmatullaahi wa barakaatuh
Kuna watu wakiona heading kama hiyo tayari astaghfirullaah zinakuwa nyingi wakidhani labda nimepotosha. Twende pamoja kwa ufupi sana utanielewa
Kalenda wanayotumia waislamu (si kwamba mimi siyo mwislamu bali mimi na wenzangu baadhi tunaitumia ikikaribia ramadhan na ikikaribia arafa) ni kalenda ya kuhesabu siku kwa kutumia mzunguko wa mwezi mwandamo ambayo wengine wanaiita lunar calendar
Kwa mujibu wa kalenda hiyo miezi ni 12 katika mwaka na mwezi unakuwa na siku 30 au 29 basi! Nyongeza ya hilo mwaka unakuwa na siku 360 tu hazizidi.
Muḥarram (mfunguo nne)
Ṣafar (mfunguo tano)
Rabial-Awwal (mfunguo sita)
Rabial-Thāni (mfunguo saba)
Jamādal-Awwal (mfunguo nane)
Jumādal-Thāni (mfunguo tisa)
Rajab
Shaʿbān
Ramaḍhān
Shawwāl (mfunguo mosi)
Dhul-Qaʿadah (mfunguo pili)
Dhul-Ḥijjah (mfunguo tatu)
Miezi hiyo kwa Kiswahili wanaita mifunguo ambapo waswahili wanahesabu kama warabu yaani mwezi wa kwanza ni Shawwāl na wa mwisho ni Ramadhani (Kwahiyo kwa mujibu wa waswahili na waarabu ile siku ya idi baada ya ramadhan (idi ndogo) ndiyo siku ya kwanza ya mwaka yaani mwaka mpya. Kwa upande wa uislamu mwezi wa kwanza ni Muharram na wa mwisho ni Dhul Hijja (Kwahiyo ukiona mahujaji wanaenda makka vile ujue ndo tupo mwisho Mwisho wa mwaka)
Kama ilivyo kawaida mitume hawakuwa wakiondoa kila kitu tu walichokikuta bali kuna vingine waliamrishwa kuviendeleza na kuvienzi kama vilivyo ila kwa namna nzuri inayofuata sheria ya mwenyezi Mungu. Basi hata miezi Waarabu walikuwa wakiiheshimu ni minne na wakawa wanafanya ibada zao za tofauti ndipo mtume alivyokuja akaendeleza utukufu wa miezi ile kama ilivyokuwa ila kwa utaratibu wa Mwenyezi Mungu
Miezi hiyo Mitukufu ni
Dhul Qa'ada (Mfunguo pili)
Dhul Hijja (Mfunguo tatu)
Muharram (mfunguo nne)
Rajab
Ramadhan haimo!
Sikuachi hivi hivi ngoja nimwambie kwa nini watu wamezoea ramadhani ni mwezi mtukufu?
Ndani ya ramadhani kuna usiku mmoja tu (sehemu ya siku miongoni mwa siku za ramaḍhān wala si mwezi mzima wala si siku nzima) ambao usiku huo umetajwa kuwa ni bora kuliko miezi elfu. Maana yake ni kwamba mtu akifanya mema kwenye usiku huo itahesabika kama amefanya mema kwa miezi zaidi ya elfu. Vivyo hivyo kwa atakaye fanya maovu usiku huo ni sawa na aliyetumia miezi zaidi ya elfu kumuasi Mola.
Tunapata kwamba ni usiku mmoja tu ulio bora sana na hata hivyo haujaambiwa ni usiku mtukufu! Pia mwezi wa ramadhani umekuwa ni mwezi mzuri wa kufanya toba na mambo mengine ya heri kwa wingi zaidi na yakakubaliwa kwa haraka kuliko miezi mingine. Tunafundishwa kwamba mashetani ibilisi na wakubwa wenzake wanafungiwa mwezi huu (nadhani ndiyo maana hata nafsi zinamkumbuka Mola kipindi hiki kwani vishawishi vikuu vya maasi havipo)
Watu kwa kuangalia ofa hizo wakaupachika jina mwezi "mtukufu wa ramadhani" kitu ambacho kiuhalisia si kweli. Kama tutaita mtukufu kwa maana hizi hizi za Kiswahili ni sawa lakini kama mtukufu itakuwa imelenga maana ileile ya sawa na ile miezi minne basi hapo itakuwa haifai! Kiswahili saa nyingine kinakosa misamiati!
Credit kwa Shk. Dr Tawakkal Hussein wa TV Imaan
Kuna watu wakiona heading kama hiyo tayari astaghfirullaah zinakuwa nyingi wakidhani labda nimepotosha. Twende pamoja kwa ufupi sana utanielewa
Kalenda wanayotumia waislamu (si kwamba mimi siyo mwislamu bali mimi na wenzangu baadhi tunaitumia ikikaribia ramadhan na ikikaribia arafa) ni kalenda ya kuhesabu siku kwa kutumia mzunguko wa mwezi mwandamo ambayo wengine wanaiita lunar calendar
Kwa mujibu wa kalenda hiyo miezi ni 12 katika mwaka na mwezi unakuwa na siku 30 au 29 basi! Nyongeza ya hilo mwaka unakuwa na siku 360 tu hazizidi.
Muḥarram (mfunguo nne)
Ṣafar (mfunguo tano)
Rabial-Awwal (mfunguo sita)
Rabial-Thāni (mfunguo saba)
Jamādal-Awwal (mfunguo nane)
Jumādal-Thāni (mfunguo tisa)
Rajab
Shaʿbān
Ramaḍhān
Shawwāl (mfunguo mosi)
Dhul-Qaʿadah (mfunguo pili)
Dhul-Ḥijjah (mfunguo tatu)
Miezi hiyo kwa Kiswahili wanaita mifunguo ambapo waswahili wanahesabu kama warabu yaani mwezi wa kwanza ni Shawwāl na wa mwisho ni Ramadhani (Kwahiyo kwa mujibu wa waswahili na waarabu ile siku ya idi baada ya ramadhan (idi ndogo) ndiyo siku ya kwanza ya mwaka yaani mwaka mpya. Kwa upande wa uislamu mwezi wa kwanza ni Muharram na wa mwisho ni Dhul Hijja (Kwahiyo ukiona mahujaji wanaenda makka vile ujue ndo tupo mwisho Mwisho wa mwaka)
Kama ilivyo kawaida mitume hawakuwa wakiondoa kila kitu tu walichokikuta bali kuna vingine waliamrishwa kuviendeleza na kuvienzi kama vilivyo ila kwa namna nzuri inayofuata sheria ya mwenyezi Mungu. Basi hata miezi Waarabu walikuwa wakiiheshimu ni minne na wakawa wanafanya ibada zao za tofauti ndipo mtume alivyokuja akaendeleza utukufu wa miezi ile kama ilivyokuwa ila kwa utaratibu wa Mwenyezi Mungu
Miezi hiyo Mitukufu ni
Dhul Qa'ada (Mfunguo pili)
Dhul Hijja (Mfunguo tatu)
Muharram (mfunguo nne)
Rajab
Ramadhan haimo!
Sikuachi hivi hivi ngoja nimwambie kwa nini watu wamezoea ramadhani ni mwezi mtukufu?
Ndani ya ramadhani kuna usiku mmoja tu (sehemu ya siku miongoni mwa siku za ramaḍhān wala si mwezi mzima wala si siku nzima) ambao usiku huo umetajwa kuwa ni bora kuliko miezi elfu. Maana yake ni kwamba mtu akifanya mema kwenye usiku huo itahesabika kama amefanya mema kwa miezi zaidi ya elfu. Vivyo hivyo kwa atakaye fanya maovu usiku huo ni sawa na aliyetumia miezi zaidi ya elfu kumuasi Mola.
Tunapata kwamba ni usiku mmoja tu ulio bora sana na hata hivyo haujaambiwa ni usiku mtukufu! Pia mwezi wa ramadhani umekuwa ni mwezi mzuri wa kufanya toba na mambo mengine ya heri kwa wingi zaidi na yakakubaliwa kwa haraka kuliko miezi mingine. Tunafundishwa kwamba mashetani ibilisi na wakubwa wenzake wanafungiwa mwezi huu (nadhani ndiyo maana hata nafsi zinamkumbuka Mola kipindi hiki kwani vishawishi vikuu vya maasi havipo)
Watu kwa kuangalia ofa hizo wakaupachika jina mwezi "mtukufu wa ramadhani" kitu ambacho kiuhalisia si kweli. Kama tutaita mtukufu kwa maana hizi hizi za Kiswahili ni sawa lakini kama mtukufu itakuwa imelenga maana ileile ya sawa na ile miezi minne basi hapo itakuwa haifai! Kiswahili saa nyingine kinakosa misamiati!
Credit kwa Shk. Dr Tawakkal Hussein wa TV Imaan