Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,658
- 4,866
Polisi wa Kidini nchini Nigeria wamekamata watu 11 siku ya Jumanne kwa kuonekana wakila chakula mchana katika mwezi wa Ramadhani.
Watu hao wamekamatwa katika jimbo la kaskazini la Kano.
Kano ina idadi kubwa ya Waislam, ambapo sheria ya kidini – Sharia- inatumika pamoja na sheria za kawaida za nchi.
Polisi wa Kiislam, maarufu kama Hisbah, hufanya misako katika maeneo ya chakula na masoko wakati wa Ramadhani.
Wanaume 10 na mwanamke mmoja waliokamatwa, waliachiliwa huru baada ya kuapa kuwa hawatoacha kufunga bila sababu muhimu.
“Tulikamata watu 11 siku ya Jumanne, akiwemo mwanamke mmoja muuza karanga aliyeonekana akila na watu wakatujulisha,” amesema msemaji wa Hisbah Lawal Fagge, akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC.
“Wengine 10 ambao ni wanaume walikamatwa mjini karibu na masoko ambapo kuna shughuli nyingi.”
Ameongeza kusema msako utaendelea lakini amesema wasio Waislam hawahusiki na msako huo.
Watu hao wamekamatwa katika jimbo la kaskazini la Kano.
Kano ina idadi kubwa ya Waislam, ambapo sheria ya kidini – Sharia- inatumika pamoja na sheria za kawaida za nchi.
Polisi wa Kiislam, maarufu kama Hisbah, hufanya misako katika maeneo ya chakula na masoko wakati wa Ramadhani.
Wanaume 10 na mwanamke mmoja waliokamatwa, waliachiliwa huru baada ya kuapa kuwa hawatoacha kufunga bila sababu muhimu.
“Tulikamata watu 11 siku ya Jumanne, akiwemo mwanamke mmoja muuza karanga aliyeonekana akila na watu wakatujulisha,” amesema msemaji wa Hisbah Lawal Fagge, akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC.
“Wengine 10 ambao ni wanaume walikamatwa mjini karibu na masoko ambapo kuna shughuli nyingi.”
Ameongeza kusema msako utaendelea lakini amesema wasio Waislam hawahusiki na msako huo.