tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,835
- 18,249
Naingia kwenye mada moja kwa moja nisiwachoshe na maneno mengi. Ukimsikiliza huyu mbunge kwa umakini utakubaliana nami pasi na shaka kwamba wabunge wa CCM walihongwa na kampuni ya DP World ili kuwauzia nchi. Inauma sana. Kumbe mkataba ulisainiwa tangu mwaka jana, sasa hawa wezi wanatuchora tu jinsi tunavyolalamika mitandaoni.
CCM ni Yuda Eskarioti, wametusaliti mchana kweupe!
Wakati watanzania tunapambana kila siku kujikusuru na umaskini, wabunge hawa wa CCM wamegeuka kuwa Yuda Eskarioti aliyemuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha. Uroho wa mali na uchumia tumbo ndivyo vinavyopewa kipaumbele kuliko utu na uzalendo kwa taifa. Hata kama wakituuza kwa hizo fedha kidogo wanadhani wataishi milele? Hawa wapuuzi wamelaaniwa sio bure.
Magufuli alaumiwe 100%
Haya yote yamesababishwa na Magufuli pale alipoamua kuchezea uchaguzi wa 2020. Ndio. Kama wabunge wa upinzani wangekuwemo bungeni huu upumbavu wa kuwauza watanzania kwa mabeberu wa kiarabu usingefanyika. Huko aliko Mungu anamuona. Kama kaburi lake lingekuwa halilindwi 24/7 tungeenda kulipiga fimbo.
CCM ni ukoo wa panya
CCM ni ukoo wa panya—babu mwizi, baba mwizi, watoto wezi, wajukuu wezi, vitukuu wezi, vilembwe wezi na vining’ina wezi! Ukoo huu wa panya walikuwa wanasafiri katika boti la muhogo, lakini kwa sababu ya uroho wao, walianza kulitafuna boti! Kilichofuata ni ukoo mzima wa kizazi cha panya kuzama na kuangamia.
Ukoo huu wa panya badala ya kuangamia peke yao wameona wagugune mtumbwi ili tuzame wote. Kuchumiia tumbo kwao limekuwa janga la taifa. Ni afadhali nchi hii iuzwe tugawene hela kila mmoja atafute nchi ya kwenda kuishi.
Hii nchi sio mahali pa kuishi tena; imegeuka kuwa shamba la wanyama. Katika shamba la wanyama inasemekana wanyama wote ni sawa lakini baadhi yao ni sawa kuliko wengine. Katika nchi hii ukoo wa panya (CCM) ni sawa kuliko wengine. Ndio maana kila kukicha wanauza rasilimali za taifa kwa bei ya kutupa bila soni.
CCM ni Yuda Eskarioti, wametusaliti mchana kweupe!
Wakati watanzania tunapambana kila siku kujikusuru na umaskini, wabunge hawa wa CCM wamegeuka kuwa Yuda Eskarioti aliyemuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha. Uroho wa mali na uchumia tumbo ndivyo vinavyopewa kipaumbele kuliko utu na uzalendo kwa taifa. Hata kama wakituuza kwa hizo fedha kidogo wanadhani wataishi milele? Hawa wapuuzi wamelaaniwa sio bure.
Magufuli alaumiwe 100%
Haya yote yamesababishwa na Magufuli pale alipoamua kuchezea uchaguzi wa 2020. Ndio. Kama wabunge wa upinzani wangekuwemo bungeni huu upumbavu wa kuwauza watanzania kwa mabeberu wa kiarabu usingefanyika. Huko aliko Mungu anamuona. Kama kaburi lake lingekuwa halilindwi 24/7 tungeenda kulipiga fimbo.
CCM ni ukoo wa panya
CCM ni ukoo wa panya—babu mwizi, baba mwizi, watoto wezi, wajukuu wezi, vitukuu wezi, vilembwe wezi na vining’ina wezi! Ukoo huu wa panya walikuwa wanasafiri katika boti la muhogo, lakini kwa sababu ya uroho wao, walianza kulitafuna boti! Kilichofuata ni ukoo mzima wa kizazi cha panya kuzama na kuangamia.
Ukoo huu wa panya badala ya kuangamia peke yao wameona wagugune mtumbwi ili tuzame wote. Kuchumiia tumbo kwao limekuwa janga la taifa. Ni afadhali nchi hii iuzwe tugawene hela kila mmoja atafute nchi ya kwenda kuishi.
Hii nchi sio mahali pa kuishi tena; imegeuka kuwa shamba la wanyama. Katika shamba la wanyama inasemekana wanyama wote ni sawa lakini baadhi yao ni sawa kuliko wengine. Katika nchi hii ukoo wa panya (CCM) ni sawa kuliko wengine. Ndio maana kila kukicha wanauza rasilimali za taifa kwa bei ya kutupa bila soni.